Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 30 June 2014

NIGERIA YANG'OLEWA, UFARANSA YAWASUBIRI UJERUMANI AU ALGERIA




France celebrate after beating Nigeria 2-0

Pogba opens door as France reach last eight

Published : 12:35 am  July 1, 2014 

(AFP) - A Paul Pogba header and a Joseph Yobo own goal saw France edge a hard-fought contest with Nigeria 2-0 in Brasilia on Monday to reach the World Cup quarter-finals.
Pogba broke the deadlock in the 79th minute, nodding into an empty net after Nigeria goalkeeper Vincent Enyeama, who plays for French club Lille, failed to collect a corner.
It was a cruel moment for Enyeama, but rewarded a barrage of French pressure sparked by the introduction of Antoine Griezmann, who forced Yobo to put through his own goal in injury time.
“I am very proud of what we have achieved,” said France coach Didier Deschamps.
“We were athletic, there were a lot of duels but we didn’t let up.” Pogba was ecstatic at being so pivotal to the result.
“To score a goal for your country in such an important game is one of the biggest moments of my life,” he said.
Deschamps’s France will now await the winners of Monday’s other last-16 tie between Germany and Algeria, who they will meet at the Maracana in Rio de Janeiro on July 4.
African champions Nigeria, meanwhile, must wait to sample the last eight at a World Cup, following defeat in their first knockout-phase match at the tournament since the 1998 competition in France.
Stephen Keshi’s side nonetheless departed to the sound of warm applause from the fans crammed into the cavernous Mane Garrincha National Stadium, who allied themselves with Nigeria’s cause from the off.
While France, who showed six changes, started purposefully, their final ball frequently let them down, which handed Nigeria opportunities to use their pace on the counter-attack.
Emmanuel Emenike thought he had put Nigeria ahead in the 19th minute when he deftly prodded in an in-swinging cross from Ahmed Musa, but the offside flag allowed French heart rates to return to normal.
France looked more threatening when they were able to bring the recalled Mathieu Valbuena into the game.
When the Marseille midfielder teed up Pogba for a vicious volley mid-way through the first half, it took a stunning reflex save from Enyeama to keep the game scoreless.
Another intelligent pass from Valbuena then gave Mathieu Debuchy a sight of goal, but the Newcastle United right-back drilled wide.
Late in the first half Emenike took aim from range, but Hugo Lloris was able to parry.
Nigeria suffered a blow early in the second period when Lazio midfielder Ogenyi Onazi had to be stretchered off after an ugly, ankle-high challenge by Blaise Matuidi, who escaped with only a caution.
Faced with growing Nigeria pressure, Deschamps introduced Griezmann in place of Olivier Giroud with half an hour to play and the move quickly paid immediate dividends.
After Lloris had saved from Peter Odemwingie, a one-two between Karim Benzema and Griezmann set the Real Madrid man clear, but although he squeezed the ball past Enyeama, Victor Moses was on hand to hook clear.
It was to prove a temporary reprieve.
Yohan Cabaye, back from suspension, saw a 20-yard half-volley crash back off the bar before Enyeama had to produce a finger-tip save to touch a Benzema header over the bar.
It was the second fine stop of the match from the 31-year-old, but seconds later his failure to claim Valbuena’s left-wing corner allowed Juventus midfielder Pogba to head in at the back post.
Enyeama then palmed a shot from Griezmann over the bar, but France made it 2-0 at the death when Yobo, under pressure from Griezmann, inadvertently steered Valbuena’s drilled cross into his own net.
http://sports.dailymirror.lk/2014/07/01/pogba-opens-door-as-france-reach-last-eight/

MUHIMU KABISA SOMA HAPA...ATHARI ZA KUTAZAMA TV


Watu wanaotazama runinga kwa saa tatu au zaidi kila siku wako katika hatari ya kuaga dunia mapema kuwaliko wale wanaotazama kwa muda mchache.
Hii ni kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa katika jarida la the American Heart Association nchini Marekani.
"Utazamaji sana wa wa runinga ni tabia ya watu wasio na kazi ya kufanyatu na kuna ongezeko la mienendo ya kila aina ya tabia za kukaa tu," mtafiti mkuu Miguel Martinez-Gonzalez, profesa wa chuo kikuu cha Navarra iliyoko Pamplona, nchini Uhispania, alisema katika taarifa ya shirika hilo.
"Matokeo ya utafiti wetu ni sambamba na utafiti tuliowahi kufanya, ambapo muda unaotumiwa kutazama runinga uliolinganishwa na idadi ya vifo vinavyotokea kwa sababu hiyo."
Watafiti hao waliwachunguz vijana wachanga 13,284 kutoka Uhispania wenye afya na waliohitimu chuo kikuu kuhusu aina tatu ya tabia za kukaa tu na hatari ya kuaga dunia kutokana na sababu zote:muda wa kutazama runinga, muda wa kutumia tarakilishi na muda wa kuendesha gari.
'Sababu nyinginezo'
Vijana hao walioshiriki, ambao walikuwa na umri wa wastani wa miaka 37 na ambao asilimia 67 walikuwa wanawake, walifuatiliwa kwa takriban miaka 8.2. mwishowe, vifo 97 viliripotiwa, vikiwemo vifo 19 vilivyotokana na mishipa na moyo, 46 kutokana na saratani na mengine 32 vilivyotokana na sababu nyinginezo.
Utafiti huo ulionyesha hatari kubwa ya kuaga dunia ilikuwa mara mbili zaidi kwa washiriki walioripoti kutazama runinga kwa saa tatu au zaidi kwa siku ikilinganishwa na wale waliotazama kwa saa moja au chini ya saa.
Watu 19 waliripotiwa kufariki kutokana na kutizama TV kwa muda mrefu
Hatari hii mara mbili zaidi ilidhihirishwa pia baada ya kutoa hesabu ya safu kubwa ya vigezo vingine vinavyohusiana na hatari kubwa ya kuaga dunia.
Watafiti hao hawakupata ushirikiano kati ya muda unaotumiwa na mtu anapotumia tarakilishi au kuendesha gari na hatari kubwa ya kuaga dunia mapema kutokana na sababu zote.
Pia waliongezea kuwa utafiti zaidi unapaswa kufanywa ili kudhibitisha ni athari zipi zilizopo kati ya kutumia tarakilishi na kuendesha gari katika viwango vya vifo, na pia kutathmini taratibu za kibayolojia zinazoweza kueleza uhusiano huo.
"Watu wanapoendelea kuzeeka, tabia za kukaa tu zitaenea zaidi, hasa kutazama runinga, na hili litasababisha mzigo mkubwa katika ongezeko la matatizo ya kiafya yanayoambatana na kuzeeka," Martinez-Gonzalez alisema.
"Matokeo ya utafiti wetu yanapendekeza watu wazima wajihusishe katika mazoezi ya viungo, waache kukaa tu kwa muda mrefu, na wapunguze kutazama televisheni kwa zaidi ya saa mbili kila siku."
BBC

NHIF YATETA NA WADAU WAKE WA MKOA WA DAR ES SALAAM

JAJI RUFAA YA PONDA AJITOA


Na Happiness Katabazi
JAJI Shabani Lila wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, Aliyekuwa amepangwa kusikiliza rufaa iliyokuwa imekatwa na Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu , Sheikh Ponda Issa Ponda, amejitoa kusikiliza rufaa hiyo  kwa maelezo Kuwa Dhamira yake inamfanya ajione hawezi kusikiliza rufaa hiyo.
Jaji Lila alitoa uamuzi huo mwishoni mwa wiki ambapo alisema Dhamira yake haimtumi kusikiliza rufaa hiyo namba 89/2013 iliyokatwa na Mwomba rufaa (Ponda) dhidi ya jamhuri inayo omba Mahakama Kuu itengue hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya Mei 9 Mwaka 2013, ambayo ilimtia hatiani kwa kosa Moja la kuingia kwa jinai Katika Kiwanja Cha Chang'ombe Markaz ambapo ilimfunga Kifungo Cha Mwaka mmoja nje na kumtaka  awe mtunza Amani na raia mwema lakini Agosti Mwaka na alikamatwa na kufunguliwa Kesi ya uchochezi kwa Madai ametenda makosa ya uchochezi wakati Akiwa ndani ya Maandalizi ya hukumu hiyo.
"Kwa Dhamira yangu hainitumi kusikiliza rufaa ya Ponda, nimerudisha jarada la rufaa hii  kwa Jaji Mfawidhi ili aweze kumpanga  jaji mwingine wa kusikiliza .....na pia nimelikataa ombi la Wakili wa Ponda, Juma Nassor lilokuwa Linaomba Mahakama hii impange Jaji mmoja atayesikiliza rufaa hiyo ya Ponda na ombi lilonalooamba Mahakama hiyo itoe amri ya Kuzuia Kesi ya uchochezi iliyofunguliwa na Jamhuri dhidi ya Ponda  Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro isimame hadi rufaa iliyokatwa na Ponda Katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, itakaposikilizwa kuamriwa.
Ponda aliwasilisha mahakamani hapo ombi la Kuomba Mahakama hiyo itoe amri ya Kuzuia Kesi ya uchochezi inayomkabili Morogoro ,isiendelee kusikilizwa hadi pale rufaa yake aliyoikata mapema Mwaka Jana ya Kapinga hukumu iliyotolewa Na Mahakama ya Kisutu Mei 9 Mwaka Jana, ambayo ilimtia hatiani Kwa kosa la kuingia Kwa jinai Katika Kiwanja Cha Markas Chang' ombe, ambapo Mahakama hiyo ilimfunga Kifungo Cha nje Cha Mwaka mmoja, lakini Agosti Mwaka Jana, alifikishwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro akikabiliwa na Kesi mpya ya uchochezi na kutenda kosa wakati yupo chini ya uangalizi wa Kifungo Cha Mwaka mmoja nje.
Hata hivyo Wakili wa Ponda ,Nassor alimwambia waandishi wa Habari Kuwa licha Jaji Lilla alikataa ombi lake la kuomba Maombi mawili ya mteja wake yapangwe wa jaji mmoja lakini Jaji Mfawidhi ameyapanga Maombi hayo mawili ya Ponda yaani rufaa iliyokatwa na Ponda na ombi la kuomba Kesi ya Uchochezi inayomkabili mTeja wake mkoani Morogoro, yamepangwa kusikilizwa kwa jaji Mmoja aitwaye Lawrnce  Kaduri ombi la kuomba Kesi ya uchochezi iliyofunguliwa Morogoro dhidi ya Ponda itaanza kusikilizwa Agosti 4 mwaka huu na rufaa yake Ponda itakuja kutajwa tarehe hiyo hiyo.
Mapema Juni Mwaka huu, Wakili Mwandamizi wa serikali Bernad Kongora aliwasilisha pingamizi la awali mahakamani Linaomba Mahakama hiyo itupilie Mbali maombi  hayo ya Ponda yanayo omba Mahakama itoe amri ya usikilizwaji wa Kesi ya uchochezi iliyofunguliwa Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro ya simama hadi rufaa yake itakapoamriwa kwasababu ombi Hilo linalengo ya kuaribu muda wa Mahakama na halina Msingi.


Chanzo: Gazeti La Tanzania Daima la Jumatatu, Juni 30 Mwaka 2014.

DK SALIM AFICHUA SIRI YA JK NA TUME YA WARIOBA



Dk. Salim Ahmed Salim

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim amesema hakutarajia kusikia kauli za Rais Jakaya Kikwete alizozitoa bungeni kukosoa Rasimu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa sababu walikuwa wanampa taarifa kwa kila hatua waliyokuwa wanafikia kabla ya kutoa rasimu hiyo.
Dk Salim alitoa kauli hiyo katika mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake Masaki, Dar es Salaam wiki iliyopita.
“Hatukutarajia kama hali ingefikia hatua iliyofikia,” alisema Dk Salim na kuongeza: “Lakini Rais ana uamuzi wake na anazingatia mambo mengine mengi.”
Akilihutubia Bunge maalumu la Katiba Machi 21, mwaka huu Rais Kikwete aligusia mambo saba ya msingi yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na kutaka yatazamwe kwa kina, huku akibainisha kuwa mengine hayawezekani kutekelezeka. Miongoni mwa mambo hayo ni muundo wa Serikali. Alipinga waziwazi pendekezo la serikali tatu lililopendekezwa na Tume na kuegemea katika muundo wa serikali mbili na idadi ya watu walioupendekeza akionyesha kuwa ilikuwa ni ndogo.
Pia alisema ni vigumu kutenganisha uwaziri na ubunge kama ilivyokuwa imependekezwa na Tume kwa maelezo kuwa mawaziri wanatakiwa kuwepo bungeni ili kujibu hoja za Serikali.
Jambo lingine alilokosoa katika Rasimu ni pendekezo la mtu kupoteza ubunge kwa sababu ya kuugua kwa miezi sita mfululizo huku akisema baadhi ya vifungu vya Katiba vinayopendekezwa vimekuwa na mambo mengi ambayo hayapaswi kuwamo katika Katiba, bali katika sheria zinazotafsiri utekelezaji wa Katiba yenyewe.
Katika mahojiano hayo maalumu, Dk Salim alisema baada ya kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Tume aliacha kuhudhuria vikao vya chama chake ili aweze kufanya kazi hiyo kwa usahihi na alimtaarifu Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais na katibu mkuu wake na walimwelewa.
Alipoulizwa anaitazama vipi Tanzania iwapo Katiba Mpya haitapatikana, Dk Salim alisema ana wasiwasi kwa kuwa suala hilo limeingizwa siasa na Bunge Maalumu limegeuka la kisiasa hivyo linaweza kuleta matatizo.
“Tuko katika hali ambayo si nzuri inayohitaji uongozi thabiti, viongozi wote watambue umuhimu wa zoezi hili kwa lengo la kulinda amani na utulivu wa nchi yetu,” alisema.
Alisema kunahitajika ufumbuzi wa kudumu na hicho ndicho kipimo cha uongozi kwa CCM, Chadema na wengine kwa kutafakari masilahi ya Watanzania wa leo, kesho na keshokutwa.

Nini kifanyike?

Dk Salim alisema jambo muhimu sasa ni pande mbili zinazoshindana kuhusu idadi ya Serikali kutumia mwezi ujao wa Julai kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao ili Bunge la Katiba liendelee bila misuguano.
“Mwezi huu wa Julai ni muhimu sana, ni mwezi pekee uliobaki wa kuwaweka pamoja wanaotofautiana. Kila jitihada zinatakiwa kufanyika ili kuhakikisha Bunge Maalumu linakutana tena Agosti na wapinzani waliosusa wanarejea ili kumaliza kazi hiyo kabla ya kutoa rasimu ya tatu kwa ajili ya kura za maoni,” alisema na kuonya kuwa kuendelea na katiba ya sasa kunaweza kuleta matatizo.
Neno ‘wasaliti wa Mwalimu Nyerere’ lamchefua
Aidha, Dk Salim ameeleza kusikitishwa na kukatishwa tamaa na kauli za baadhi ya wanasiasa dhidi yake na wajumbe wenzake wa Tume kwa kuwaita wasaliti na hasa kitendo cha kutilia shaka uzalendo wao.
“Inakatisha tamaa sana. Mimi nina umri wa miaka 72, kati yake zaidi ya miaka 30 nimeitumikia nchi yangu, haiingii akilini katika umri huu wa mwisho nianze kuisaliti nchi yangu, inasikitisha sana kusikia eti hawa wasaliti wa Mwalimu Nyerere,” alisema.
Dk Salim ambaye ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF), alisisitiza kuwa wajumbe hao wamekuwa wakishutumiwa na watu wenye malengo yao, akitolea mfano kuwa hata Dk Mwesiga Baregu aliwahi kushutumiwa na chama chake na kutakiwa ajitoe kwenye tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.
Itakumbukwa kwamba Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekuwa ikishutumiwa na wanasiasa hasa kutoka CCM kutokana na mapendekezo yake ya mfumo wa Muungano wa serikali tatu badala ya mbili zinazoungwa mkono na chama hicho.
Kutokana na tofauti hiyo, wajumbe walio wengi wa Bunge Maalumu la Katiba kutoka CCM waliamua kubadili baadhi ya vifungu vya rasimu.
“Ni bahati mbaya sana binadamu unapotukanwa, unatupiwa madongo, tunaonekana wapuuzi kwa kazi ya kukusanya maoni ya wananchi, inaumiza sana,” alisema.
Kama ambavyo Jaji Warioba amesema mara nyingi, Dk Salim aliitetea Rasimu ya Katiba, akisema kilichopendekezwa ndiyo picha halisi ya maoni ya Watanzania.
Alisema Tume hiyo ilikusanya maoni ya wananchi yenye hoja nzito yakieleza hasa matatizo yao katika nyanja mbalimbali kama afya, elimu, ardhi na mengine, ingawa hoja kuhusu muundo wa Serikali ndizo zinaonekana kushikiwa bango na wanasiasa.
Alisema ushahidi wa watu waliohojiwa upo katika maandishi, sauti na picha za video na idadi yao inatosha kuwakilisha Watanzania wote.

“Wanasema hatukuhoji watu wengi, waliohojiwa ni representative sample (sampuli), huwezi kuhoji Watanzania wote milioni 45,” alisema Dk Salim.
Alisema ni jambo la kushangaza kuwa mchakato umetekwa nyara na wanasiasa lakini Katiba inastahili kuwa ya kitaifa ya Watanzania wote, wenye vyama na wasio na vyama vya siasa.

Alisema hata kwenye tume, walikuwapo wajumbe zaidi ya 12 ambao hawatokani na CCM, wakitoka vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi na wote walikuwa na mawazo tofauti lakini waliamua kuyaweka kando na kutoa rasimu inayotoa taswira ya mawazo na masilahi ya wananchi.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Dk-Salim-afichua-siri-ya-JK-na-Tume-ya-Warioba-/-/1597296/2366416/-/qlooj5/-/index.html

MUHIMU SOMA HAPA...WASIOREJESHA MIKOPO VYUO VIKUU MARUFUKU KWENDA NG'AMBO

Tanzanian graduates with unpaid HESLB loans to be denied 'visas'


Graduates from higher learning education institutions who have not repaid their higher education loans will no longer get permits to travel outside Tanzania until they clear their debts.
The plan is to implement in joint efforts between the Ministry of Education and Vocational Training and the Immigration Department. 
Deputy Minister for Education and Vocational Training, Jenister Mhagama, told the House:
“We will not issue visas to graduates who have acquired loans from the Higher Education Students Loans Board (HESLB) and not settled the debts.
“We are ready to bring to parliament a list of our plans to recover the loans…and we are determined to get the money back so that it may be used to educate other students.”
She also said that ongoing issuance of national IDs will help HESLB track the
defaulters. 
She said the government is considering re-introduction the bond program that was in use in the early 1970s when the government used to sign special bonds with students to ensure that they work in the country for a specific period of time as repayment of their loans before they would be allowed to travel abroad for work.
The Deputy Minister was responding to a question by Namelock Sokoine (CCM-Special Seats) which was asked on her behalf by Betty Machangu (also CCM- Special Seats). 
In her main question, Sokoine wanted to know whether the government had any plans to ensure that graduate teachers who have benefited from education loans do not leave the country without paying them back.
In a supplementary question, Machangu expressed concerns over HESLB’s failure to recover loans from graduates and inquired as to what plans the board has to do so efficiently.
In a related development, Mhagama said a total of 89,500 secondary school teachers are required in the country, but there are only 74,250 of them and to bridge this gap, the government is prioritizing loans to students seeking to become teachers.
SOURCE: THE GUARDIAN

HII NDIYO SAFU MPYA YA KAMATI YA UTENDAJI YA TAIFA (SEKRETARIETI) YA CUF


1. Naibu Katibu Mkuu (Bara), Mhe. Magdalena Sakaya.
2. Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Mhe. Nassor Ahmed Mazrui.
3. Mkurugenzi wa Mipango na Chaguzi, Mhe. Omar Ali Shehe.
4. Naibu Mkurugenzi wa Mipango na Chaguzi, Mhe. Shaweji Mketo.
5. Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano na Umma, Mhe. Salim Bimani.
6. Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano na Umma, Mhe. Abdul Kambaya.
7. Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria, Mhe. Kulthum Mchuchuli.
8. Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria, Mhe. Pavu Abdallah Juma.
9. Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha, Mhe. Joran Bashange.
10. Naibu Mkurugenzi wa Uchumi nau Fedha, Mhe. Abdallah Bakari Hassan.
11. Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama (hajateuliwa).
12. Naibu Mkurugenzi wa Uinzi na Usalama, Mhe. Yussuf Salim Hussein.
13. Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Mhe. Ismail Jussa.
14. Naibu Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Mhe. Abdallah Mtolea.

GIGGS: SIKUWA TAYARI KUWA KOCHA WA MANCHESTER UNITED


Sikuwa tayari kuwa mkufunzi
Aliyekuwa kaimu kocha na mchezaji wa Manchester United Ryan Giggs amekiri kuwa hakuwa tayari kwa majukumu ya kazi kama kocha wa klabu hiyo ya Uingereza.
Giggs anasema kuwa uteuzi huo ulikuwa mapema kuliko alivyotarajia.
Giggs alichukua hatamu kama kaimu kocha mwisho wa msimu uliopita baada ya kocha David moyes Kutemwa kufuatia msururu wa matokeo duni tangu achukue hatamu Old Trafford.
Giggs aliyekuwa kocha katika mechi nne za mwisho alitwaa ushindi katika mechi 1 akashindwa moja na kisha akatoka sare katika mechi ya mwisho Manchester united ilipomaliza msimu katika nafasi ya 7 .

Giggs aliyasema hayo alipokuwa akikamilisha kozi ya ukufunzi akijitayarisha kusaidiana na Louis van Gaal Old Trafford .

Giggs alistaafu kama mchezaji msimu uliopita baada ya kuiwakilisha Man united katika mechi 963 na kufunga mabao 168 .
BBC

PISTORIOUS MWANARIADHA WA AFRIKA KUSINI ALIYEUA MPENZI WAKE HANA MATATIZO YA AKILI

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius hakuwa na tatizo lolote la kiakili wakati alipomuua mpenzi wake mwaka jana.
Haya ni matokeo ya uchunguzi wa kiakili aliofanyiwa Oscar Pistorius huku kesi yae ikianza kusikilizwa tena nchini Afrika Kusini.
Mawakili wake walikuwa wamedai kuwa Pistorius aliukuwa anakumbwa na hali ya wasiwasi na kuzongwa na mawazo wakati wa mauaji ya Reeva Steenkamp.Ripoti hiyo iliwasilishwa baada ya uchunguzi kufanywa kuhusu hali yake ya kiakili wakati alipofanya mauaji hayo mwaka jana.
Mwanariadha huyo amekana kumuua kwa maksudi mpenzi wake Reeva Steenkamp akisema kuwa alimpiga risasi kwa bahati mbaya baada ya kupatwa na wasiwasi akidhani jambazi alikuwa amevamia nyumba yake.
Upande wa mashitaka pamoja na utetezi wamekubali matokeo ya uchunguzi huo.
Upande wa utetezi sasa unasikia ushahidi wake daktari aliyemkata miguu Pistorius, Gerry Versfeld, anayetoa ushahidi kuhusu athari za Pistorius kukatwa miguu.
Upande wa utetezi nao unatarajiwa kumaliza ushahidi wake katika siku chache zijazo.
Bi Steenkamp, alikuwa na umri wa miaka 29, wakati wa mauaji yake Februari mwaka jana.
BBC

RIWAYA TAMU: JUDITH…JUDITH…! - 17



INNOCENT A. NDAYANSE (ZAGALLO)


0755 040 520 / 0653 593 546 

UTANGILIZI
Judith ameingia ndani ya Jiji la Dar es Salaam na Baraki anampangishia chumba cha gesti Magomeni. Kunapokucha anamuaga kwamba anakwenda kazini lakini anamwambia wazi kuwa ameoa ingawa anamtoa hofu asiwe na wasiwasi. Lakini baadaya Baraki kuondoka Judith anagundua kwamba hana nguo, hivyo anatoka nje mapokezi kuomba msaada. Je, nini kitaendelea? Ungana na msimulizi wako …

 Judith hakutaka Swaumu awe rafiki wa karibu. Ni ugeni wake tu uliomfanya aambatane naye. Kwa mtazamo wa haraka haraka alimwona Swaumu kuwa ni mwanamke ambaye hajatulia. Yuko macho juu-juu. Maswali mengi, udadisi usiokoma. Kichwani mwake hakumwona kuwa ni mtu anayefaa kwa ushirikiano wowote baina yao. Akaamua kujihadhari naye, lakini kwa namna ambayo Swaumu mwenyewe hatamshtukia.
Jioni ilifika, usiku ukaingia. Baraki hakuonekana. Lakini ilipotimu saa 4 usiku Judith akamwona Yohana, mhudumu wa gesti akimjia na simu mkononi. “Simu yako,” alimwambia huku akimpatia simu hiyo.
Alikuwa ni Baraki aliyepiga. Judith alipoipokea na kusikiliza, akapokea taarifa kutoka kwa Baraki kuwa kwa siku hiyo hatafika kwa kuwa amekuta matatizo katika familia yake.
“Kesho mchana tutawasiliana, sawa?” Baraki alimalizia.
“Sawa,” Judith alijibu kwa unyonge.
Usiku huo Judith akaamua kupiga pasi nguo zile alizonunua mchana kisha akaziweka juu ya kiti kilichokuwa chumbani humo. Angeziweka wapi wakati hakuwa hata na kijibegi kidogo? Baada ya hapo akalala. Usingizi haukumjia mapema. Alikuwa akiwaza jinsi atakavyomudu kuishi katika nchi hiyo ngeni ilhali hana hata ndugu huku pia ubalozi wa Rwanda ukiwa hauna taarifa yake. Akaendelea kuwaza na kuwazua, jibu asilipate. Hatimaye akaamua kufumba macho na kuulazimisha usingizi.
Dakika kumi baadaye alipitiwa na usingizi bila ya kujitambua, akazinduka asubuhi. Sasa akapiga moyo konde na kuamua kutoka, aukague mji huo mkubwa wa Dar es Salaam, labda huenda akapiga hatua moja nzuri katika kuhangaika huko.   
Na sasa hakutaka kumshirikisha mtu yeyote hususan yule Swaumu ambaye jana walikubaliana kuwa leo watakwenda wote kwenye maduka ya kubadilisha pesa. Hata huyu mhudumu wa mapokezi naye hakupaswa kujua ni kipi kinachoendelea.
Hivyo, mara tu baada ya kuoga, alivaa nguo nyingine kisha akaondoka kimya-kimya, machoni mwa wapita njia wenzake akionekana kuwa ni mwanamke wa kuvutia. Ndani ya pochi ambayo nayo aliinunua jana kule sokoni, kulikuwa na pesa kidogo za Tanzania, shilingi 9,000 zikiwa ni masalia ya zile 30,000/- alizoachiwa jana na Baraki.
Alitembea huku akiwafuata watu wengine walioonekana kuwa na haraka, wengi wao wakiwa wamevalia kinadhifu, hali iliyompa hisia kuwa huenda walikuwa wakielekea kule ambako watu hupaita ‘mjini.’ Na wengi kati ya watu hao walikuwa ni wanawake. Akaendelea kuwafuata.
Alikumbuka kuwa jana, wakati akiwa na Swaumu wakienda sokoni, aliyaona mabasi madogo ya abiria yenye maandishi ubavuni: CITY BUS. Alitaka ayatumie magari hayo kumfikisha huko panapoitwa ‘mjini.’ Akaendelea kuwafuata hao watu wengi ambao baadhi yao walikuwa na mabegi madogo mikononi.  
Robo saa baada ya kuianza safari hiyo, akajikuta akitokea Barabara ya Rashid Kawawa. Akaivuka na kushika Barabara ya Chemchemi. Hatimaye alijikuta akiibukia katika kituo cha daladala cha Magomeni Mapipa ambako alikuta idadi kubwa ya watu wanaosubiri usafiri.
Daladala zilikuja, daladala zikaondoka. Yeye hakukurupuka kupanda. Hakujua ni wapi alikopaswa kwenda na pia hakuwa na haraka. Akaendelea kuwatazama abiria wakikimbilia kila daladala iliyoingia. Kuna zilizokwenda Posta, nyingine Kariakoo, Muhimbili na hata Kivukoni.
Hatimaye aliamua kupanda daladala lililokwenda Posta, bila ya kupajua huko Posta na kama atafanikiwa kutimiza malengo yake.
Aliteremkia Posta Mpya. Akavuka barabara bila ya kumuuliza mtu yeyote, jambo lolote. Moyoni mwake alipanga kutafuta duka la kubadilisha pesa, lakini aliamua kuwa makini kwa kuwa alijua fika kuwa thamani ya pesa alizonazo ni kubwa hivyo kama watu wengine wangefahamu huenda ingekuwa hatari kwa upande wake. Kuna vibaka, matapeli na majambazi. Yeyote kati ya hao anaweza kumfanyia unyama kwa kujitwalia pesa hizo kwa njia moja au nyingine.
Akaifuata Barabara ya Jamhuri, akitembea kwa kujiamini kama vile ni mwenyeji wa eneo hilo . Huko mbele akajikuta akikumbana na Mtaa wa Zanaki. Hapo akasita. Sasa akajiwa na wazo la kuachana na Mtaa wa Jamhuri.
Akapinda kushoto na kufuata Mtaa wa Zanaki. Hakufika mbali, mara akaliona duka lenye bango kubwa ukutani: SAKA BUREAU DE CHANGE. Akasimama na kulitazama kwa sekunde chache kisha akalifuata. Dakika ishirini baadaye alikuwa akitoka ndani ya duka hilo huku akiwa na pesa za Tanzania, shilingi 2,000,000 na ushei. Akasimama kando ya barabara akiwa hajui ni wapi alikopaswa kwenda na kipi alichopaswa kufanya.
Akatulia kando ya barabara hiyo, nje ya duka hilo huku akiwa ameduwaa. Dakika mbili baadaye akapata uamuzi wa kukodi teksi. Japo alikuwa mgeni, lakini hakuwa mtu wa kushindwa kuzitambua teksi za jijini Dar, ambazo zilikuwa na utambulisho rasmi. Akaipungia mkono teksi  ambayo ilimtii.
“Magomeni,” alimwambia dereva teksi akiwa ameshaingia garini.
“Magomeni ipi?”
Lilikuwa ni swali ambalo Judith hakulitarajia. Hakuijua vizuri Magomeni na vitongoji vyake. Amwambie ni Magomeni ipi? Hata hivyo hakutaka kuudhihirisha ugeni wake kwa huyu dereva. Akamjibu, “Nitakuelekeza mbele ya safari.”
Walipofika jirani na Bondeni Hotel, Judith akakikumbuka kile kituo cha daladala alichopandia wakati anakuja Posta. Akamwambia dereva akate kulia. Dereva akatii. Walipofika jirani na kituo hicho, akamwamuru asimame.
“Ni kiasi gani?”
“Elfu saba.”


