Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 18 August 2016

MALINZI AMPONGEZA RAIS BFA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za pongezi Rais mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Botswana Maclean Letshwiti aliyechaguliwa kushika wadhifa huo katika uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Maclean Letshwiti ambaye ni nguli katika masuala ya biashara, alimshinda Tebogo Sebego kwa kura 32 kwa 28.
Katika barua yake ya pongezi kwenda kwa Letshwiti, Rais Malinzi amemtakia kila la kheri Rais huyo mpya wa BFA aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Mochudi Centre Chiefs maarufu kwa jina la Magosi.
Katika barua hiyo, Malinzi amesema: “Nakuandikia barua hii kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya TFF na kwa niaba yangu mwenyewe, kukupongeza wewe baada ya kushinda nafasi ya urais katika uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Bostwana.”
“Mheshimiwa Rais, uchaguzi wenu ni ushahidi tosha wa kazi nzuri iliyowapa imani katika klabu uliyoiongoza na shirikisho la mpira wa miguu hapo Bostwana.,” amesema Malinzi katika taarifa yake na kuahidi ushirikiano wa kutosha kwa Rais Letshwiti.
Kadhalika, Rais Malinzi aliwapongeza Segolame Ramotlhwa na Marslow Motlogelwa waliochaguliwa kuwa Makamu Rais wa Kwanza na Makamu Rais wa Pili kwa kufuatana.

No comments:

Post a Comment