Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 30 January 2017

RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA KATIKA KUTANGAZA JINA RASMI LA KITUO CHA AMANI NA USALAMA KILICHOPEWA JINA LA MWALIMU JULIUS NYERERE KATIKA MAKAO MAKUU YA UMOJA WA AFRICA (AU) ADDIS ABABA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na viongozi wa mataifa mabalimbali wakiwa katika picha ya pamoja katika jengo jipya la kituo cha  Amani na Usalama (JULIUS NYERERE) lililopo katika Makao makuu ya Umoja wa Afrika Addis Ababa nchini Ethiopia.

MAKATIBU WAKUU WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NA WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI WATEMBELEA MPAKA WA TUNDUMA/NAKONDE



Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda (kushoto), akiwa pamoja na Mkuu wa wilaya ya Momba mkoani Songwe, Bw. Juma Irando (katikati), na maafisa kadhaa wa Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Viwanda, Biashara naUwekezaji, wakitoka katika Ofisi za Mkurugenzi wa Mji wa Tunduma kuelekea mpakani mwa Tanzania na Zambia eneo la Tunduma na Nakonde.

MLIMBWENDE WA SHINDANO LA MISS KIBOSHO 2017 JIJINI MWANZA APATIKANA.

Baada ya mtifuano mkali wa kumtafuta mlimbwende wa shindano la MISS KIBOSHO 2017 kufanyika kwa mara ya kwanza usiku wa ijumaa Januari 27, 2017 na jana jumamosi Januari 28,2017 katika Ukumbi wa Kibosho Luxury Bar Kiseke Ilemela Jijini Mwanza, hatimaye mshindi amejulikana.

AFRICA GRADUATE UNIVERSITY CHAWATUNUKU PhD WANAOFANYA KAZI ZA JAMII NCHINI

Mkuu wa Chuo cha Africa Graduate cha jijini Dar es Salaam, Profesa Steven Nzowa, akiongoza mahafali ya kuwatunuku Tuzo ya Heshima ya Udaktari (PhD) wanaharakati na watumishi wa mungu nane pamoja na wengine kadhaa waliotunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili HDD Dar es Salaam jana.

UONGOZI WA BODABODA MKOANI MWANZA WAPONGEZA ZOEZI LA UKAGUZI WA POLISI

Binagi Media Group
Umoja wa waendesha bodaboda mkoani Mwanza umepongeza zoezi la ukaguzi wa vyombo hivyo linaloendeshwa na jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani.

WATANZANIA WAOMBWA KUMUUNGA MKONO RAIS DK.JOHN MAGUFULI

 Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa nchini, John Shibuda (katikati), akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kuuaga mwaka wa 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 Dar es Salaam jana. Kulia ni Msajili Msaidizi Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ADA na Waziri wa Nchi asiye na Wizara Maalum, Zanzibar.

Thursday 26 January 2017

NAIBU WAZIRI ELIMU MHANDISI MANYANYA AFANYA ZIARA MKOANI SINGIDA NA KUHAMASISHA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI YA WATU WAZIMA

Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Mhandisi Stella Manyanya akiwasili katika halmashauri ya Wilaya ya Singida ambapo alipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Singida Eliya Digha.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI MASAUNI MPAKANI TUNDUMA KUKAGUA SHUGHULI ZA UINGIAJI NA UTOKAJI WA WAGENI NA RAIA

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisaini daftari la wageni baada ya kuwasili wilayani Momba Mkoani Songwe, kwa lengo la  kutembelea na kukagua uingiaji na utoakaji wa raia na wageni katika mpaka wa Tunduma unaotoa huduma kwa watu wanaoingia na kutoka katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afika Kusini, Namibia na DRC Congo.Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Momba, Juma Irando. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

DOKTA NCHIMBI AHIMIZA KILIMO CHA MUHOGO ILI MKOA WA SINGIDA UWE MZALISHAJI MKUBWA WA ZAO HILO NCHINI

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (mwenye kitambaa cha pink) akisaidiwa kuvuna muhongo aliozawadiwa na mkulima wa kijiji cha Mwankonko Manispaa ya Singida Gideoin Itambu juzi alipofanya ziara katika Manispaa ya Singida kukagua shughuli za kilimo.

