Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 30 April 2014

WAANDISHI WAFUNDWA KUHUSU UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU


Na Miza Kona (Maelezo), Zanzibar
TATIZO la Wananchi  kujichukulia hatua mikononi mwao na matumizi ya nguvu zisizo za lazima kwa baadhi ya vyombo vya dola ni changamoto kubwa inayodhoofisha utekelezaji wa haki za binadamu.
Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria Zanzibar Harusi Miraji Mpatani kwenye  mafunzo ya Haki za Binadamu yaliyoandaliwa kwa ajili ya Waandishi wa habari katika  Ofisi ya Kituo hicho  Migombani Mjini Zanzibar.
Amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kujichukulia sheria mikononi mwao  pale inapotokea tuhuma  inayopelekea kuwepo kwa uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
Amesema licha ya juhudi zinazochukuliwa katika kuhakikisha kuwa sheria ya haki za binadamu zinafikiwa kwa jamii,  bado matukio ya uvunjwaji na ukiukwaji  wa Haki za binadamu yanaendelea kutokea nchini.
“Watoto na walemavu wamekuwa ni wahanga wakubwa wa matukio ya unyanyasaji na udhalilishaji wa kingono, mbali na hali dhaifu ya kimaumbile waliyonayo bado jamii haijabadili mtazamo kuwa kundi hili linahitaji kulindwa kutokana na vitendo hivyo”, alifahamiisha Bi Harusi.
Aidha ameeleza kuwa waandishi wa habari wanawajibu katika kusimamia haki hizo kwa kutoa taaluma juu ya haki za binadamu kwa jamii wanayoifanyia kazi kwa kutumia vyema kalamu zao ili kujiepusha kuandika habari zinapelekea  uchochezi na kusababisha uvunjifu wa haki za binadamu.
Amewataka Waandishi kufuatilia bila ya woga matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu ili kuweza kuibua matukio mbali mbali ili sheria iweze kuzifanyia kazi na kuondosha matatizo hayo.
Mada nane zinatarajiwa kujadiliwa katika mafunzo hayo zikiwemo Ufafanuzi wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Haki za Binadamu na nafasi ya Waandishi wa habari katika kusimamia Haki za Binadamu, Utawala bora pamoja na Utawala wa Sheria.
Mafunzo hayo  ya siku mbili yametaarishwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  na yanawashirikisha waandishi wa vyombo mbali mbali  vya Habari vya Serikali na biinafsi nchini.

SERIKALI YASHAURIWA KUANGALIA SHULE YA ILBORU


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

SERIKALI imeombwa kuendelea kutenga fedha za ukarabati wa majengo kila mwaka kwa shule Ilboru iliyopo jijini Arusha ili kujenga mazingira mazuri mazuri ya kujifunzia na kufundishia yatakayofanya shule hiyo iweze kuonekana kama shule ya kipaji maalumu kwani majengo ya sasa yalijengwa toka mwaka 1946.
Hayo yalisemwa na mkuu wa shule ya sekondari hiyo Julius Shula alipokuwa akizungumza na wadau na wazazi katika mahafali ya 21 ya kidato cha sita yaliyofanyika shuleni hapo ambapo jumla ya wahitimu 153 walitnukiwa vyeti vyao.
Shula alisema kuwa serikali inapaswa kuendelea kutenga fedha za ukarabati kila mwaka haswa kwa shule kongwe zenye wanafunzi wenye vipaji maalum kiakili ili walau iweze kuwafanya wanafunzi hao kujituma zaidi kwa kuwa kuwepo kwa mazingira mazuri ya kujifnzia kunachangia hata wanafunzi kfanya vizuri katika masomo yao.
Alieleza kuwa shule hiyo imepata mafanikio makubwa katika eneo la ukarabati wa baadhi ya  majengo na miundombinu mingine baada ya serikali kutoa kiasi cha shilingi milioni 100 ambapo kupitia fedha hizo waliweza kukarabati mabweni sita pamoja na bwalo ambapo ukarabati huo umechangia sana kuongeza kiwango cha ufaulu shuleni hapo.
“Naishauri serikali yetu sikivu iendelee kutenga fedha za ukarabati wa majengo kwa kila mwaka ili kuzijengea mazingira ya kujifunzia na kufundishia hali hii itachangia sana kuwafanya wanafuzi wajitume zaidi katika kufanya vizuri katika masomo yao,” aliongeza Shula.
Alidai kuwa pamoja na shule hiyo kuwa na mafanikio ya kitaaluma lakini bado inakabiliwa na changamoto ya upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi hali inayosababisha shule kutafuta walimu wa muda ambao malipo yao ni makubwa sana kwa mwezi huku shule ikiwa haina uwezo wa kumudu gharama hizo.
Alitaja changamoto ingine kuwa ni pamoja na uchakavu mkubwa wa madarasa pamoja na nyumba za watumishi ambapo wanafunzi wanakosa mahali pazuri pa kujifunzia kutokana na uchakavu mkubwa wa madarasa huku nazo nyumba za walimu zikiwa zinakatisha tama kwa kuwa nyumba wanazoishi sio rafiki kabisa.

SHULE YATENGA SHS. 90 MILIONI KWA WANAFUNZI WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot.com, Arusha

SHULE ya Sekondari Edmund iliopo Sinon Mjini Arusha imetenga zaidi Shs. 90 milioni kwa wanafunzi 90 kila mwaka kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaotokea katika mazingira magumu huku lengo likiwa ni kuwaepusha na mimba za utotoni lakini pia uvunjifu wa amani kwenye jamii.
Fedha hizo zinatolewa na wafadhili wa nje ya nchi pamoja na mfuko wa shule hiyo ujulikanao kama Mfuko wa Edmund ambao pia huo unalenga kuhamasisha ufadhili wa ndani.
Hayo yameelezwa na Mkwabi Francis ambaye ni mkuu wa shule hiyo wakati akiongea na wanafunzi, wazazi pamoja na walezi wa shule hiyo kwenye maafali ya nane ambapo jumla ya wanafunzi 240 wanatarajia kuhitimu katika shule hiyo.
Mkwabi alisema kuwa mpango huo wa kuwasidia watoto wanaotokea katika mazingira magumu umeweza kuwanufaisha watoto wanaotokea katika vijiji vya Murieth, Mkono,Nadosoito,Unga Limited, na Sinoni ambapo walengwa ni wale wenye maitaji muhimu.
Alifafanua kuwa walengwa hao ni wale watoto wanaotokea katika familia ambazo hazina uwezo,na mayatima ambapo watoto hao huweza kukupewa ufadhili maalumu kwa ajili ya kusoma na kupata elimu ya Sekondari.
"Wafadhili wetu wakubwa wanatokea katika Nchi za Ausralia, Newzeland,Iland, na Marekani na hawa wanatufanikikishia hawa watoto 90 kuweza kupata elimu yao bora sana ya Sekondari ingawaje na sasa sisi tumejipanga kuhakikisha kuwa na sisi hapa hapa shuleni tunatoa ufadhili kwa watoto wetu ili siku hata kama tukikosa wafadhili basi tunaweza kusaidia jamii'aliongeza Mkwabi.
Pia alisema kuwa nao wazazi wanapaswa kujua na kutambua kuwa nao wana nafasi kubwa sana ya kuweza kuwasaidia watoto hasa wale ambao hawana uwezo wa kupata elimu ya sekondari kwani kupitia njia ya ufadhili wa ndani inawezekana kabisa 
"Kama wazazi, na walezi wakiwa na tabia ya kuchangia sekta ya maendeleo ya shule hasa mifuko ya shule  basi wataweza kusaidia jamii na hatutaweza kuwategemea zaidi wafadhili ambao wanatokea nje ya nchi kwani wakati mwingine wanapokatisha ufadhili wao wanasababisha watoto wawe kwenye hali ya uoga," aliongeza Mkwabi.
Wakati huo huo Wanafunzi wa shule hiyo ambao ni wahitimu waliwashauri walimu wa shule hiyo lakini pia wale wa shule nyingine kuachana na tabia ya kuwatenganisha wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha nne dhidi ya wale wa kidato cha tano na sita kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha wale wa vidato vya chini kutopata hamasa ya kujiunga au kufanya vema ili kuweza kujiunga na kidato cha tano na sita.

