Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 31 August 2016

NMB YAWAKUMBUKA WATOTO WENYE USONJI, YAWAPA MSAADA WA VIFAA VYA MASOMO


Pamoja na kuwa bora utoaji wa huduma za kibenki lakini pia benki ya NMB imejipanga kuhakikisha inakuwa pia bora katika kusaidia jamii na katika kudhihilisha hilo imetoa msaada wa vifaa vya kutumia darasani na vya michezo kwa watoto walio na usonji (autism) ambao wanasoma katika shule ya msingi Mbuyuni, iliyopo Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU AHUDHURIA UFUNGUZI WA MKUTANO WA 36 WA SADC MJINI MBABANE SWAZILAND


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa kwenye mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofunguliwa leo kwenye ukumbi wa Mandvulo uliopo Lozitha, Swaziland.

Tuesday 30 August 2016

TTCL YAJITOSA MISS HIGHER LEARNING INSTITUTIONS 2016


Meneja Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Aron Msonga akizungumza na washiriki wa Shindano la TTCL Miss Higher Learning Institutions 2016 pamoja na wageni wengine walipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za TTCL jijini Dar es Salaam leo. Nyuma yake ni washiriki wa shindano la TTCL Miss Higher Learning Institutions 2016. Meneja Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Aron Msonga akizungumza na washiriki wa Shindano la TTCL Miss Higher Learning Institutions 2016 pamoja na wageni wengine walipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za TTCL jijini Dar es Salaam leo. Nyuma yake ni washiriki wa shindano la TTCL Miss Higher Learning Institutions 2016.

TANESCO KUBORESHA KITUO KIKUU CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME CHA ILALA, MAENEO KADHAA KUATHIRIKA NA UPATIKANAJI UMEME JIJINI DAR ES SALAAM



NA K-VIS MEDIA
SHIRIKA la Umeme Tanzania, (TANESCO), linapenda kuuarifu umma kuwa kutakuwepo na katizo la umeme KUANZIA Septemba 3, 2016 kwenye maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam kutokana na kazi kubwa ya kuboresha miundombinu ya umeme kwenye kituo kikubwa cha kupoza na kusambaza cha Msongo wa Kilovolti 132 cha Ubungo-Ilala.

SHUKRANI ZA FAMILIA YA MAREHEMU MOHAMED MTATURU MKONONGO

Marehemu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo enzi za uhai wake
 

Familia ya marehemu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo na mkewe Bi. Naiz Edriss Mavura pamoja na familia ya Mama Amina Mtaturu, Mheshimiwa DC Miraji Jumanne Mtaturu na Mzee Salum Chima; tunapenda kuwashukuru ndugu, jamaa na marafiki wote kwa upendo na faraja mliyowapatia na kwa kushiriki kwenu kikamilifu katika kufanikisha maziko ya mpendwa wetu, Ndugu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo (pichani), ambaye aliitwa na Mungu alhamisi, 21 Julai 2016 saa 1:40 asubuhi, kwa ajali ya gari.

TIGO YATOA MSAADA WA MADAWATI 235 KWA SHULE ZA MSINGI MKOANI KAGERA

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Deodatus Kinawiro akipokea msaada wa madawati 235 kwa mkoa wa Kagera toka kwa Meneja wa Tigo kanda ya ziwa , Edgar Mapande jana kwenye shule ya msingi Katoro wilayani Bukoba.

DC NDEJEMBI AJIONEA KITUO CHA AFYA KILICHOJENGWA CHINI YA KIWANGO


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Mhe Deogratius Ndejembi akisisitiza jambo wakati akizungumza na wananchi waliofika kupatiwa huduma ya afya.

RC SINGIDA AKABIDHI MADAWATI 630 KWA WAKURUGENZI WA WILAYA NA MANISPAA

Na Mathias Canal, Singida

Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri za Mkoa wa Singida wamekabidhiwa jumla ya madawati 90 kwa kila Halmashauri ili kuondoa adha waliyokuwa wanakumbana nayo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kampeni ya kuchangia madawati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipowaagiza wakuu wa mikoa yote nchini wakati akiwaapisha Ikulu, jijini Dar es Salaam Machi 15, 2016.



Wakurugenzi hao wametakiwa kuyachukua haraka madawati hayo na kuyapeleka Katika shule zenye kadhia hiyo ikiwa ni ishara ya kuamsha taswira ya elimu kwa wanafunzi mchini kuondokana na mateso ya kukaa chini wakiwa darasani.

 Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe wakati wa makabidhiano hayo katika Ukumbi wa Ofisi za Mkoa huo huku akisifu wadau na Taasisi mbalimbali kujitolea kuunga mkono uchangiaji wa madawati ambao awali ulianza kwa ngazi ya Halmashauri kabla ya kuhusisha taasisi mbalimba sambamba na wadau wa maendeleo Mkoani humo.
Mtigumwe amesema kuwa Hali ya Madawati katika Mkoa ilikuwa chini ya asilimia 40% lakini chini ya uongozi wake kwa kushirikiana na wadau 67 wa Maendeleo wameweza kuchangia jumla ya shilingi milioni 42,626,500 hivyo kufanikisha lengo la utengenezaji wa madawati kufikia asilimia 98% ambapo hata hivyo upungufu Mkubwa ulikuwa zaidi katika Halmashauri za Singida na Manyoni.

Monday 29 August 2016

WAZIRI WA FEDHA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA KIGOMA


Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (kushoto) akimsikiliza kwa makini Bi. Rehema Kabuye (katikati) aliyekua akilia kwa uchungu, akimsihi Waziri huyo wa Fedha na Mipango, amsaidie ili mume wake ambaye ni Nahodha wa meli ya MV Liemba pamoja na wafanyakazi wengine wa Mamlaka ya Huduma za meli mkoani Kigoma, walipwe mishahara yao ya miezi nane ili kuwaondolea adha ya maisha inayowakabili wao na familia zao.

RAIS MALINZI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUNISHI

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Kipa wa Young Africans na timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Deogratius Munishi kutokana na kifo cha Baba yake mzazi, Mzee Boniventur Munishi kilichotokea jana Agosti 28, 2016.

MCHEZO WA LIGI KUU YOUNG AFRICANS V JKT RUVU

Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imethibitisha kuwa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Young Africans ya Dar es Salaam na JKT Ruvu ya Pwani, ulipangwa kufanyika Jumatano Agosti 31, 2016 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam imeahirishwa mpaka itakapopangiwa tarehe nyingine.

KIPAO AMBADILI MUNISHI TAIFA STARS

Kocha Mkuu wa timu ya Mpira wa Miguu Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa, amefanya mabadiliko kwenye kikosi kinachotarajiwa kusafiri Jumatano Agosti 31, 2016 kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017) dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo, Super Eagles.

DALADALA LAGONGA MAGARI MATATU MAJI MATITU TEMEKE JIJINI DAR

 Wananchi wakiangalia ajali iliyosababishwa na daladala lenye namba za usajili T 397 BVB linalofanya safari zake kati ya Temeke na Gongo la Mboto kwa kuyagonga magari mengine matatu eneo la Maji Matitu Temeke Dar es Salaam leo asubuhi. Katika ajali hiyo dereva wa gari dogo namba T 628 DFE alijeruhiwa.
 Gari dogo namba T 628 DFE lililogongwa na daladala hilo likiwa limeharibika.
 Daladala hiloegonga gari namba T 458 CAN.
 Kuku waliokuwa kwenye moja ya gari lililogongwa wakiondolewa kuku kadhaa walipoteza maisha katika ajali hiyo.
 Askari wa Usalama barabarani akiangalia ajali hiyo.
Daladala uso kwa uso na gari dogo.

Na Dotto Mwaibale

MKAZI wa Chamazi ambaye ni mwanamke amejeruhiwa baada ya gari lake dogo alilokuwa akiendesha kugongwa na daladala lenye namba T 397 BVB linadodaiwa kuiba njia.

Ajali hiyo imetokea Maji Matitu Temeke jijini Dar es Salaam leo  asubuhi ambapo daladala hilo pia liliyagonga magari mengine matatu na kuzua kizaazaa katika barabara ya Charambe kwenda Chamazi.

Mkazi wa eneo hilo Hamisi Juma aliyeshuhudia ajali hiyo amesema ni mungu kasaidia kutokea kwa vifo kwani ajali hiyo ilikuwa ni mbaya sana.

" Saa 12 na dakika 55 nikiwa nasubiri gari kwenda kazini niliona daladala lililokuwa likitoka Charambe kwenda Chamazi lilikuwa likipita upande ambao si wake likiwa katika mwendo wa kasi na ghafla lililigonga gari dogo namba T 628 DFE ambalo ligeuka na kulala katika mtaro" alisema Juma.

Alisema baada ya kuligonga gari hilo liliyaparamia magari mengine madogo mawili likiwepo lililobeba kuku na kuyasukumia kwenye mtaro.

Aliongeza kuwa baada ya kutokea tukio hilo dereva wa daladala hilo alikimbia na kulitelekeza gari lake.

Magari yaliyohusika katika ajali hiyo ni T 628 DFE, T 397 BVB, T 451 CQB na T 458 CAN.

Jitihada za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke ili kuzungumzia suala hilo hazikuzaa matunda baada ya simu yake kuita bila kupokewa alipopigiwa simu mara kadhaa.

MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA JWTZ, JKT MGULANI YATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE SHIDA KURASINI JIJINI DAR ES SALAAM

 Meja Dora Kawawa wa Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa 831 KJ Mgulani (kushoto), akimkabidhi msaada wa vyakula, Ofisa Mfawidhi wa Makao ya Taifa ya Watoto wenye shida Kurasini, Beatrice Lawrance, Dar es Salaam leo jioni , ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), ambapo kilele chake kitakuwa Septemba Mosi mwaka huu.

MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AHUDHURIA KIKAO CHA SADC TROIKA MJINI MBABANE SWAZILAND


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akipata maelezo kutoka kwa  Mkurugenzi na Balozi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Innocent Shio (katikati) kulia ni Waziri Mambo ya Njena ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) muda mfupi kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Troika Summit) unaowahusisha Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika umefanyika mchana huu  katika ukumbi wa Grand- Lozitha mjini Mbababe Swaziland.

WAKAZI WA MULEBA WALIPOKEA KWA SHANGWE TAMASHA LA TIGO FIESTA USIKU WA JANA


Mkuu wa wilaya ya Muleba  Bw Richard Ruyango , akifungua rasmi tamasha la Tigo fiesta kwenye uwanja wa David Zihimbile wilayani humo usiku wa jana, Kulia ni Meneja wa Tigo kanda ya ziwa Edgar Mapande na kushoto mkurugenzi wa vipindi clouds Ruge Mutahaba na mwakilishi kutoka wilayani.

WATANZANIA WAASA KUHIFADHI LUGHA ZA ASILI ILI KUONGEZA MISAMIATI YA KISWAHILI.

Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Dar es Salaam
Serikali inathamini jitihada za wadau katika kuhifadhi, kutunza na kusambaza lugha za makabila mbalimbali nchini ambazo ndio msingi wa lugha aushi ya Kiswahili ambayo ni lugha ya taifa.

DC MTATURU AWATAKA WANANCHI WALIOVAMIA ENEO LA HIFADHI KUHAMA NDANI YA MWEZI MMOJA


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisikiliza Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kaugere Beatus Kapatya akitoa taarifa juu ya kusimama kwa ujenzi wa Zahanati hiyo.

KIFAHAMU KIPINDI KIPYA CHA 'CHUKUA HATUA' KINACHOHUSU VIJANA MKOANI DODOMA

 Watangazaji wa kipindi kipya cha CHUKUA HATUA Happy Balisidya na Mohammed Hammie, siku ya kwanza walipokutana wakati wa maandalizi ya kutengeneza kipindi hicho.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWASILI MJINI MBABANE SWAZILAND TAYARI KWA MKUTANO WA 36 WA SADC

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye ardhi ya mji wa Mbabane nchini Swaziland tayari kuhudhuria mkutano wa 36 wa SADC wa Wakuu wa nchi  na Serikali ambao utafanyika tarehe 29 Agosti mjini hapo.

NI HESHIMA UKICHINJIWA MBUZI WA SUPU MKOANI MARA.

Kuna Sherehe za aina mbalimbali mkoani Mara. Leo BMG inakujuza juu ya Shereze ya kuchinjiwa supu ya mbuzi. Hii hufanywa zaidi kwa wanajamii wa kabila la Wakurya mkoani humo.

KAMPUNI YA MABIBO YAWAANDALIA BONANZA WASHIRIKI MISS KINONDONI 2016 ILI KUWAWEKA FITI

 Wanyange wa Lete Raha Miss Kinondoni 2016 wakionesha moja ya shoo katika Bonanza walioandaliwa na Mdhamini wao Mkuu Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd lililofanyika ufukwe wa Jangwani Sea Breeze Mbezi jijini Dar es Salaam jana lenye lengo la kuwaweka fiti kabla ya shindano lao litakalofanyikaa Septemba mbili Hoteli ya Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.