WAANDISHI WA HABARI WAPATA SEMINA KUHUSU MAHINDI YA GMO NA MATUMIZI YA BIOTEKNOLOJIA KATIKA KILIMO

 Mshauri mstaafu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAM), Dk.Nicholas Nyange, akitoa mada kwa waandishi wa habari kuhusu matumizi ya Bioteknolojia katika matumizi ya kilimo walipotembelea kituo cha utafiti wa kilimo cha Makutupora mkoani Dodoma.

BENKI YA DUNIA YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUKUZA UCHUMI

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (wa Pili kutoka kulia) akisisitiza jambo wakati wa alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia ukanda wa Afrika Bw. Makhtar Diop, makao makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar salaam.

WASANII 400 WA AFRIKA KUTIKISA TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA ZANZIBAR 2017

Mkurugenzi wa tamasha la Sauti za Busara Bw.Yusuf Mahmoud akionesho moja ya kitabu chenye mambo lukuki yahuso tamasha hilo pamoja la habari mbalimbali za wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo la aina yake kwa wakazi wa Zanzibar na wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali za nchi na nje.

TANESCO YAWATOA HOFU WATEJA WAKE, YASEMA GRIDI YA TAIFA IKO SALAMA


Kaimu Meneja Mwandamizi udhibiti mifumo ya umeme TANESCO makao makuu, Mhandisi Abubakar Issa,(katikati), akionyesha kifaa kilicholipika (female connector), cha umeme wa 132kv kutoka Ubungo kwenda Chalinze. Kulia ni KaimunMeneja Uhusiano, Bi. Leila Muhaji na kushoto ni mwangalkizi mkuu wa kituo cha kupoza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam, Bw. Deodatus Ngwanda.

BILIONI 13.1 KUTUMIKA KUGHARIMIA MIRADI YA MAENDELEO SINGIDA

Mkurugenzi Bravo Kizito Lyampembile (wa kwanza kushoto) na Meya Manispaa ya Singida, Chima Gwae (katikati) wakitiliana saini mkataba wa mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 5.75 za mjini hapa kwa kiwango cha lami,na mwakilishi wa kampuni ya China Henan Internatioanl Co operation Ltd ya jijini Dar es salaam, Bi. Zephyr Liu. Ujenzi huo utagharimu zaidi ya shilingi 13.1 bilioni ambazo zimetolewa na benki ya dunia.

Na Nathaniel Limu, Singida
Halmashauri ya manispaa ya Singida inatarajia kutumia zaidi ya shilingi 13.1 bilioni, kwa ajili ya kugharamia miradi mitatu ya uimarishaji miji (ULGSP) inayogharamia na benki ya dunia.

VIDEO – THE MIGTHY ELEPHANT WAITOA MAJI MAJI FA CAP KWA 5 – 4,WAMTESA MCAMEROON WA MAJI MAJI KWA PENATI.

Timu ya Maji Maji imetolewa katika mashindano ya kombe la shirikisho la azam na THE MIGHTY ELEPHANT kwa penati 5 kwa 4.Tizama vijana wa The Migthy Elephant walivyomtesa golikipa wa Maji Maji ambaye ni mCameroon .

 

KAMA ULIPITWA NA HII,TUMEKUSOGEZEA HIGHLIGHTS ZA MCHEZO WA MAJIMAJI VS YANGA KATIKA MCHEZO ULIOCHEZWA UWANJA WA MAJI MAJI SONGEA

WAKUU WA WILAYA WATEMBELEA SHAMBA LA JARIBIO LA MAHINDI LA KITUO CHA MAKUTUPORA MKOANI DODOMA

 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine (kushoto), akizungumza na wakuu wa wilaya za Dodoma na maofisa watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa na wadau wa kilimo  alipotembelea shamba la Jaribio la Mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) chini ya Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (WEMA) katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha  Makutupora mkoani Dodoma leo.

Monday 23 January 2017

NAIBU WAZIRI MASAUNI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI JIJINI MBEYA

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisalimiana na maafisa wa Jeshi la Polisi alipowasili Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi ikiwa na lengo la kubaini mafanikio na changamoto za jeshi hilo. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Friday 20 January 2017

DENMARK KUHAMASISHA WAWEKEZAJI KUJA KUWEKEZA TANZANIA


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (wa kwanza kulia), akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na ujumbe kutoka nchini Denmark, ukiongozwa na Waziri wa nchi anayeshughulikia Sera, Bw. Martin Hermann, walipokutana Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es salaam.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI SITA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha Emanuel Nchimbi kuwa Balozi Nchini Brazili, Ikulu jijini Dar es Salaam.