WANACHAMA 1,000 UVCCM MERU WAFUNGA BARABARA ARUSHA


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida vijana zaidi ya 1000 ambao ni wanachama wa umoja wa vijana chama cha mapinduzi (UVCCM)wilaya ya Meru mkoa wa Arusha wamevamia ofisi za chama hicho kuanzia ngazi ya Wilaya hadi mkoa huku wakidai kuwa Makao makuu ya chama hicho wamewaonea kwa kutangaza uamuzi wao wa kuwachagulia viongozi tofauti na matakwa yao ambapo wao walimchagua Kamanda wao ambaye Ni John Palangyo ila CCM makao makuu walitofautiana nao.
hataivyo maandamano hayo ambayo yaliratibiwa na wajumbe wa UVCCM Meru yaliweza kusababisha shuguli mbalimbali za chama hicho kuanzia ofisi ya Wilaya hadi Mkoa kusimama kwa kuwa wajumbe hao walilazimika kuingia kwa nguvu ndani ya ofisi hizo na kisha kushinikiza kusikilizwa kwa madai yao
Akiongea kwa niaba ya wajumbe hao mmoja wa wajumbe hao Joshua Mbwana "Mwarabu"alisema kuwa kilichosababisha waweze kufanya maandamano hayo ambayo yalianzia kuanzia eneo la Usa River Mpaka Arusha ni kuelezea umma kuwa wapo baadhi ya viongozi katika chama hicho ambao wanawachagulia viongozi wa kuwaongoza bila kuwauliza
"hivi juzi tulikuwa na tulimchagua kamanda wetu ambaye ni John Palangyo na tulimpitisha lakini baada ya jina kufika mkoani ghafa jina lilibadilishwa kama haitoshi makao makuu wakasema kuwa wana mtu wao sasa je wao ndio wanatuchagulia mtu wa kutuongoza au sisi kamwe hatutakubali na badala yake tutapigana hadi mwisho hii tabia imetucosha sana"aliongeza Joshua

wakati huo huo alidai kuwa endapo kama hali hiyo itaendelea kufanyika ambapo wananchi, wajumbe, na wanachama watachagua kiongozi alafu makao makuu pamoja na uongozi wa Mkoa wakakataa basi mapambano yatakuwa makubwa sana.
Kutokana na hilo mjumbe huyo alisema kuwa pamoja na kuwa wamevamia ofisi za CCM wakiwa wanachama zaidi ya 300 bado kama hawatapewa majibu yha kuridhisha juu ya kamanda wa vijana ambaye amechaguliwa kwa kura zote na wajumbe wa baraza hilo basi ndani ya siku nne kutoka sasa huenda wakaandamana hadi makao makuu ya ofisi za CCM
"Tumesharatibu maandamano hayo na yataenda vizuri itakuwa ni histori a kwa CCM kuchagulia viongozi kwa maslahi yao binafsi na matakwa ya viongozi wa ngazi za juu hasa wale ambao wana malengo ya kugombea nafasi za ubunge katika majimbo kwani ujumbe wetu ni lazima tutauweka wazi na kila mtu aweze kuosoma lakini hata kuingia ndani ya ofisi hizo bila taarifa wala kibali cha aina yoyote ile"aliongeza Joshua.
Hata hivyo, Katibu wa chama hicho Wilaya ya Meru, Langaeli Akyoo alisema kuwa mchakato wa kumpata kiongozi ambaye vijana hao wanamtaka ulienda vizuri na majina matatu yalifikishwa Dar es saalam makao makuu lakini baadaye hayakurudi kama ilivyoratarjiwa
Akyoo alisema kuwa majina mawili yalirudi majina mawili ambayo yana utata mkubwa ambapo utata huo ndio uliosababisha maandamano makubwa kuanzia Meru hadi Arusha.
"Jamani maombi yenu nimeyapata na ninapenda kuwaambia kuwa majina ambayo yalienda Dar es saalam makao makuu yalirudishwa mawili ambayo yana utata na wao walisema kuwa mchakato unatakiwa kuanza moja jambo ambalo sisi hatukubalini nalo kabisa"aliongeza Akyoo
Awali mwenyekiti wa umoja wa vijana Wilaya hiyo Bw Elirehema Mbisse alisema kuwa mchakato wa kumpata Kamanda huyo unaendelea na hivyo amewataka wawe na subira ili waweze kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo ambalo limesababisha ofisi za CCM  kusimamisha kazi kwa muda.
Uongozi wa Uvccm kupitia kikao chake cha kamati ya utekelezaji kilipendekeza majina matatu ambayo ni John .D. Palangyo, Sioi Solomoni Sumari, na Daniel Mirisho Palangyo,na baadaye muhtasari uliweza kupelekwa mkoani ambapo Mkoa ulijiridhisha na majina hayo na uliweza kuhoji na hatimaye waliweza kumpata John.D. Palangyo kama Kamanda wa Vijana Wilaya ya Meru, lakini baadaye barua ilikuja na kudai kuwa kamanda wa Meru siyo huyo jambo ambalo si la kweli.

AIRTEL YATOA MSAADA WA VIFAA VYA OFISI KWA SHULE YA MSINGI CHAU CHALINZE



Mobile phone company Airtel Through its Activities to social services has provided support for office supplies rice to School Based on the Ambient mu Chau Chalinze Coast Region
Speaking on behalf of Airtel Chief Sales coastal William Rocky said "today we are pleased to provide support to the chairs and tables in favor of the office of the teachers at the school here, this support is aimed at improving the office environment and enable teachers to do their jobs more effectively.

This is our continuity of service to the community, especially in the education sector where the project through our "our school" have enabled secondary schools to get textbooks and textbook fees and to the challenges of shortage of textbooks in schools. Parallel and books are also donated desks and office equipment as we do today in this school based on Chau
"We believe this will help bring productivity and improve the performance of work for teachers in school," added Rocky
In turn the head teacher of a primary school Chau master Elvin Msangi said "I appreciate very Airtel to reach schools here, this is yakwanza receive the help like this in school, so we feel comfortable to see a company like Airtel is doing a great job in supporting the education sector. We have many needs here at school, We hope this is the beginning so shall tumkumbuka in our program come in the future.
This support will enable teachers have good office and kuwaboreshea their working conditions have improved.
Airtel through its project of our school can enable various schools in profit and books, more than 900 school in the country have benefited from this project so far.

ASASI YA IRAWS – TANZANIA YAWASILISHA STADI JUU YA JINSI YA KUDHIBITI IDADI YA WAFUNGWA MAGEREZANI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

image
image_1 image_2 photo
Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali waliohudhuria Kikao hicho cha uwasilishaji wa Stadi juu ya jinsi ya kudhibiti idadi ya Wafungwa Magerezani. Kikao hicho kimefanyika  katika Ukumbi wa Luther House, leo Aprili 30, 2014 Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia) ni Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya IRaWS – TANZANIA, Kamishna Mkuu Mstaafu Magereza Nicas Banzi(wa pili kushoto) ni Mwenyekiti wa Asasi ya IRaWS – Tanzania, Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza Onel Malisa(wa kwanza kushoto) ni Afisa Mwandamizi Mstaafu wa Magereza, Bi Regina Thomas(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).


CHANZO,FULL SHANGWE 

SEMINA YA WAANDISHI KUHUSU UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU YAFANYIKA ZANZIBAR

PICT2016
Na Miza Kona Maelezo Zanzibar
TATIZO la Wananchi  kujichukulia hatua mikononi mwao na matumizi ya nguvu zisizo za lazima kwa baadhi ya vyombo vya dola ni changamoto kubwa inayodhoofisha utekelezaji wa haki za binadamu.
Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria Zanzibar HarusiMiraji Mpatani kwenye  mafunzo ya Haki za Binadamu yaliyoandaliwa kwa ajili ya Waandishi wa habari katika  Ofisi ya Kituo hicho  Migombani Mjini Zanzibar.
Amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kujichukulia sheria mikononi mwao  pale inapotokea tuhuma  inayopelekea kuwepo kwa uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu.
Amesema licha ya juhudi zinazochukuliwa katika kuhakikisha kuwa sheria ya haki za binadamu zinafikiwa kwa jamii,  bado matukio ya uvunjwaji na ukiukwaji  wa Haki za binadamu yanaendelea kutokea nchini.
“Watoto na walemavu wamekuwa ni wahanga wakubwa wa matukio ya unyanyasaji na udhalilishaji wa kingono, mbali na hali dhaifu ya kimaumbile waliyonayo bado jamii haijabadili mtazamo kuwa kundi hili linahitaji kulindwa kutokana na vitendo hivyo”, alifahamiisha Bi Harusi.
Aidha ameeleza kuwa waandishi wa habari wanawajibu katika kusimamia haki hizo kwa kutoa taaluma juu ya haki za binadamu kwa jamii wanayoifanyia kazi kwa kutumia vyema kalamu zao ili kujiepusha kuandika habari zinapelekea  uchochezi na kusababisha uvunjifu wa haki za binadamu.
Amewataka Waandishi kufuatilia bila ya woga matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu ili kuweza kuibua matukio mbali mbali ili  sheria iweze kuzifanyia kazi na kuondosha matatizo hayo.
Mada nane zinatarajiwa kujadiliwa katika mafunzo hayo zikiwemo Ufafanuzi wa katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Haki za Binadamu na nafasi ya Waandishi wa habari katika kusimamia Haki za Binadamu, Utawala bora pamoja na Utawala wa Sheria.
Mafunzo hayo  ya siku mbili yametaarishwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  na yanawashirikisha waandishi wa vyombo mbali mbali  vya Habari vya Serikali na biinafsi nchini.

CHANZO,FULL SHANGWE 


UKAWA RUKSA KUUNGURUMA LEO ZANZIBAR


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.

Dar es Salaam. Hatimaye mkutano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), uliokuwa umezuiwa kupisha sherehe za Muungano utafanyika leo katika Viwanja vya Kibandamaiti, Unguja baada ya kupata baraka za polisi.

Mkutano huo awali ulikuwa ufanyike Aprili 19, mwaka huu lakini ukazuiwa na polisi kwa maelezo kuwa intelijensia yao ilionyesha kuwa kungekuwa na tishio la maisha ya watu. Hivyo walishauriwa wapange tarehe nyingine baada ya Sikukuu ya Pasaka.
Hata Aprili 23 ambayo ilikuwa imepangwa kufanyika kwa mkutano huo, ilikataliwa na polisi kwa madai kwamba askari na maofisa wa jeshi hilo walikuwa Dar es Salaam katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano yaliyofanyika Aprili 26, mwaka huu.
Msemaji wa Polisi Zanzibar, Mohamed Mhina amethibitisha kuruhusiwa kwa mkutano huo na kuwataka wananchi watakaohudhuria kuwa watulivu kabla na baada ya mkutano.
“Tumewaruhusu kufanya mkutano huo lakini maandamano hayataruhusiwa kufanyika,” alisema Mhina.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Julius Mtatiro alisema mkutano huo utakaoanza saa 8 mchana hadi saa 12 jioni, utahudhuriwa na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF, Freeman Mbowe na Dk Willibrod Slaa wa Chadema, Mchungaji Christopher Mtikila wa DP na Dk Emmanuel Makaidi wa NLD.
Wengine ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, wawakilishi 10 kutoka kundi la 201 na wanachama mbalimbali kutoka umoja huo.
“Tunakwenda kuwaelimisha wananchi nini maana ya Katiba, jinsi ya kulinda maoni yao waliyoyatoa yasichakachuliwe na kuwaeleza kwa nini tuliamua kutoka bungeni,” alisema Mtatiro na kuongeza:
“Kesho (leo) tunafanya mkutano Unguja na keshokutwa (kesho) Pemba na tutatoa ratiba ya mikutano mbalimbali itakayofanyika Tanzania Bara kwa makundi tofauti.” Aprili 16 mwaka huu, Ukawa wakiongozwa na Profesa Lipumba walisusia Bunge la Katiba na kutoka nje kwa madai ya kutokuridhishwa na mienendo ya mjadala ya Bunge hilo.
Baada ya kutoka bungeni, walitangaza kufanya mikutano nchi nzima wakianzia Zanzibar.
CHANZO, MWANANCHI

MAANDAMANO KUHUSU WASICHANA WALIOTEKWA

 Maandamano kuhusu wasichana waliotekwa

Maandamano makubwa ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Nigeria- Abuja baadaye leo watu wakiitaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwanusuru wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislam .

Wasichana hao walichukuliwa kutoka shule yao ya malazi iliyopo katika eneo lisiloweza kufikiwa kwa urahisi kaskazini mashariki mwa nchi zaidi ya wiki mbili zilizopita.

Waandalizi wa maandamano hayo wanaita serikali kuelekeza juhudi zao kwa wasichana waliopotea .

Mpango ni kuandamana hadi bungeni na kwa mshauri wa taifa wa masuala ya usalama na kuwasilisha barua ya kutoa wito wa kufanyika kwa juhudi zaidi kuwanusuru wasichana hao.

Mwanaharakati mmoja wa kijamii amesema katika nchi nyingine yoyote ile suala la kutekaji nyara wa wasichana hao wengi lingekuwa ni mjadala wa kila siku .

Lakini serikali ya Nigeria imekuwa ikikabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kukaa kimwa huku wazazi wenye shauku wakisailia kuwa gizani kuhusu nini kinachoendelea kuhusiana na wasichana wao.

Huenda kwa kuhisi hilo rais wa Seneti , David Mark, sasa amezungumza. Amewatolea wito watekaji kuawaachilia mara moja wasichana bila masharti na akasema bila shaka taifa letu liko vitani .

CHANZO, BBCSWAHILI


SUDAN K.KUJUA HATIMA YAKE KATIKA EAC LEO


Mkutano wa jumuiya ya Afrika Mashariki waanza leo Tanzania

Mkutano wa kumi na mbili wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaaanza rasmi hii leo mjini Arusha nchini Tanzania.

Miongoni mwa maswala muhimu yatakayojadiliwa ombi la Sudan Kusini kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

Mkutano wa mwisho kama huu uliofanyika mjini Kampala Uganda mwezi Novemba mwaka jana, uliweka bayana kwamba ni katika mkutano huuu wa Arusha, ambapo tarehe ya Sudan Kusini kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki itakapotangazwa.

Lakini wadadisi wanasema kuwa msukosuko wa kiuchumi pamoja na vita vya wenyewe kwa wenyewe huenda ikawa sababu ya taifa hilo kunyimwa uanachama wa jumuiya hiyo. Hii ni baada ya machafuko ya wenyewe kwa wenyewe kuzuka, na kusambaratisha nchi hiyo kisiasa na kiuchumi.

Maswala mengine yatakayojadiliwa ni ripoti ya mawaziri, mikakati ya kifedha katika kuiendesha jumuiya hiyo na mbinu za nchi wanachama kuendelea kupeana taarifa za kijasusi, katika juhudi za kupambana na tishio la ugaidi.

