Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 16 January 2017

WENGI WAJITOKEZA KUMUAGA AMINA ATHUMAN DAR


 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari za Michezo wa Gazeti la Uhuru, Amina Athuman  walipokuwa wakioutoa nyumbani kwake Banana, Dar es Salaam leo, kuliingiza kwenye gari tayari kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Lushoto kwa mazishi. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

 Mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari za Michezo wa Gazeti la Uhuru, marehemu  Amina Athumani ukiombewa dua nyumbani kwake, Banana, Ukonga.
 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania, Juma Pinto (kushoto) akimzungumzia marehemu Amina kuhusu uchapakazi wake enzi za uhai wake
 Baadhi ya waombolezaji wakiwemo wanahabari wakiwa eneo la msiba nyumbani kwa marehemu Amina Athuman, Banana, Ukonga Dar es Salaam
 Mwili ukpelekwa kwenye gari

 Mhariri Msanifu Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, ambaye kabla ya kujiunga na gazeti hilo alikuwa Mhariri Mtendaji wa gazeti la Uhuru,Joseph Kulangwa (kushoto), na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania, Juma Pinto wakiwa na huzuni wakati jeneza lenye mwili wa Amina Athuma likitolewa ndani tayari kusafirishwa kwenda Lushoto.
 Mgane wa marehemu Amina, Towfiq Majaliwa
 Ndugu wa marehemu
 Kiongozi wa kundi la wasapu la Waandishi wa Habari za Michezo Innocent Okamwa (kulia) akimkabidhi Baba mkubwa wa marehemu Amina Athuman, Athuman Kazukamwe mchango wa rambirambi sh. 600,000 zilizochangwa na wanahabari wa kundi hilo.Katikati ni mwanachama wa kundi hilo, Somoye Ng'itu.
 Kazukamwe akitoa shukrani kwa mchango huo

 Sehemu ya waombolezaji
 Mgane wa marehemu Amina, Towfiq Majaliwa akifarijiwa na Naibu Mhariri Mtendaji wa gazeti la Uhuru
Wanahabari wakiwa na huzuni

No comments:

Post a Comment