Kikosi cha Yanga cha mwaka 1994. Kutoka kushoto waliosimama ni Salum Kabunda 'Ninja', Constantine Kimanda, Steven Casmir Nemes, Kenneth Pius Mkapa, Selemani Mkati. Waliochuchumaa kutoka kushoto ni Nico Bambaga 'Machine', Sekilojo Chambua, Edibily Lunyamila, James Tungaraza 'Boli Zozo', na Said Mwamba 'Kizota'.
Na Daniel
Mbega
YOUNG
Africans, ambayo mwaka 1993 iliteswa sana na wapinzani wake wa jadi, Simba,
baada ya kutamba misimu miwili ya nyuma, hatimaye Jumamosi Februari 26, 1994
iliingia kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakabili ‘wanyama hao wakali’
wa Msimbazi, ambao mwaka huo walikuwa wameongeza makucha yao kwa kuwasajili
wachezaji mahiri na wauaji wa mabingwa hao watetezi wa Tanzania Bara, Yanga.