CHANZO, BBCSWAHILI. 

WARIOBA AWATAJA WASALITI WA NYERERE


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.

Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji JosephWarioba amesema wanasiasa wanaomtuhumu kwa kumsaliti Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuhusu Muungano, ndiyo wasaliti kwa kuwa waliingiza kwenye Katiba, mambo yanayokinzana na makubaliano ya Muungano huo.


Jaji Warioba amesema usaliti huo ni pamoja na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuondoa mamlaka ya Bunge la Muungano katika utungaji wa sheria, kuitambua Zanzibar kuwa nchi inayojitegemea na kuongeza mambo ya Muungano bila kufuata Katiba.
Ametoa kauli hiyo kujibu mwendelezo wa lugha za kejeli na matusi anazorushiwa na baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wengi kutoka CCM na baadhi ya viongozi wa Serikali baada ya Tume aliyoiongoza kupendekeza muundo wa serikali tatu.
Akizungumza juzi usiku katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV, Jaji Warioba alisema viongozi wa pande mbili za Muungano wanaomtuhumu, ndiyo waliouvuruga Muungano huo
“Mwalimu aliacha Bunge likiwa na mamlaka kamili, aliacha nchi ni moja, aliacha mambo ya Muungano 11 sasa yamekuwa ni 22, kwa bahati nzuri Rais Jakaya Kikwete alieleza bungeni hilo kwamba mambo hayo yaliongezekaje,” alisema na kuongeza:
“Katika kubaini kuongezeka kwa mambo ya Muungano ndivyo ilikuwa inapunguza mamlaka kwa Zanzibar, mambo 11 yaliyoachwa na mwalimu yaliingizwa kikatiba lakini haya yaliyoongezeka yalipatikana kienyeji.”
Jaji Warioba alisema enzi za uhai wake, Mwalimu Nyerere aliheshimu na kuilinda Katiba hivyo, walioivunja ndiyo wasaliti wa Muungano.
“Sasa kati ya mimi na wao ni nani msaliti kwa Mwalimu, angekuwapo (Mwalimu) ni yupi angeonekana msaliti wa Serikali ya Muungano? Wao ndiyo wameuvuruga, alichokiacha Mwalimu ni tofauti na kinachoonekana kwa sasa,” alisema Jaji Warioba.
Kuhusu Bunge
Jaji Warioba alisema mipango mingi ya maendeleo inayopangwa ndani ya Bunge la Muungano inatekelezwa upande wa Bara pekee.
“Si hivyo tu, Bunge hilo linajadili mambo ya Bara tu na halihusishi upande wa Zanzibar. Zanzibar nayo inajadili mambo yake na kujiamulia lakini jina la Bunge hilo ni Muungano,” alisema Jaji Warioba.
Kutokana na mazingira hayo, Jaji Warioba alisema Zanzibar iliamua kuondoa mamlaka ya Bunge hilo katika utungaji wa sheria kupitia Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
“Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema sheria zinazotungwa katika Bunge hilo zitatumika ndani ya pande zote za Muungano, lakini Zanzibar wakabadilisha hilo kupitia Katiba yao wakasema sheria zote zitakazotungwa ndani ya Bunge hilo, lazima zipitiwe tena na Baraza la Wawakilishi,” na kuongeza: “(Zanzibar) Hawakuishia hapo, wakafanya mabadiliko ya Katiba mwaka 2010 iliyovunja Katiba ikiitambua Zanzibar kama nchi kamili, ikaondoa mamlaka ya Rais wa Jamhuri kugawa wilaya na mikoa kwa Zanzibar tofauti na Katiba ya Muungano, kwa maana hiyo Zanzibar ikavunja nguvu ya Bunge la Muungano.”
Aidha, alisema hatua hiyo ilionekana kuuvunja Muungano kwa vitendo baada ya kuvunja mamlaka ya Rais na kutambua marais kamili katika nchi mbili tofauti.
“Kwa kawaida nchi inakuwa na amri jeshi mkuu mmoja ambaye anapigiwa mizinga 21, Jeshi la Muungano linapiga mizinga kwa marais wawili kitu ambacho hakiwezekani,” alisema.
Malalamiko ya Watanganyika
Jaji Warioba alisema Kwa upande wa Tanzania Bara, walibaini malalamiko ya Watanganyika kuwa ni pamoja na kukosa fursa mbalimbali ndani ya Zanzibar. “Watu wa bara nao wanasema Zanzibar inashiriki Bunge la Muungano, inakagua miradi ya bara na kuihoji lakini wao hawana nguvu ya kushiriki mambo hayo kwa upande wa Zanzibar,” alisema.
Aliongeza: “Mbaya zaidi wanasema Wazanzibari wanaweza kumiliki ardhi na kupata uraia kwa upande wa bara lakini haki hizo haziwezi kupatikana kwa Mtanganyika, njia pekee tukaona ni vyema Zanzibar nayo ilete mambo yake ndani ya Muungano lakini ikashindikana.”
Hoja ya takwimu
Jaji Warioba aliwataka wajumbe wa Bunge wasihangaike na takwimu badala yake wajibu maswali yaliyojitokeza kutoka kwa washirika wa Muungano.
“Takwimu siyo tatizo, sisi hatukufanya jambo jipya, ila ilikuwa ni kama marudio tu ya Tume ya Nyalali, wanahoji takwimu hizo je, hawakuona dosari kwa takwimu za maoni ya asilimia 20 kwa jaji Nyalali?
Alisema Tume yake ilizunguka nchi nzima ikiwa na waandishi waliorekodi kwa tepu, video na maandishi kwa ajili ya kuweka kumbukumbu katika mtandao wa Tume.
 CHANZO, MWANANCHI