Itaendelea kesho…

BRAZIL YATWAA KOMBE LA DUNIA KWA KUICHAPA UJERUMANI 2-0 JAPAN 2002

File:NISSANSTADIUM20080608.JPG
Uwanja wa International jijini Yokohama, Japan ulikofanyikia mchezo wa fainali mwaka 2002

Na Daniel Mbega

Tunaendelea kujikumbusha mambo mbalimbali ya fainali za Kombe la Dunia ambapo leo ni miaka 12 tangu Brazil ilipoichapa Ujerumani katika mchezo wa fainali na kutwaa Kombe la Dunia kwa mara ya tano.
Mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa International, Yokohama nchini Japan mwaka 2002 ulihudhuriwa na watazamaji 69,029 na ulichezeshwa na 'Kipara' Pierluigi Collina wa Italia aliyesaidiwa na Leif Lundberg (Sweden) na Philip Sharp (England), wakati mwamuzi wa akiba alikuwa Hugh Dallas (Scotland).
Huu ndio ulikuwa mchezo wa kwanza na pekee mpaka sasa baina ya nchi hizo mbili katika historia ya Kombe la Dunia. 
Brazil ilishinda mchezo huo kwa mabao 2–0, huku mshambuliaji wake nyota Ronaldo (ambaye hakufanya vizuri katika fainali za mwaka 1998 kule Ufaransa), aliyeweka rekodi ya ufungaji mabao kwenye Kombe la Dunia mwaka 2006, alifunga mabao mawili kati ya mabao yake 15 ya Kombe la Dunia kwenye kipindi cha pili cha mchezo huo, akaiongoza Brazil kutwaa ubingwa na yeye akatwaa Kiatu cha Dhahabu. 
Pia mechi hiyo ilimfanya nahodha wa Brazil Cafu kucheza mchezo wa fainali wa tatu mfululizo, rekodi ambayo bado haijafikiwa na mchezaji mwingine yeyote katika historia ya mashindano.
Timu zote zilikuwa zimeongoza katika makundi yao kabla ya kwenda kwenye mtoano, ambako Ujerumani iliwafunga wapinzani wake wote na kufuzu fainali, wakati Brazil iliruhusu bao moja tu kwa England. 
Ujerumani iliwaondoa Marekani na wenyeji-wenza Korea Kusini, wakati Brazili iliitoa England.
Taji hilo la tano la Brazil kwenye Kombe la Dunia hakuna timu ambayo imeifikia rekodi hiyo, na katika mechi hiyo Brazil ikaweka rekodi ya kushinda mechi zote saba bila kuingia katika muda wa nyongeza au penalti. 
Ujerumani ilipoteza mchezo wa fainali kwa mara ya nne, na kuweka rekodi nyingine ya Kombe la Dunia. Walikuwa wamejiandaa kuifikia rekodi ya Brazil ya kutwaa taji hilo mara nne, kwani mpaka wakati huo ilikuwa imetwaa mara tatu.
Katika fainali hizo Ujerumani ilikuwa Kundi E pamoja na Jamhuri ya Ireland, Saudi Arabia na Cameroon na katika mechi yao ya kwanza waliichabanga Saudi Arabia mabao 8-0 kwenye Uwanja wa Sapporo Dome huku Miroslav Klose akipiga hat-trick. 
Katika mechi yao ya pili Ujerumani iliongoza kwa muda mrefu kwa bao 1-0, lakini katika dakika za majeruhi Robbie Keane akaisawazishia Ireland. Ikiwa inahitaji ushindi ili iongoze kundi hilo, Ujerumani ikaichapa Cameroon 2-0 kwenye Uwanja wa Shizuoka, huku Klose akifunga bao lake la tano la mashindano lililomfanya aibuke mfungaji bora.
Katika hatua ya mtoano Ujerumani ilipambana na Paraguay na kuifunga 1-0 kabla ya kutoa kipigo kama hicho kwa Marekani katika robo fainali.
Ujerumani ilikutana na Korea Kusini kwenye nusu fainali katika mchezo ambao ilijihami zaidi. Kabla ya kupatikana kwa bao lolote, Michael Ballack wa Ujerumani akapewa kadi ya pili ya njano katika dakika ya 71 na kumfanya akose mchezo unaofuata. Lakini ni Ballack huyo aliyefunga bao la ushindi dakika nne kabla ya mchezo kumalizika.
Brazil yenyewe ilikuwa Kundi C pamoja na China, Costa Rica na Uturuki. Kufuatia kupoteza mchezo wa fainali mwaka 1998, Brazil ilikuwa na kocha mpya, Luiz Felipe Scolari, ambaye alikuja na staili ya kucheza kwa kutumia nguvu.
Katika mchezo wa kwanza na Uturuki Brazil ilishinda kwa mabao 2-1 na mchezo uliofuata dhidi ya China kwenye Uwanja wa Ulsan Munsu ikapata ushindi wamabao 5-2 yaliyofungwa na Roberto Carlos, Rivaldo, Ronaldinho, na Ronaldo akifunga mawili.
Katika mechi yao ya mwisho dhidi ya Costa Rica wakapata ushindi mwingine wa mabao 5-2, Ronaldo akifunga mawili.
Kwenye hatua ya mtoano Brazil ilikumbana na washindi wa pili wa Kundi H Ubelgiji ambapo Rivaldo na Ronaldo waliipatia ushindi wa mabao 2-0 na kukumbana na kibarua cha England kwenye robo fainali. Michael Owen aliifungia England katika dakika ya 23 lakini Rivaldo na Ronaldinho wakafunga na kuipatia ushindi wa 2-1 ingawa Ronaldinho alitolewa nje.
Kwenye nusu fainali Brazil ikakutana na Uturuki kwa mara ya pili katika Uwanja wa Saitama na Ronaldo akafunga bao katika dakika ya 49 lililoisukuma Brazil fainali.
Zaidi ya nchi 200 ziliutangaza mchezo wa fainali kupitia radio na televisheni ambapo kwa ujumla wake vituo 232 vya TV viliuonyesha ikiwa ni rekodi mpya kabla haijavunjwa mwaka 2006. Zaidi ya watazamaji milioni 63 waliutazama mchezo huo kupitia kwenye luninga.
Vikosi vya siku hiyo vilikuwa; Ujerumani: Oliver Kahn (nahodha), Thomas Linke, Carsten Ramelow, Christoph Metzelder, Torsten Frings, Dietmar Hamann, Jens Jeremies/Gerald Asamoah 77', Marco Bode/Oliver Bierhoff 74', Bernd Schneider, Miroslav Klose (kadi ya njano 9')/Christian Ziege 84', Oliver Neuville. Kocha alikuwa Rudi Völler.
Brazil: Marcos, Lúcio, Edmílson, Roque Júnior (kadi ya njano 6'), Cafu (nahodha), Gilberto Silva, Kléberson, Roberto Carlos, Ronaldinho/Juninho 85', Rivaldo, Ronaldo/Denílson 90'. Kocha alikuwa Luiz Felipe Scolari, ambaye anaifundisha tena mwaka huu.

Ujerumani yalichabanga Argentina 4-2
Lakini siku kama ya leo, mwaka 2006 kule Ujerumani, wenyeji walifanikiwa kuvuka hatua ya robo fainali kwa mikwaju ya penalti 4-2 dhidi ya Argentina baada ya matokeo ya dakika 120 kuwa bao 1-1.
Huu ndio ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Argentina kufungwa kwa penalti kwenye Kombe la Dunia: mpaka kufikia mechi hiyo Argentina na Ujermnai zilikuwa zimeshiriki mara tatu katika upigaji wa penalti, na zote zikashinda.
Mjini Gelsenkirchen, England ilikumbana na Ureno na Wayne Rooney akatolewa nje, Ureno ikashinda kwa mikwaju ya penalti 3-1 baada ya matokeo ya dakika 120 kuwa 0-0 hivyo ikasonga mbele kwenye nusu fainali kwa mara ya kwanza tangu zama za Eusébio miaka 40 nyuma, na kumhakikishia kocha Luiz Felipe Scolari ushindi wake wa tatu mfululizo wa robo fainali dhidi ya kikosi cha England chini ya Sven-Göran Eriksson.
Julai Mosi Italia iliifunga Ukraine 3-0 iliyofuzu kwa mara ya kwanza kwenye robo fainali. Ufaransa ikaichapa Brazil 1–0. Brazil ilipiga shutimoja tu golini katika mechi hiyo ambayo ilishuhudia 'uchawi' wa chenga kwenye kiungo wa Zinedine Zidane ambaye pasi yake ya mpira wa adhabu kwa Thierry Henry ndiyo iliyozaa bao la ushindi.

Hungary yaifunga Uruguay 4-2
Aidha, tarehe kama ya leo miaka 60 iliyopita, yaani mwaka 1954, ulichezwa mchezo wa nusu fainali baina ya Hungary na Uruguay ambapo Hungary ilishinda kwa mabao 4-2 baada ya dakika 120.
Mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Stade Olympique de la Pontaise, jijini Lausanne, Uswisi na kuhudhuriwa na watazamaji 37,000, ulichezeshwa na mwamuzi Benjamin Griffiths kutoka Wales.
Mabao ya Hungary yalifungwa na Czibor 13', Hidegkuti 46', na Kocsis 111', 116' wakati yale ya Uruguay yalifungwa na Hohberg 75', 86'.
Katika nusu fainali ya pili siku hiyo, Ujerumani iliichakaza Austria kwa mabao 6-1 katika Uwanja wa St. Jakob, mjini Basel mbele ya watazamaji 58,000 huku mwamuzi akiwa Mtaliano Vincenzo Orlandini.
Mabao ya Wajerumani yalifungwa na Schäfer 31', Morlock 47', F. Walter 54' (pen.), 64' (pen.), na O. Walter 61', 89' wakati lile la Austria lilifungwa na Probst 51'.
Hatimaye Ujerumani ndiyo iliyotwaa ubingwa mwaka huo kwa kuifunga Hungary 3-2 kwenye fainali, huku mabao yake yakifungwa na Morlock 10', Rahn 18', 84', na yale ya Hungary yakifungwa na Puskás 6' na Czibor 8'.
Mchezo huo uliofanyika Julai 4 katika Uwanja wa Wankdorf mjini Bern mbele ya watazamaji 60,000 ulichezeshwa na Mwingireza William Ling.
Mfungaji bora wa mashindano hayo alikuwa Sándor Kocsis wa Hungary aliyezifumania nyavu mara 11.

Argentina 1-2 Brazil
Kwa siku kama ya leo, miaka 40 iliyopita katika fainali zilizofanyika Ujerumani Magharibi, Argentina ilikubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Brazil katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Niedersachsenstadion, mjini Hanover na kuhudhuriwa na mashabiki 38,000.
Mchezo huu wa raundi ya pili uliochezeshwa na mwamuzi Vital Loraux wa Ubelgiji ulishuhudia Brazil ikianza kufunga kupitia kwa Rivellino katika dakika ya 32 kabla ya Brandisi kusawazisha dakika ya 35. Jairzinho aliipatia Brazil bao la ushindi dakika ya 49.
Katika mchezo mwingine wa mtoano, Ujerumani Mashariki nayo ilichapwa mabao 2-0 na Uholanzi ambayo yalifungwa na Neeskens katika dakika ya 7 na Rensenbrink dakika ya 59.
Mchezo huo ulifanyika kwenye Uwanja wa Parkstadion, Gelsenkirchen ukihudhuriwa na watazamaji 67,148, ambapo mwamuzi alikuwa Rudolf Scheurer wa Uswisi.
Siku hiyo Poland nayo ikicheza kwenye Uwanja wa 
Waldstadion, jijini Frankfurt mbele ya watazamaji 55,000, iliweza kuichapa Yugoslavia mabao 2-1 kupitia kwa Deyna aliyefunga kwa penalti dakika ya 24 na Lato dakika ya 62, wakati Karasi aliifungia Yugoslavia dakika ya 43. Mwamuzi alikuwa Rudi Glöckner wa Ujerumani Mashariki.
Wenyeji Ujrumani Magharibi, ambao ndio baadaye walikuja kuwa mabingwa, siku hiyo waliichabanga Sweden kwa mabao 4-2 katika Uwanja wa Rheinstadion, huko Düsseldorf mbele ya mashabiki 66,500.
Wafungaji wa Ujerumani walikuwa Overath dakika ya 51, Bonhof dakika ya 52, Grabowski dakika ya 76 na Hoeneß alifunga kwa penalti dakika ya 89, wakati yale ya Sweden yalifungwa na Edström   dakika ya 24 na Sandberg dakika ya 53. Mwamuzi alikuwa Pavel Kazakov wa Urusi.

Argentina yashinda kwa matuta
Mabingwa watetezi, Argentina, siku kama ya leo miaka 24 iliyopita (mwaka 1990) kule Italia ilijikuta ikivuka kwa mbinde hatua ya robo fainali mbele ya Yugoslavia ambayo ilicheza na watu 10 kwa dakika 90.
Baada ya dakika 120 bila bao ikabidi mikwaju ya penalti ipigwe, ndipo Argentina ikavuka kwa mikwaju 3-2, huku penalti ya Diego Maradona ikiokoloewa.
Aliyewaokoa Argentina siku hiyo ni kipa Sergio Goycochea (aliyechukua nafasi ya Nery Pumpido aliyevunjika mkuu katika hatua ya makundi) ambaye aliokoa penalti mbili za Yugoslavia huku Pedro Troglio akiwa ameikosesha Argentina penalti nyingine ambayo ingewatoa mashindanoni.
Ireland nayo ilibanjuliwa na Italia kwa bao 1-0 la Salvatore Schillaci katika hatua hiyo, wakati ambapo Ujerumani Magharibi waliichapa Czechoslovakia bao 1-0 ka mkwaju wa penalti wa Lothar Matthäus.
Mechi iliyokuwa inatazamwa na wengi siku hiyo ya Juni 30 ilikuwa baina ya England na Cameroon, ambayo ilikuwa imeonyesha maajabu makubwa kwenye fainali hizo.
Ndiyo mechi pekee ya robo fainali ambayo ilikuwa na goli zaidi ya moja, kwani England ilishinda kwa mabao 3-2 baada ya dakika 120.
Kwanza England ilipata bao kupitia kwa David Platt katika dakika ya 25. Lakini baada ya mapumziko mkongwe Roger Milla akaingizwa na kuubadili mchezo ndani ya sekunde tano ambapo Cameroon walipata penalti iliyofungwa na Emmanuel Kunde. Baadaye katika dakika ya 65, Eugene Ekeke akafunga bao la kuongoza. Waafrika wakajua wanakwenda nusu fainali, lakini wakasababisha penalti ambayo ilifungwa na Gary Lineker. Katikati ya muda wa ziada, England wakapata penalti nyingine ambayo ilifungwa na Lineker na wakauzu kwa nusu fainali.

Croatia yaicharaza Romania
Siku kama ya leo, lakini mwaka 1998 ule Ufaransa, Croatia ikishiriki kwa mara ya kwanza fainali za Kombe la Dunia iliicharaza Romania kwa bao 1-0 katika mchezo wa robo fainali baolililofungwa kwa mkwaju wa penalti na Davor Å uker katika dakika za majeruhi za kipindi cha kwanza. Mchezo huo ulifanyika kwenye Uwanja wa Parc Lescure, mjini Bordeaux mbele ya mashabiki 31,800 na ulichezeshwa na Javier Castrilli wa Argentina.
Mchezo mwingine wa siku hiyo ulikuwa baina ya Argentina na England ambazo hadi dakika 120 zinamalizika matokeo yalikuwa 2-2. Gabriel Batistuta aliifungia Agentina bao la kuongoza kwa mkwaju wa penalti dakika ya 6, lakini Alan Shearer akasawazisha kwa penalti dakika ya 10 kabla ya Michael Owen kuongeza la pili dakika ya 16. Zanetti alisawazisha mambo kwenye dakika ya 45, matokeo ambayo yalidumu hadi dakika 120 zinamalizika.
Katika mikwaju ya penalti, Argentina ilipata nne na England wakapata tatu, hivyo Waingereza wakatolewa. Mchezo huo ulifanyika kwenye Uwanja wa Geoffroy-Guichard, mjini Saint-Étienne mbele ya watazamaji 30,600 na ulichezeshwa na  Kim Milton Nielsen wa Denmark.


MECHI YA 26 BRAZIL VS COLOMBIA, BRAZIL YASHINDA MARA 15, COLOMBIA MARA MBILI TU

Neymar wa Brazil akishangilia ushindi

Na Daniel Mbega

MECHI ya robo fainali baina ya Brazil na Colombia ni ya kwanza kabisa kwa timu hizo mbili za Amerika Kusini kupambana kwenye mashindano ya fainali za Kombe la Dunia, lakini ni ya 26 kuzikutanisha timu hizo katika historia yao.
Ukitazama rekodi vitabuni, unaweza kusema kwamba Colombia ni vibonde wa Brazil, kwani katika mechi 25 walizocheza tangu mwaka 1945 mpaka sasa, Brazil imeshinda jumla ya 15, kutoka sare mara nane na kufungwa mechi mbili tu.
Kwa ujumla wake, Brazil imefunga mabao 55 na kufungwa 11, ikiwa ni rekodi kubwa mno ya mabao.
Timu hizo zimepambana mara 10 katika mashindano ya awali ya Kombe la Dunia ambapo katika mechi hizo Brazil imeshinda mara tano na kutoka sare mara tano pia.
Aidha, katika mashindano ya Ubingwa wa Amerika Kusini maarufu kama Copa America (zamani yakijulikana kama South American Championship), timu hizo zimepambana mara tisa na Brazil imeshinda mara saba, kutoka sare moja na kupoteza moja.
Zilipopambana katika mashindano ya 7 ya Kombe la Dhahabu (Gold Cup) kule Miami, Marekani mwaka 2003, Brazil ilishinda kwa mabao 2-0.
Katika mechi za kirafiki, timu hizo zimepambana mara tano, na hapa pia Brazil ikashinda mara mbili, sare mbili na kupoteza mechi moja.
Kwa rekodi hizo, haijajulikana mchezo wao war obo fainali utakuwa na matokeo gani, ingawa kwa ujumla mpira unadunda na mpaka filimbi ya mwisho itakapopulizwa ndipo mwamba atakapojulikana. Na hapa ijulikane wazi kwamba hakutakuwa na sare, lazima mshindi apatikane hata kwa shilingi.