Sunday 28 August 2016

ASASI YA FEDHA YAWAKUMBUSHA WANACHUO UMUHIMU WA KUWEKA AKIBA


Mkurungezi mtendaji wa Asasi ya Fedha Jafari Selemani akisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa warsha iliyofanyika katika Chuo cha Kilimanjaro Insitute college  na kuwakutanisha wanavyuo zaidi ya mia 2 hapa jijini Dar es salaam ambapo alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana kuwa na tabia ya kuweka akiba na kujiandaa na maisha ya uzee ambapo Moto wa asasi hiyo ni "UHURU WA KIFEDHA NI WAJIBU WAKO " kulia kwake ni mtaalamu wa biashara na mhamasishaji wa vijana Fasili  Boniface   mapema mwishoni wa wiki iliyopita.

RAIS DKT MAGUFULI AHUDHURIA MISA YA JUBILEI YA DHAHABU (MIAKA 50) YA NDOA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA NA ANNA MKAPA

 Rais Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe wakati akiwasili kuhudhuria  Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016.

KAMANDA SIRRO ATANGAZA KIAMA KWA WANANCHI WATAKAO ANDAMANA SEPTEMBA MOSI JIJINI DAR

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi (CP), Simon Sirro akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo, wakati akitangaza kiama kwa mwananchi yeyote atakayefanya maandamano Septemba Mosi ya kupinga udikiteta Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). 

EAGT LUMALA MPYA MWANZA KUFANYA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA JIPYA NA LA KISASA.


Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji kiongozi, Dkt.Daniel Moses Kulola, linapenda kuwakaribisha watu wote kwenye Harambee ya Ujenzi wa Kanisa jipya na la kisasa linalotarajiwa kujengwa katika viwanja vya kanisa hilo.

TIGO FIESTA YATIKISA MJI WA KAHAMA

Msanii wa Bongofleva Baraka Da Prince  akitumbuiza katika Tamasha la Tigo Fiesta 2016 lililofanyika katika uwanja wa Taifa usiku wa jana Mjini Kahama na kuwakutanisha wasaniii wengine nguli hapa nchini katika mziki wa kizazi kipya.

WAFANYAKAZI WA NMB TAWI LA NELSON MANDELA WASHIRIKI ZOEZI LA USAFI MJINI MOSHI LEO.

Wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi wakiwa wamebeba vifaa kwa ajili ya kufanya usafi katika eneo la njia mbili maarufu kama Double Road mjini Moshi leo.

Saturday 27 August 2016

WATANZANIA WALIOSOMA CHINA KUPATA UONGOZI MPYA

By LEAH MUSHI
Chama cha watanzania waliosoma China- China Allumni Association of Tanzania (CAAT) hii leo tarehe 27 August, 2016 kinatarajia kufanya uchaguzi mkuu kwa ajili ya kupata viongozi wake wapya.

Friday 26 August 2016

KAMPUNI YA UDALALI YA YONO YAINGIA MKATABA WA KIMATAIFA NA KAMPUNI YA BIDDERS CHOICE YA AFRIKA KUSINI

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yono Auction Mart & Co. Ltd, Scholastika Christian Kevela (kushoto), akiwaonesha waandishi wa habari Dar es Salaam leo (hawapo pichani), mkataba wa kimataifa walioingia na Kampuni ya Bidders Choice ya Afrika Kusini wa ushirikiano kwa ajili ya kufanya mnada wa mitambo ya kampuni ya uchimbaji ya Acacia inayomiliki mgodi wa dhahabu Bulynhulu uliopo mkoani Shinyanga. Kulia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Yono, Stanley Kevela.

KAMATI YA BUNGE YA TAMISEMI YATEMBELEA MRADI WA MABASI YAENDAYO HARAKA (DART) JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkurugenzi Mkuu wa Udart, David Mgwassa (katikati), akizungumza na wajumbe wa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) wakati wa ziara yao ya kutembelea mradi wa Udart Dar es Salaam leo.

Thursday 25 August 2016

KESHO NI KESHO TANZANIA V IVORY COAST

Mchezo wa kwanza wa mpira wa miguu wa ufukweni, kati ya Tanzania na Ivory Coast unatarajiwa kufanyika kesho kuanzia saa 10.00 jioni kwenye Uwanja uliotengenezwa maalumu kwa ajili ya mchezo huo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.