UCHAGUZI IRAQ


Uchaguzi kufanyika Iraq

Wapiga kura nchini Iraq wanashiriki katika zoezi la upigaji kura katika mikoa yote isipokuwa mkoa mmoja katika uchaguzi wa kwanza wa wabunge tangu wanajeshi wa Marekani waondoke nchini humo mwaka 2011.


Waziri mkuu wa sasa Nouri al-Maliki anagombea kiti chake kwa muhula wa tatu lakini kampeni zimekuwa zikipigwa kwa misingi ya vurugu za kisiasa zinazoendelea kukithiri nchini humo.

Selikali ya muungano ya bwana Maliki inayoongozwa na chama cha Kishia imekabiliwa na wakati mgumu kupambana na uasi unaongozwa na kundi lenye ufungamano na Al Qaeda katika mji wa Falluja na mkoa wa Anbar.

Sauti za mizinga zimekua taswira ya kila siku katika baadhi ya maeneo ya Iraq wakati kampeni za kuelekea uchaguzi huu.

Matokeo yake ni mashambulio ya kujitolea mhanga karibu kila siku.


Helikopta za kijeshi zinashika doria katika anga ya Baghdad na serikali imefunga uwanja wa ndege na baadhi ya barabara kuu ndani na nje ya mji huo.

Hatua hizo zinanuia kuwapa imani wapigaji kura watakaojitokeza kwani ni bayana kuwa huenda vituo vya kupigia kura vikalengwa.

Watu 160 wameuawa wiki iliyopita huku wengine 275 wakijeruhiwa.

Baadhi ya taarifa zinaeleza kuwa vikosi vya usalama vimepoteza maafisa elfu moja mwaka huu kwenye mapigano ya kukabiliana na uasi katika maeneo ya Fallujah na Anbar.

Inatabiriwa kuwa huenda Bw Maliki akashinda awamu ya tatu na kumuwezesha kuunda serikali ya muungano lakini ni bayana kuwa swala la usalama litasalia kuwa changamoto kubwa.

CHANZO BBCSWAHILI