Takwimu kamili ni hizi:

Ubingwa wa Amerika Kusini
21/01/1945 Colombia 0-3 Brazil - Santiago, Chile
17/04/1949 Brazil 5-0 Colombia - São Paulo, Brazil
24/03/1957 Colombia 0-9 Brazil - Lima, Peru
14/03/1963 Brazil 5-1 Colombia - La Paz, Bolivia
07/07/1989 Brazil 0-0 Colombia – Salvador, Brazil
13/07/1991 Colombia 2-0 Brazil РVi̱a del Mar, Chile
19/07/1991 Brazil 2-0 Colombia – Santiago, Chile
13/07/1995 Colombia 0-3 Brazil – Rivera, Uruguay
19/06/1997 Brazil 2-0 Colombia – Santa Cruz, Bolivia

Michuano ya awali Kombe la Dunia
06/08/1969 Colombia 0-2 Brazil – Bogotá , Colombia
21/08/1969 Brazil 6-2 Colombia – Rio de Janeiro, Brazil
20/02/1977 Colombia 0-0 Brazil – Bogotá, Colombia
09/03/1977 Brazil 6-0 Colombia – Rio de Janeiro, Brazil
28/03/2000 Colombia 0-0 Brazil – Bogotá, Colombia
15/11/2000 Brazil 1-0 Colombia РṢo Paulo, Brazil
07/09/2003 Colombia 1-2 Brazil – Barranquilla, Colombia
13/10/2004 Brazil 0-0 Colombia – Maceio, Brazil
14/10/2007 Colombia 0-0 Brazil – Bogotá, Colombia
15/11/2008 Brazil 0-0 Colombia – Rio de Janeiro, Brazil

Gold Cup
19/07/2003 Brazil 2-0 Colombia – Miami, Marekani

Mechi za kirafiki
01/02/1981 Colombia 1-1 Brazil – Bogotá, Colombia
25/04/1985 Brazil 2-1 Colombia – Belo Horizonte, Brazil
15/05/1985 Colombia 1-0 Brazil – Bogotá, Colombia
20/12/1995 Brazil 3-1 Colombia – Manaus, Brazil
15/11/2012 Colombia 1-1 Brazil – New Jersey, Marekani

                       P     W   D   L   F-    A   PTS
Brazil                  25    15     8     2     55-  11    53
Colombia          25      2     8   15     11-   55   14

ROBBEN AMEKIRI KUJIANGUSHA


Arjen Robben amekiri kuwa alidanganya timu yake ikapewa penati.

Mshambulizi wa Uholanzi Arjen Robben amekiri kuwa alidanganya timu yake ikapewa penalti ya ushindi lakini akasema alikuwa ametegwa .
Kocha wa Mexico Miguel Herrera amemkashifu refarii wa mechi yao na Uholanzi Pedro Proenca kwa kuipendelea Uholanzi .

Herrera amesema kuwa Penalti hiyo dakika tatu kabla ya kukamilika kwa mechi hiyo haikufaa''hiyo ni njama ya FIFA kuiondoa Mexico kwenye kinyang'anyiro hicho .
Robben alikunguwa katika eneo la lango Uholanzi ilipokuwa imesawazisha bao moja kwa moja na ikaisaidia Uholanzi kuibuka mshindi kwa mabao 2-1 .
Penalti hiyo ilifungwa na Jan-Klaas Huntelaar

“nataka kwanza kuwaomba radhi mashabiki wangu kwa kudanganya na kujiangusha ukweli haikufaa '' Robben aliiambia runinga ya Uholanzi NOS.
''nafikiri kuwa refarii Proenca alifanya kweli kuashiria penalti akisema kuwa alikuwa ametegwa na nahodha wa Mexico Rafael Marquez.
Mexico ilikuwa imeongoza hadi dakika ya 88 ya kipindi cha pili kabla Wesley Sneijder kuisawazishia Uholanzi kabla ya Huntelaar kufunga penalti iliyozua ubishi mkubwa.
Herrera alisema kuwa haikufaa refarii kutoka ulaya alipewa mechi kati ya timu kutoka ulaya na Marekani ya kusini.
Kwanini FIFA hawakutupa refarii mwafrika mhindi ama hata refarii kutoka Marekani kusini ?

 CHANZO, BBC SWAHILI


WASHIRIKI 20 WA SHINDANO LA TMT WAINGIA RASMI KAMBINI JANA USIKU, TAYARI KWA SAFARI YA KUWANIA MILIONI 50

IMG_0474
Muonekano wa TMT House ambayo washiriki 20 wa Shindano la Tanzania Movie Talents wameweka kambi rasmi kuanzia jana Usiku kwa mchakato wa kuwania Milioni 50 katika fainali itakayofanyika Mwishoni mwa Mwezi wa nane.
IMG_0507
Mmoja kati ya Washindi watatu kutoka Kanda ya Kusini, Mwanaafa Mwizago akiingia rasmi kambini hapo jana wakati wakitokea kwenye matembezi. Washiriki wote 20 ambao ni washindi kutoka Kanda sita za Tanzania sasa wapo kambini kwaajili ya kujifua ili kuwania kitita cha Shilingi Milioni 50 katika fainali kubwa itakayofanyika mwisho wa Mwezi wa nane.
IMG_0509
IMG_0510
Baadhi ya washiriki wa Fainali ya Shindano la TMT wakiingia kambini hapo jana Usiku.
IMG_0516
Washiriki wakiwa ndani ya Nyumba ya TMT tayari kwa kambi.
IMG_0522
Washiriki wakipewa maelekezo mara baada ya kuwasili kambini hapo jana.(Picha zote na Josephat Lukaza – Lukaza Blog).
Na Josephat Lukaza – Proin Promotions – Dar Es Salaam.
Washiriki 20 kutoka Kanda sita za Tanzania wameingia rasmi kambini hapo Jana mara baada ya kumaliza zoezi la Kupima Afya, kutembezwa sehemu mbalimbali za Jiji la Dar pamoja na Ofisi za Global Publishers.
Washiriki hao watakaa kambini kwa Siku 64 ambapo wataanza rasmi kufundishwa Hapo kesho siku ya Jumatatu na walimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na Chuo Cha Sanaa Bagamoyo ambapo baadae sasa baadae zoezi la kuanza kuwapigia kura washiriki hao litaanza na hatimaye watanzania ndio watakuwa majaji kwa washiriki hao ambapo mshindi mmoja wa Shilingi Milioni 50 atapatikana katika Fainali itakayofanyika Mwishoni mwa Mwezi wa Nane.
Zoezi la Upigaji kura litaanza mapema wiki ijayo ambapo washiriki wote watakuwa tayari washapewa namba za ushiriki na hatimaye watanzania kuweza kuwachagua washiriki wanaowaona wana vipaji.
Zoezi hili la kupiga kura litapelekea Washiriki wawili kuondolewa kila wiki katika Kambi ya TMT ambapo pona yao ni kutoka kwa Watanzania ambao ndio watakuwa majaji kwa kuwapigia kura.
Vilevile Mara baada ya washindi hawa wa kanda kuingia kambini Vipindi vyetu vitaendelea Kurushwa kila siku ya Jumamosi Saa 4 Usiku na Kurudiwa kila Siku ya Jumapili Saa 10 Jioni na Jumatano Saa tano usiku kupitia Runinga ya ITV.
Tunawaomba watanzania kuendelea kutizama vipindi vyetu kwani vimekuwa na mvuto wa hali ya juu sana lakini pia kuendelea kuwawezesha Washiriki wanaowaona wana vipaji ili kuwa ushindi.
Namba za washiriki zitaanza kuonekana katika Kipindi chetu kijacho ambapo Sasa watanzania wataanza kuwapigia kura kwenda namba 15678
Na ili kuweza Kufahamu taarifa zaidi za TMT unaweza kutuma neno “TMT” kwenda namba 15678.

CHANZO MO BLOG