NAIBU WAZIRI MASAUNI AIONGOZA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA KUTEMBELEA GEREZA LA KILIMO SONGWE

Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimpokea Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Kanali Mstaafu Masoud Ally (wapili kushoto), wakati wa ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na Gereza la Kilimo Songwe, wilayani Mbalizi, mkoani  Mbeya. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

MZUNGUKO WA TANO WA AZAM SPORTS FEDERATION CUP KUENDELEA JUMAMOSI HII

Raundi ya tano ya mechi za kuwania Kombe la Shirikisho la Azam 2016/17 (Azam Sports Federation Cup - ASFC), utaanza Jamamosi Januari 21, 2017 kwa timu za Majimaji na Mighty Elephant za Songea kucheza kwenye Uwanja Majimaji mjini Songea.

SKIPPERS HAVEN: HOTELI ILIYOSHEHENI MICHEZO LULUKI YA BAHARINI

 Na Jumia Travel Tanzania

Unaweza usiamini kwamba ile michezo ya baharini unayoiona kupitia kwenye runinga, wazungu wakiicheza unaweza ukaifanya ukiwa hapahapa nchini Tanzania. Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukujuza kuwa hoteli ya Skipper’s Haven iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam, inayo michezo kadhaa ya baharini ambayo itakustaajabisha.

SERIKALI KUANGALIA UPYA KANUNI ZA TAFITI ILI ZIWEZE KUFANYA KAZI KWA WAKATI

 Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi,  Charles Tizeba (kushoto), akizungumza na watafiti wa kilimo na wanahabari (hawapo pichani), wakati alipotembelea shamba la jaribio la mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya uhandisi jeni chini ya mradi wa Wema katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Makutupora mjini Dodoma leo. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk.Hassan Mshinda.

Thursday 19 January 2017

KAMPENI MAALUM YA KUINUA MAADILI KITAIFA JAN - DEC, 2017

Kiongozi wa Kampeni ya Kuinua Maadili Kitaifa Bi Mayrose Kavura Majinge, siku ya Jumamosi Jan 14, ameweza kushirikiana na wadau mbali mbali jijini hapa Washington kwa lengo la kuinua Maendeleo Maalum ya Maadili Kitaifa, yaliyoanza rasmi kufanyika mwezi huu Januari hadi Disemba 2017, kwa lengo la kuinua na kudumisha maadili ya Watanzania ili kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazodhoofisha mfumo wa muundo wa jamii yetu ya Kitanzania.

DKT. MPANGO AZINDUA JINA NA NEMBO MPYA YA KIBIASHARA YA BENKI YA POSTA TANZANIA

Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (Tpb Bank Plc), Bw. Sabasaba Moshingi, akitoa hotuba ya mafanikio ambayo Benki yake imeyapata katika biashara ya Sekta ya Fedha ikiwemo kukuza mtaji, kupata faida na kufanikiwa kubuni Jina Jipya na Nembo Mpya ya Kipepeo, itakayoanza kutumika kuanzia leo Januari 19,2017, baada ya kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es salaam

SERIKALI YAONYA WAWEKEZAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO


Na Woinde Shizza,Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua wawekezaji wanaochochea migogoro katika wilaya ya Ngorongoro na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kuchangia kuzorota kwa shughuli za maendeleo.
Gambo ameyasema hayo katika ziara yake wilayani Ngorongoro inayolenga kutatua migogoro wa pori tengefu lenye ukumbwa wa kilomita za mraba elfu kumi na tano ambapo amekutana na wadau mbalimbali ikiwemo wawekezaji, wafugaji pamoja na viongozi wa kiserikali.

WAKUU WA MASHIRIKA YA UMEME KUTOKA NCHI KUMI ZA AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA ARUSHA KUJADILI NAMNA YA KUUNDA MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME KWA NCHI HIZO


Na Woinde Shizza,Arusha

Wakuu wa  mashirika umeme kutoka katika nchi kumi za Afrika zinazozalisha
umeme(Eastern Africa Power pool(EAPP)          zimekutana  jijini arusha
kwa malengo ya kujadili mfumo wa usafirishaji wa umeme ikiwa ni pamoja na
namna wananchi wao watakavyoweza pata nishati ya umeme kwa uraisi tofauti
na sasa

Hayo yalisemwa na naibu katibu mkuu wizara ya nishati na madini Dkt.Juliana
palangyo alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wakuu wa
mashirika ya umeme katika nchi hizo za Eastern Africa Power
Pool (EAPP) mapema leo.

NYOTA AIRTEL WATAWALA LIGI YA WANAWAKE, MECHI MBILI KUCHEZWA KESHO

Wakati Ligi Kuu soka ya Wanawake ikitarajiwa kuendelea kesho Ijumaa Januari 20, 2017 kwa michezo mitano, wachezaji 19 kati 25 bora walioteuliwa katika mradi wa kuibuka na kukuza vipaji vya soka wa Airtel (Airtel Rising Stars), wametawala katika klabu zinazoshiriki michuano hiyo, inayoendelea.

OMBI LA ZANZIBAR KUJADILIWA CAF


Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limepitisha ombi la Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) la Zanzibar kuwa mwanachama kamili wa CAF. Katika kikao chake cha Kamati ya Utendaji kilichoketi Januari 12, mwaka huu kiliamua kupitisha ombi hilo kuwa moja ya ajenda za Mkutano Mkuu wa CAF utakaofanyika Machi 16, 2017 huko Addis Ababa, Ethiopia.

FIFA YAMTEUA MALINZI MJUMBE KAMATI YA MAENDELEO

Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maendeleo ya soka ya FIFA kwa miaka minne ijayo. Uteuzi huo unaanza mwaka huu 2017 hadi 2021.

NAIBU WAZIRI MASAUNI AKUTANA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA JIJINI MBEYA

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akijibu maswali yaliyoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika leo jijini Mbeya.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kanali Mstaafu Masoud Ally.( Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

WIMBO MPYA WA ASILI WENYE VIONJO VYA KISASA KUTOKA KWA SEKO BWAY-NZUGWI

Pata fursa ya kusikiliza wimbo mpya wa asili ya kisukuma kutoka kwa mwanamuziki Seko Bway. Wimbo unaitwa Nzugwi na umeimbwa kwa vionjo vya muziki wa kisasa. Umetengenezwa na King Fenya kutoka Mbunda Records ya Jijini Mwanza.
Bonyeza hapa kusikiliza

KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA MAKAO MAKUU YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, MPINGO HOUSE

 Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhandisi Atashasta Nditiye baada ya kuwasili makao makuu ya Wizara hiyo Mpingo House Jijini Dar es Salaam jana huku akiongozana na wajumbe wa kamati hiyo.

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 300 ZILIZOKUWA ZIENDE KWA KWA WAKANDARASI


 Image may contain: 1
person, phone and indoor


Na Woinde Shizza,Arusha
Halmashauri ya jiji la Arusha imeokoa zaidi ya shilingi  milioni mia tatu
sitini na nne  zilizokuwa zitumike kwa ajili ya kuwapa wakandarasi  kwa ajili ya kujenga madarasa  baada yake  kamati za shule kupewa jukumu la kusimamia ujenzi wa madarasa hayo badala ya mkandarasi.

WAFANYABIASHARA WAILALAMIKIA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA ,WAPINGA NOTISI WALIYOPEWA

Image result for WAFANYABIASHARA WA MADUKA ARUSHA

Na Woinde Shizza, Arusha


WAFANYABIASHARA wa maduka jijini Arusha,wameilalamikia halmashauri hiyo ,wakipinga notisi ya miezi mitatu waliopewa ,inayowataka kuondoka katika maduka hayo,ifikapo Machi 30,mwaka huu, kufuatia maduka yao kudaiwa kumilikiwa ma madalali na hivyo kuikosesha  mapato halmashauri hiyo.

SHIRIKA LA UNDER THE SAME SUN LATOA ELIMU KWA WADAU KUHUSU UALIBINO JIJINI MWANZA.

Afisa Maendeleo ya Jamii mkoani Mwanza Isaac Ndassa, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, kwenye ufunguzi wa semina kwa wadau wanaosaidia kutokomeza ukatili dhidi ya watu wenye ualibino, inayofanyika kwa siku nne kuanzia leo Jijini Mwanza. 

MADIWANI WA MANISPAA YA MOSHI WATEMBELEA OFISI ZA MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA)

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akizungumza wakati wa ukaribisho wa Madiwani wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi walipotembelea ofisi za mamlaka hiyo.

WASICHANA WANNE WA TANZANIA WAENDA KUPATA MAFUNZO YA UONGOZI, UTAMADUNI AFRIKA MASHARIKI NA KATI


 Wasichana wanne wa Tanzania wakiaga  kwa kupungia mikono huku wakiwa na , Bendera ya Taifa waliyokabidhiwa na Kamishna Mkuu wa Chama cha Tanzania Girl Guids (TGGA), Symphorosa Hangi katika hafla ya kuwaaga kwenda Uganda ambako watakutana na wenzao 31 kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati katika mafunzo ya uongozi na utamaduni katika nchi hizo. Hafla hiyo ilifanyika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam juzi. Kutoka kulia ni Farida Mjoge,Elizabeth Betha, Edna Chembele na Ummy Mwabondo.

MSIMU WA 15 WA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA MBIO ZA KILIMANJARO PREMIUM LAGER MARATHON 2017 WAZINDULIWA RASMI MKOANI KILIMANJARO.

Mkuu wa wilaya ya Moshi, Kippi Warioba akizungumza wakati wa uzinduzi wa msimu wa 15 wa mbio za kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2017 ,uzinduzi uliofanyika Kibo Palace Home mjini Moshi.

TANZANIA KUANZA KUTUMIA MFUMO WA DIRISHA MOJA LA HUDUMA (ELECTRONIC SINGLE WINDOW SYSTEM)

Kaimu Kamishna Mkuu TRA, Mary Maganga.
Katika kuhakikisha inaboresha huduma kwa wafanyabiashara ambao wanaingiza mizigo nchini kwa njia ya bandari, mipaka na viwanja vya ndege, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imeeleza mpango wa Serikali wa kuanza kutumia mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System) ambao kwa hakika utamaliza tatizo la mizigo kukaa muda mrefu kwa sababu ya kukosekana vibali.

KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA MAKAO MAKUU YA TTSA, TAWA NA TAFORI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizaya hiyo, Meja Generali Gaudence Milanzi (kushoto) wakiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii walipowasili katika ofisi za Wakala ya Miti za Mbegu Tanzania (TTSA) mjini Morogoro jana kwa ajili ya kuona kazi na miradi ya wakala huyo. Kushoto ni wajumbe wa kamati hiyo, Silafi Maufi ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa na Godwin Molel (wa pili kushoto), Mbunge wa jimbo la Siha.

PROF. MBARAWA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA POSTA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akiwasili Ofisi za Posta Kuu ya Shirika la Posta maeneo ya Posta Mpya wakati alipofanya ziara ya kushtukiza Dar es Salaam leo. Kulia ni Postamasta Mkuu, Fortunatus Kapinga. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)

ZINGATIA HAYA ILI KUREJESHA ARI YA KUFANYA KAZI BAADA YA LIKIZO


Na Jumia Travel Tanzania

IWAPO unazitambua vizuri barabara za jiji la Dar es Salaam, basi utagundua kwamba kuna tofauti kubwa kwenye msongamano wa magari ukilinganisha na kipindi cha sikukuu. Hali hiyo imetokana na idadi kubwa ya watu kurejea jijini kuendelea na shughuli za kazi, ambapo wengi walikuwa kwenye likizo na mapumziko ya mwisho wa mwaka.

WAZIRI MKUU AONGOZA KUZINDUA DUKA LA BOHARI YA DAWA (MSD), MPANDA, MKOANI KATAVI


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (katikati), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa  duka la Dawa la Bohari ya Dawa (MSD), Mpanda mkoani Katavi. Kutoka shoto mwenye shati la kijani ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa  Katavi, Peter Mselemu, Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Kanali mstaafu Raphael Muhuga. Wa tatu kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA KINGDOM LEADERSHIP NETWORKS


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Taasisi ya Kingdom Leadership Network Tanzania Ibrahimu Kaduma aliyemtembelea Makamu wa Rais na kumuelezea mikakati ya kuanzisha Chuo cha Joseph Business School.

TIGO YAZINDUA TWENDE APP KUSAIDIA HUDUMA YA USAFIRI WA TEKSI NCHINI TANZANIA

 Mkuu wa Zana za Kidijitali wa Kampuni ya Simu ya Tigo,  Tawonga Mpore (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu kampuni hiyo kuzindua Twende APP kwa ajili ya kusaidia huduma ya usafiri wa teksi nchini. Kulia ni Mkuu wa Utawala na Fedha wa DTBi ambao ni wawezeshaji wa mradi huo, Mramba Makange na Mkurugenzi wa Idara ya Ubunifu wa Costech,  Dk. Digushilu Mafunda.

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI ATEMBELEA MRADI WA UJENZI NYUMBA ZA ASKARI MAGEREZA, UKONGA JIJINI DAR

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto), akisalimiana na Mshauri wa Kitengo cha Utafiti wa Udongo kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (BICO,UDSM), Dk. Dalmas Nyaoro, baada ya kuwasili eneo la Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makazi ya Askari Magereza ambao unakadiriwa kuhifadhi watumishi zaidi ya 300 ukikamilika  katika eneo la Ukonga, jijini Dar es Salaam. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

RITA KABATI: WAPINZANI HAWATASHINDA UCHAGUZI MDOGO WA KATA YA IGOMBAVANU NA IKWEA

 

Mbunge wa viti maalumu mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati akimpigia kampeni mgombea udiwani wa kata ya Igombavanu na kuwataka wapinzani kusahua kama watashinda katika kampeni za kuwania kiti cha udiwani katika kata ya Igombavanu tarafa ya Sadani wilayani Mufindi mkoani iringa zinaendelea kupamba moto huku uchaguzi ukitarajiwa kufanyika siku ya tarehe 22 /01 /2017.

MASAUNI AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA MAHAKAMA YA UMOJA WA MATAIFA (UNMICT-TAWI LA ARUSHA), JIJINI DAR



Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akimkaribisha Mkuu wa Mahakama ya Umoja wa Mataifa (UNMICT), Ofisi ya Arusha, Samwel Akorimo wakati viongozi wa Mahakama hiyo walipomtembelea kiongozi huyo wa Wizara, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya UNMICT na Wizara hiyo. Katikati ni Msajili wa Mahakama hiyo, Dk. Elias Olufemi.  Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Monday 16 January 2017

VIDEO: BINTI ALIYE MDATISHA MWANAUME MTANDAONI KWA PICHA ZISIZO ZAKE AAIBISHWA

Ni jambo la kusisimua kutokana na huruka za vijana kwenye mitandao ya kijamii, hii ni mara baada ya kuona matumizi mabaya ya mitandao kama Facebook,Twitter, Instagram nk vikiongezeka. Vijana wengi  wanashindwa kutumia mitandao ya kijamii  kwa ajili ya masilahi yao badala yake wamekuwa wakitumia mitandao hiyo, kutafuta wapenzi,utapeli, umbeya, kuanika nyeti zao yaani kuweka picha chafu nk.

TAASISI ZA UMMA MARUFUKU KUJENGA VITUO BINAFSI VYA KUHIFADHI DATA

Afisa Mkuu wa Ufundi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw Senzige Kisenge (aliyenyoosha mkono), akitoa maelezo ya Utendaji wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe Prof Makame Mbarawa (Katikati) alipotembelea Makao Makuu ya TTCL leo jijini Dar es Salaam. Afisa Mkuu wa Ufundi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Bw Senzige Kisenge (aliyenyoosha mkono), akitoa maelezo ya Utendaji wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe Prof Makame Mbarawa (Katikati) alipotembelea Makao Makuu ya TTCL leo jijini Dar es Salaam.

WASTAAFU WANAOLIPWA NA HAZINA WAHAKIKIWA KIGOMA

Mkaguzi Mkuu wa Ndani Msaidizi Bw. Stanslaus Mpembe akimhudumia mstaafu wakati wa zoezi la uhakiki wa wastaafu wanaolipwa na Wizara ya Fedha na Mipango, linalofanyika katika Halmashauri ya Mji wa Kigoma, Mkoani Kigoma.