MIILI YA ASKARI WALIOUAWA NA MAJAMBAZI YAAGWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM



Waziri wa Wizara ya  Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa  kuaga miili ya askari waliouawa katika eneo la Mbande, Temeke baada ya kuvamiwa na majambazi .Ibada hiyo ya kuaga  ilifanyika katika Viwanja vya  Polisi  vilivyopo  barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

MKURUGENZI BUNDA AMSIMAMISHA KAZI MTHAMINI ARDHI KWA RUSHWA

Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara, Bibi. Janeth Mayanja akiwa ofisini kwake.


Na Immaculate Makilika- MAELEZO
Mkurugenzi Mtendaji  wa Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara, Bibi. Janeth Mayanja amemsimamisha kazi mtumishi wa Idara ya Ardhi na Mipango Miji kwa kosa la kujipatia fedha kinyume na taratibu za utumishi wa umma.

MFUKO WA PSPF WATOA ELIMU YA KUJIUNGA KATIKA MFUKO WA KUJICHANGIA KWA HIARI KWA WANANCHI WASIO KATIKA SEKTA RASMIN ZANZIBAR



Afisa wa Mfuko wa PSPF Tawi la Zanzibar Bi Fadhila akizungumza wakati wa Mkutano Taasisi zisizo rasmin za Wavuvi, Madereva wa gari za mchanga, Kifusi na Wakulima wa mbogamboga kujiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari ya Mfuko wa PSPF uliofanyika katika ukumbi wa Betilyamin Malindi Zanzibar.

TATIZO LA CHADEMA WANAPIMA HOMA KWA KIGANJA!


Na Daniel Mbega
NILIWAHI kuandika wakati fulani kwamba “UKWELI WA MWANASIASA NI JINA LAKE TU”  lakini wakatokea watu wengi kunikosoa, wakipinga uchambuzi wangu huo na wengine wakinitisha kwa maneno kwa sababu tu nilikuwa nimekisema kile ambacho wao ama wapendwa wao hawakupenda kisemwe hata kama kiko wazi.
Ilikuwa ni wakati wa kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu 2015 wakati nilipozichambua kauli za mawaziri wakuu wa zamani – Edward Lowassa na Frederick Sumaye – waliokwenda kutafuta hifadhi Chadema baada ya kuona ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hawana nafasi ya kwenda Ikulu tena kama wakuu wa nchi.
Nilisema kwamba wanasiasa hao wamefuzu katika sanaa. Bora Lowassa tunajua alisomea sanaa, lakini Sumaye alisomea kilimo!
SOMA ZAIDI HAPA

BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI LAKUTANA KUJADILI MAENDELEO YA MKAKATI WA KUPUNGUZA AJALI



Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, wakiongozwa na Mwenyekiti wa baraza ambae pia ni Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(katikati),  katika kikao cha kujadili maendeleo ya Mkakati wa Kudhibiti Ajali za Barabarani , ambao ulizinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi wa nane,ukiwa na lengo la kupunguza ajali kwa asilimia kumi  ifikapo mwezi Februari, mwakani.Wa kwanza mkono wa kulia kwa Naibu Waziri ni Katibu  Mtendaji  wa  baraza ambae pia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani ,  Mohamed Mpinga. Kikao  kilifanyika katika ukumbi wa wizara,jijini Dar es Salaam.

RC SIMIYU ATOA UFAFANUZI SAHIHI WA TAARIFA KUHUSU WALIMU WAKUU KUVULIWA MADARAKA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthon Mtaka akizungumza na Maafisa Elimu na Viongozi wa CWT wa Mkoa huo katika kikao maalum cha kutoa ufafanuzi wa agizo lililotolewwa na Serikali Mkoani humo la kufanya mabadiliko ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu kata, ambalo liliripotiwa tofauti katika vyombo ya habari na mitandao ya kijamii. kuwa Serikali imetangaza kuwavua madaraka.

Wednesday 24 August 2016

TAIFA STARS YA KUIVAA NIGERIA HII HAPA

Kocha Mkuu wa timu ya Mpira wa Miguu Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa, ametangaza wachezaji 20 watakaounda kikosi kitakachosafiri mwishoni mwa mwezi huu kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017) dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo, Super Eagles.

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA ANAYESHUGHULIKIA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Kanda ya Afrika Mashariki  Dkt. Nyamajeje Calleb Weggoro, Ikulu jijini Dar es salaam.