Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 28 April 2014

MCHUNGUZI WA UMOJA WA ULAYA AACHILIWA


Mchunguzi wa Umoja wa Ulaya aachiliwa huru

Mmoja wa wachunguzi wa muungano wa Ulaya waliokamatwa na wanamgambo wanaotaka kujitenga ambao wanaiunga mkono Urusi ameachiliwa huru katika mji wa Sloviansk nchini Ukraine.
 Msemaji wa kundi hilo ameiambia BBC kwamba mwanamme huyo anayeaminika kuwa raia wa Sweden-aliachiliwa huru kwa misingi ya kiafya.

Mwangalizi huyo kutoka Sweden anayeaminika kuugua ugonjwa wa kisukari alionekana akisafirishwa kwa gari la Shirika la usalama na ushirikiano la mataifa ya Ulaya OSCE .
Lakini wenzake saba bado wanazuiliwa huku juhudi za kidplomasia kujaribu kuwakomboa zikiendelea.

Awali waangalizi hao walionyeshwa kupitia vyombo vya habari vya habari
.
Mmoja wao ambaye ni Kanali kutoka Ujerumani , Axel Schneider, amesema waangalizi hao walikua katika harakati za kidiplomasia na hawakuwa na silaha.

Shirila hilo la OSCE lina kundi kubwa la waangalizi nchini Ukraine ambao walikubaliwa na Urusi, lakini waangalizi hawa ni kutoka nchi kadhaa za shirika hilo waliokwenda nchini Ukraine kwa mwaliko wa serikali.


CHANZO, BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment