Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 29 November 2015

MSD YAKARABATI JENGO LA DUKA LA DAWA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI KWA KASI KUBWA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS DK.MAGUFULI

Mafundi wakikarabati jengo ambalo Bohari ya Dawa (MSD), itafungua duka la dawa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MSD) Dar es Salaam jana kwa ajili ya kuhudumia wananchi kwa karibu zaidi vikiwemo vifaa tiba. Duka hilo linatarajiwa kufunguliwa kesho kutwa.

CHAMA CHA WASHIRIKA-WAUGUZI TANZANIA KUKUTANA DESEMBA 12, 2015 JIJINI DAR ES SALAAM KUJADILI MAENDELEO NA CHANGAMOTO ZAO

 Ofisa Ushirika wa Wilaya ya Kinondoni jijini  Dar es Salaam, Omary Mkamba (kulia), akimkabidhi cheti cha Usajili wa Chama cha Ushirika -Wauguzi Tanzania  (Tanna Saccos Ltd) , Mwenyekiti wa chama hicho, Kapteni Adam Leyna katika mkutano uliofanyika hivi karibuni. Mkamba ni mlezi wa chama hicho.

KAMANDA MPINGA AZINDUA OPERESHENI PAZA SAUTI JIJINI DAR

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani,DCP  Mohamed Mpinga, akisalimiana na Mabalozi wa Usalama Barabarani, muda mfupi kabla ya kuzindua Operesheni ijulikanayo kwa jina la “Paza Sauti” yenye lengo la kuwaelimisha abiria ili waweze kutoa taarifa mara wanapoona kuna viashiria vya uvunjifu wa sheria za barabarani. Operesheni hii ilizinduliwa jijini Dar es Salaam.

TAFRIJA YA MCHAPALO WA UZINDUZI WA INTERNET YA KASI ZAIDI YA TIGO YAFANA TANGA


Mkuu wa kitengo cha biashara (B2B) katika kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Rene Bascope, akihutubia hadhira iliyohudhuria uzinduzi wa mfumo wa intaneti wenye kasi zaidi (4G LTE) uliozinduliwa jana jijini Tanga.

KAMPENI YA ABIRIA PAZA SAUTI YAZINDULIWA RASMI JIJINI DAR

Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa Umma wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Abel Swai (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo, kuhusu kampeni ya Abiria Paza Sauti iliyozinduliwa Dar es Salaam leo asubuhi.

MWILI WA MAWAZO KUAGWA KITAIFA KATIKA UWANJA WA FURAHISHA JIJINI MWANZA.

Mkutano wa Naibu Katibu Mkuu Chadema Salum Mwalimu na Wanahabari Jijini Mwanza hii leo.
Na:Binagi Media Group
Mwili wa aliekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Geita Marehemu Alphonce Mawazo, kesho unatarajiwa kuagwa Jijini Mwanza kabla ya kusafirisha kwenda Mkoani humo kwa ajili ya Mazishi.

MAGUFULI TUNATAKA MAWAZIRI 15 TU!

Magufuli katika ziara wizara ya fedha

Na Daniel Mbega

WAKATI uchumi wa Tanzania ni mdogo, baraza la mawaziri limeonekana kuwa kubwa na mzigo kwa taifa, tofauti na mabaraza ya nchi ambazo uchumi wake ni mkubwa, kama Marekani, China, Uingereza na hata nchi jirani ya Kenya, Uwazi Mizengwe linaandika.

UFISADI WA WABUNGE BALAA



Na Daniel Mbega

YALE madai ya ufisadi wa wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameanza. Wamegomea mkopo wa Shilingi milini  90 kwa ajili ya kununulia magari ya kifahari aina ya Toyota Land Cruiser, ambayo ni vitendea kazi vyao.

BARUA KWA WATUMISHI WA UMMA

meiomosi-2013Nawasalimuni nyote katika jina la nchi yetu nzuri Tanzania, Jina ambalo huko nyuma sote tuliliimba “Tazama ramani utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka…nchi hiyo mashuhuri huitwa Tanzaniaaa!” 

CHAMPIONI YATUNUKU TUZO KWA WAANDISHI NA WAHARIRI WAKE

TUZO CHAMPIONI (20)Meneja wa Global Publishers, Abdallah Mrisho (kushoto) akikabidhi tuzo ya Mhariri Bora kwa John Joseph. 

KOMBE AMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KWA KUWAPATIA JAMBO LEO FAGIO ZA USAFI SIKUKUU YA UHURU


 Waandishi wa habari wa gazeti la Jambo Leo, wakifurahia kupata fagio walizokabidhiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Zahanati ya Mji Mwema Kigamboni, Dar es Salaam, Omary Kombe (kulia), katika hafla iliyofanyika katika chumba cha habari cha gazeti hilo, Dar es Salaam. Kombe ametoa msaada huo kuunga mkono maelekezo ya Rais Dk. John Magufuli ya kufuta sherehe za Sikukuu ya Uhuru ili wananchi washiriki siku hiyo kufanya usafi wa mazingira kwa lengo la kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu nchini. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)

CHANZO CHA MAJI CHA RUVU CHINI KUWATUA AKINA MAMA NDOO ZA MAJI

Meneja Mradi Ruvu chini Mhandisi Emmanuel Makasa akiwaonesha waandishi wa habari sehemu ya bomba la kusafirisha maji kutoka chanzo cha Ruvu chini kwenda jijini Dar es salaam.

HII NDIYO BOMOBOMOA SALASALA ILI KUPISHA UJENZI WA BOMBA LA MAJI RUVU CHINI

Katapila likiwa ndani ya gari tayari kwa kazi ya bomobomoa eneo la Salasala jijii Dar es salaam ili kupisha ujenzi wa bomba la maji kutoka Ruvu Chini hadi jijini Dar es salaam.

MO APATA TUZO NYINGINE, ADHIHIRISHA TAMAA YA KUWATUMIKIA WATANZANIA

IMG_3351
Mfanyabiashara maarufu ambaye pia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akitembea kwenye 'Red Carpet' mara baada ya kuwasili katika hotel ya Hilton Sandton jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwenye hafla ya utoaji tuzo iliyoandaliwa na jarida maarufu la Forbes na kutunukiwa tuzo ya "Forbes Africa Person Of the Year 2015".(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).

Friday 27 November 2015

TIGO YADHAMINI ONESHO LA MWANAMUZIKI MOUSSA DIALLO KUTOKA NCHINI MALI LITANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM KESHO

Meneja wa Mawasiliano wa Kampuni ya Simu ya Tigo, John Wanyanja (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu kampuni hiyo kudhamini onesho la mwanamuziki Mousa Diallo kutoka nchini Mali litakalofanyika kesho katika Mgahawa wa Chakula na Vinywaji wa Samaki Samaki, Masaki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Mkuu wa Masoko wa Mgahawa wa Samaki Samaki, Saum Wengert na katikati ni Mwanamuziki, Moussa Diallo.

WENGI WAJITOKEZA KATIKA UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE JIJINI DAR ES SALAAM

Maelfu wajitokeza katika maandamano ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, hapa wakiendelea na matembezi ya kupinga ukatili wa Kijinsia
  Maandamano yakipokelewa na Mkurugenzi wa shirika la misaada la Marekani USAID  Daniel Moore, Mwakilishi wa Balozi wa Ireland nchini Maire Matthews, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa Wanawake Lucy Melele, Mkurugenzi wa shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo barani Afrika - WiLDAF, Dr. Judith Odunga, pamoja na wawakilishi wa mashirika wahisani na viongozi mbalimbali.
 Dr. Judith Odunga kutoka WiLDAF akiwakaribisha wageni.
 Mwanaharakati mama Siwale, Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Anna Mghwira(wa kwanza kulia) ni miongoni mwa waliohudhuria maadhimisho hayo.
 Wageni mbalimbali
 Maigizo kuhusu uchapaji wa viboko kwa wanafunzi
 Mwakilishi wa Balozi wa Ireland Maire Matthews akizungumza
  Lucy Melele kutoka shirika la UN Women akizungumza
 Mwalimu akitoa ushuhuda
  Paulina Mkonongo(wa kwanza kulia), Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Akisikiliza jambo
 Mgeni rasmi Bi. Paulina Mkonongo Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi akitembelea sehemu za maonyesho kutoka kwa mashirika mbalimbali.
 Baadhi ya wadau wakitembelea mabanda
 Wadau mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake.

Maadhimisho ya Siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake leo yamefunguliwa rasmi kwa kuanza na maandamano ya amani yaliyoanzia uwanja wa Tipi Sinza darajani hadi ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl iliyopo jengo la Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.

Maandamano hayo yalihudhuriwa na maelfu ya watu yaliongozwa na bendi ya jeshi la polisi kupitia njia za Shekilango kisha barabara ya Morogoro hadi katika jengo la Ubungo Plaza ambapo yalipokelewa na Mkurugenzi wa shirika la misaada la Marekani USAID  Daniel Moore, Mwakilishi wa Balozi wa Ireland nchini Maire Matthews, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa Wanawake Lucy Melele, Mkurugenzi wa shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo barani Afrika - WiLDAF, Dr. Judith Odunga, pamoja na wawakilishi wa mashirika wahisani na viongozi mbalimbali.

Akitoa neno la ukaribisho, Dr. Judith Odunga alisema kampeni ya siku 16 kwa mwaka huu imelenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama mashuleni. Lengo kuu ikiwa kuhamasisha umma kuhusu ukubwa wa ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu mashuleni.

“Ni kutokana na unyeti wa tatizo la ukatili wa kijinsia mashuleni, WILDAF na wadau mbalimbali tumeona kuna umuhimu wa kushirikisha Wizara ya elimu na ufundi stadi ili kuzungumzia ukatili wa kijinsia mashuleni na kujenga mikakati ya kuzuia ukatili huo” Aliongezea.

Dr. Odunga aliitaja kauli mbiu ya mwaka huu kuwa ni FUNGUKA! CHUKUA HATUA, MLINDE MTOTO APATE ELIMU. “Kauli hii inalenga kumshawishi mtu binafsi, kuwashawishi walimu, wanafunzi, wazazi na jamii kwa ujumla, kuwalinda watoto dhidi ya ukatili wa kijinsia na kuhakikisha kwamba shule ni mahala salama. Ni vyema kutafakari kwa kina jinsi vitendo vya ukatili wa kijinsia mashuleni vinavyoathiri maendeleo ya watoto wetu kielimu.” Alisema Dr. Odunga.

Dr. Odunga alitumia nafasi hiyo kuiomba serikali kufanya yafuatayo:

1.      Kufutwa kabisa kwa adhabu ya viboko mashuleni na waalimu kufundishwa au kutafuta mbinu za kutoa adhabu mbadala.
2.      Kutengeneza mwongozo wa utekelezaji wa sera ya elimu ya mwaka 2014 utakaoelekeza upatikanaji wa elimu ya msingi iliyo bora na salama.
3.      Kuboresha miundombinu rafiki ya elimu ikiwa ni pamoja na kuwa na madarasa ya kutosha, madawati, vyoo na sehemu za kujisitiri watoto wa kike, mabweni, uzio pamoja na kuwa na usafiri wa uhakika kwa wanafunzi.
4.      Serikali kuweza kuunda na kusimamia mabaraza yatakayo kuwa yanasikiliza malalamiko ya wanafunzi mashuleni.
5.      Tunaomba Wizara ya elimu na ufundi stadi kushirikiana na wizara ya Katiba na Sheria na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kutunga Sheria ya Ukatili wa Majumbani sambamba na kubadilisha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inayoruhusu ndoa kwa mtoto chini ya miaka 18.


Akifungua rasmi kampeni hizi, mgeni rasmi Paulina Mkonongo ambaye ni Mkurugenzi wa Elimu ya sekondari kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi aliyemuwakilisha Katibu mkuu wa wizara hiyo alisema, “ukatili wa kijinsia huleta athari hasi katika utoaji na upatikana wa fursa mbalimbali za kijamii ikiwemo fursa ya elimu kwa watoto wetu, hivyo kuwa ni kikwazo katika kujenga usawa wa kijinsia nchini.

Aidha Mkonongo alisema serikali imefanya juhudi za makusudi kuzuia ukatili na kuleta usawa katika kupambana na ukatili wa kijinsia kwa kuweka sera na mipango inayozingatia usawa na kupinga ukatili kwa makundi mbalimbali, katika jamii ukiwemo ukatili wa kijinsia.

Mkonongo alitoa wito kwa wananchi wote kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili na kwamba kila mtoto ana haki ya kulindwa popote anapokuwepo iwe nyumbani, shuleni, kwenye vyombo vya usafiri, michezoni na njiani wanapokwenda na kurudi shuleni pia kuwapa mbinu za kujilinda wenyewe.

Naye mwakilishi wa Balozi wa Ireland nchini Bi. Maire Matthews alisema kuwa takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa wastani wa asilimia 45 ya wanawake Tanzania wenye umri kati ya miaka 15 – 49 waliripoti kuwahi kufanyiwa ukatili wa kimwili au kingono katika maisha yao. Alisema takwimu nyingine zinakadiria kiwango hicho kuwa kati ya 41 – 56%.

Kwa upande wake Lucy Melele kutoka shirika la UN Women aliyemwakilisha Mwakilishi wa shirika hilo hapa nchini Anna Collins alisema wanawake na wasichana ulimwenguni kote wanapitia aina mbalimbali za ukatili ambayo inawanyima haki zao za msingi, ni tishio la demokrasia na ni kizuizi cha amani ya kudumu. Hata hivyo alisema shirika la umoja wa mataifa litaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na wadau wa maendeleo, serikali, mashirika mbalimbali, na jamii katika kampeni ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia pia inafanyika kikanda katika kanda ya ziwa (Mwanza, Mara na Shinyanga, kanda ya Kaskazini (Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga), kanda ya kati (Dodoma, Morogoro na Singida), kanda ya Kusini (Mtwara, Songea, Mbeya, Iringa na Lindi, Kanda ya Pwani (Dar es salaam na Pwani) zikisimamiwa na wadau mbalimbali wakiwemo mashirika ya Kivulini, CWCA, NAFGEM, Morogoro Paralegal,  Mtwara paralegal, WiLDAF, TWCWC pamoja na jeshi la Polisi.




WAKAZI WA MIKOA YA MANYARA, ARUSHA NA KILIMANJARO WAJITOKEZA UZINDUZI WA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA.

Brass Band ya Chuo cha Polisi Moshi ikiongoza maandamano ya uzinduzi wa kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kanda ya kaskazini .

KAMPUNI YA MEGATRADE INVESTMENT LTD YAVIPIGA JEKI CHUKO KIKUU CHA USHIRIKA NA BIASHARA,MOSHI NA CHAMA CHA SOKA MKOA WA KILIMANJARO.

Meneja masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ya jijini Arusha,Edmund Rutaraka akimkabidhi hundi ya kiasi cha shilingi Milioni 1.5 ,katibu wa Chama cha soka mkoa wa Kilimanjaro ,KRFA,Mohamed Musa kwa ajili ya kusadia ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa iliyoanza hivi karibuni.

MUULIZE MO!: TUANDIKIE MASWALI YAKO KUMUULIZA MOHAMMED DEWJI (CEO WA METL GROUP) TUTAKUWA NA MAHOJIANO NAYE HIVI KARIBUNI

mo
Msomaji na mdau wa mtandao wako wa habari www.modewjiblog.com unakupa nafasi wewe kumuuliza maswali/swali lolote lile Afisa Mtendaji Mkuu wa MeTL Group, Mohammed Dewji. Maswali yote yatajibiwa na kutolewa ufafanuzi wa kina. Tutakuwa na mahojiano naye karibuni. Asanteni sana.
Utaratibu wa kumuuliza maswali ni kwa kukomenti kwenye post hii kisanduku cha maoni, Zingatia Kanuni na sheria ikiwemo kutotumia lugha zisizo rasmi.
Pia waweza kutoa maoni yako kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ukiwemo ukurasa wa Mohammed Dewji : https://www.facebook.com/mohammeddewjitz/
au Ukurasa wa Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL):https://www.facebook.com/MeTLGroup/photos

TAMASHA KUBWA LA BURUDANI LA INSTAGRAM PARTY KUFANYIKA JUMAMOSI VIWANJA VYA ESCAPE ONE MIKOCHENI JIJINI DAR ES SALAAM

  Mkurugenzi wa Freconic ideaz, Fred Ngimba.

MBUNGE WA CHUMBUNI ZANZIBAR AWASHUKURU WAPIGA KURA WAKE

Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza AMJAD akiwasalimia Wananchi wa Jimbo la Chumbuni wakati wa mkutano wake wa kutowa shukrani kwa Wapiga kura wake mkutano uliofganyika katika Afisi za Jimbo Tawi la CCM Muembemakumbi Zanzibar.

MBUNGE WA UBUNGO SAID KUBENEA AWATEMBELEA WANANCHI WAKE KUWASHUKURU KUMCHAGUA NA KUJUA CHANGAMOTO ZAO

 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Said Kubenea akiongea na wananchi Stendi ya Mabasi ya Ubungo Dar es Salaam leo, kuwashukuru kwa kumchagua na kujua changamoto zao mbalimbali. Mbunge huyo jana alitembelea Soko la Ndizi la Mabibo, Soko la Mabibo, Kituo cha Mabasi cha Mawasiliano  na kumpa pole ya sh. milioni 1.1 Diwani wa Kata ya Manzese, Ramadhani Kwangaya ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Mus'ab kilicho chomwa moto na kuunguza magodoro 30.

MAKUNDI YA JAMII ASILIA YA WAHADZABE, WABARABAIG, WAMASAI WAIOMBA SERIKALI YA TANZANIA KUWATAMBUA KAMA JAMII NYINGINE!

DSC_0928
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu, Mh. Idd Ramadhan Mapuri (katikati) akizindua taarifa ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu utafiti wa Hali ya Haki za watu wenye kuishi maisha asilia Tanzania. kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay na (kulia) ni mmoja wa wajumbe walioshiriki kuandaa ripoti hiyo, kutoka nchini Kenya katika taasisi ya ACHPR, Dk. Naomi Kipuri.(Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).

Thursday 19 November 2015

VIONGOZI WA KIMILA WAPITISHA AZIMIO LA KUMLINDA MTOTO WA KIKE

IMG_1623
Pichani juu na chini ni baadhi ya viongozi wa mila (Laigwanan na Laiboni) na akina mama mashuhuri (Ngaigwanan) wilayani Lolilondo wakisoma na kujadili azimio la pamoja la kumlinda mtoto wa kike kabla ya kulipitisha na kusaini wakati wa kongamano kubwa la siku mbili lililofanyika katika ofisi za halmashauri ya wilaya Ngorongoro, jijini Arusha.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

SERIKALI YAIPONGEZA JUHUDI ZINAZOFANYWA NA TAASISI YA DORIS MOLLEL FOUNDATION ZA KUSAIDIA WATOTO NJITI!

DSC_1839
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Saidi Meck Sadiki akizungumza mbele ya wanahabari, madaktari na baadhi ya akina mama waliokuwa na watoto waliozaliwa kabla ya wakati maarufu kama Njiti (Hawapo pichani). Kushoto ni DoriS Mollel ambaye ni Mwanzilishi na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation (DMF) na wengine ni maafisa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).

KLABU YA ROTARY YA DAR ES SALAAM OYSTERBAY WATOA MATIBABU YA BURE KWA WAKAZI WA KEREGE-BAGAMOYO

DSC_1602
Rais wa klabu ya Rotary Dar es Salaam Oyster Bay kwa mwaka huu wa 2015-2016, Mohamed Versi akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) katika mji wa Kerege jana Novemba 15. wakati wa zoezi hilo la kambi ya bure ya upimaji wa afya. (Picha zote na Andrew Chale ).

JIJI LA MBEYA HATARI KUKUMBWA NA UGONJWA WA KIPINDUPINDU


Wafanyabiashara ndogo ndogo katika eneo la Makunguru jijini Mbeya wakiendelea na shughuli zao kama kawaida .



Na Mwandishi wetu,Mbeya

Halmashauri ya jiji la Mbeya limewataka wafanyabiashara ndogondogo hususani wa chakula  kujijengea tabia ya kuchoma taka nyakati za jioni mara wamalizapo kuuza biashara zao na si kusubili gari ya taka kuja kuzoa.



Aidha imewataka  wakazi hao kuondokana na fikra duni  ya kuamini kuwa kazi ya uzoaji wa taka na kusafisha mazingira ni ya halmashauri ya Jiji na sio mali ya mtu.



Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Jiji la Mbeya, Dkt. Samweli Lazaro, amesema, wananchi wanatakiwa kujenga tabia ya usafi na sio kusubili kupigizana kelele na serikali kwa kuwahimiza kufanya usafi kwani adui mkubwa wa afya ni uchafu hivyo kila mmoja anapaswa kuwa mlinzi wa mwezake katika kutunza mazingira.



Hali hiyo imesababisha kuwepo kwa malimbikizo mengi ya taka  kwenye sehemu zisizorasmi  ndani ya JIji la Mbeya na kupelekea jiji hilo kuwa chafu hususani katika maeneo ya  sokoni.



Amesema, hivi sasa halmashauri ilianzisha mpango wa uzoaji wa taka barabarani ambapo mpango huo umeonekana  kupokelewa na wananchi kwa asilimia 100 changamoto inakuja kwa upande wa halmashauri kuonekana kuzidiwa kutokana na ukosefu wa vitendea kazi.



“Halmashauri ilianzisha zoezi la kupitia taka zinazozalishwa na wananchi ambazo huziweka barabarani na magari yanapitia lakini mapango huu umeonekana kuzaa matunda kwa jamii kuupokea lakini tatizo ni uhaba wa vitendea kazi,”alisema.



Alisema, ili zoezi hilo lifanikiwe halmashauri inahitaji zaidi ya gari saba za ubebaji taka na kontena 80 lakini mpaka sasa magari yaliyopo ni manne na kontena 30 .



Hata hivyo kutokana na changamoto hiyo, Lazaro anawasihi wananchi kujenga tabia ya kuweka mazingira safi hasa kipindi hiki cha mvua kwani ndipo magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu yanapoibuka na kusababisha vifo vya watu.





JAMIIMOJABLOG MBEYA