Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 27 June 2014

PANONE FC KUSAJILI WACHEZAJI NDANI NA NJE YA NCHI.

indexMabingwa wa mkoa Kilimanjaro timu ya Panone Fc yenye makazi yake mjini Moshi inatarajia kufanya usajili wa wachezaji 6 kutoka  vilabu mbalimbali  vya  ndani na nje ya nchi. 
Afisa habari wa timu ya Panone Cassimu Mwinyi alisema kuwa  timu hiyo itafanya usajili huo ili kuiongezea timu ngvu mpya wakichanganya na wachezaji waliopo kutokana na mipango waliyojiwekea ya kuhakikisha  timu inafuzu kucheza katika michuano ya ligi kuu.
 
“Nia yetu ni  kuweza kupata vijana  wenye vipaji na watakaojituma zaidi katika mchezo kwani huu  ni wakati wao muafaka  wa kuweza kuijenga timu imara vile vile kuwaweka pamoja na kufanya mpira kuwa ajira yao itakayo   wasaidia kuepukana na vitendo viovu ikiwemo utumiaji wa madawa ya kulevya,  .”alisema Mwinyi.
 
Kwa upande wa meneja wa timu hiyo  Gido Marandu yeye amezungumzia mipango ya timu ikiwa ni pamoja na  kuhakikisha wanacheza mechi nyingi za kirafiki ili kuwawezersha vijana kuelewana.
 
“Tunatarajia kuialika timu ya simba sc kucheza naye mchezo wa kirafiki katika kujiweka sawa  vile vile    uongozi wa timu upo katika maandalizi  ya kuandaa hafla kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji wao kwa juhudi kubwa walioifanya katika kuiwezesha timu kushiriki ligi daraja la kwanza ambapo hafla hiyo itafanyika baada ya wachezaji kutoka likizo.”alisema Marandu
 
 Huku akiwasihi wadau wote wa soka waendelee kuonyesha ushirikiano kwa timu  yao hasa katika kuiunga mkono katika kinyang’anyiro cha kuelekea kushiriki  ligi daraja la kwanza ili iweze kushinda na kuwakilisha vyema mkoa msimu ujao wa  ligi kuu soka Tanzania bara.

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment