Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 25 June 2014

WANAOUPINGA UONGOZI CHADEMA WATINGA KWA MSAJILI, CAG


TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU WAJUMBE WA BARAZA KUU NA MKUTANO MKUU WA CHADEMA KWENDA KWA MSAJIRI WA VYAMA VYA SIASA NA KWA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI.


A.UTANGULIZI

Ndugu wanaHabari,

Mtakumbuka kwamba Juzi, katibu wa CHADEMA mkoa wa Tabora kwa niaba yetu wajumbe 78 wa baraza kuu na viongozi wengine wa mabaraza ya vijana na wanawake 4 kufanya kuwa jumla ya wajumbe 82 kwa pamoja tulizungumza na waandishi wa habari kuzungumzia maswala mbali mbali yanayotishia ustawi wa chama chetu.

Na mtakumbuka kwamba tuliazimia kwamba tutakwenda kumuona msajiri wa vyama vya siasa ili tumpatiemalalamiko yetu haya.

B. KWENDA KWA MSAJIRI WA VYAMA VYA SIASA.

Ndugu wanaHabari, Mapema leo Tumekwenda ofisini kwa msajiri wa vyama vya siasa na
tumekabidhi barua yenye malalaiko mbali mbali juu ya uvunjifu ya KATIBA unaofanywa kihuni na kwa makusudi na viongozi wetu wa CHADEMA hasa mwenyekiti Mbowe na Katibu mkuu SLAA. Tunaambatanisha na nakala ya barua tuliyoipeleka kwa msajiri.

C. KWENDA KWA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI.

Ndugu wanaHabari, Kutokana na Ukweli kwamba viongozi wetu hasa Mwenyekiti Mbowe na Katibu Mkuu SAA, wanahusika moja kwa moja na Ubadhirifu wa fedha za chama zinazotokana na kodi za Umma, za zaidi ya BILIONI 10.038 na wao wanasema hayo madai siyo mapya na kwamba wameyazoea.

Hivyo basi tumepeleka kwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, barua yenye kuomba kupatiwa nakala ya Taarifa ya Ukaguzi wa hesabu za CHADEMA baada ya ofisi yake kukamilisha ukaguzi huo.

Pia pamoja na kuomba Nakala hiyo, tumeomba pia mkaguzi azitoe taarifa hizo hadharani ili wanachama wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla waone kilichopo ndani yake.

D. MSINGI WA HOJA ZETU.

Tunamuomba katibu mkuu wa chama, ajibu hoja zetu na aache kuleta viroja kama ambavyo amenukuliwa na vyombo vya hbari jana.

Msingi wa hoja zetu sisi ni katibu mkuu kujilip zaidi ya million 130 kwa mwaka huku makatibu wake wa mikoa, wilaya na kata wakilipwa shilingi 0.

Msingi wa hoja zetu ni katibu mkuu SLAA kujikopesha zaidi ya Millioni 160 kwenda kumalizia deni la nyumba yake bila kufuata utaratibu wowote wa kukopa.

Msingi wa hoja zetu ni kitendo cha mbowe kutukodishia magari yake kwa mamillioni ya pesa kila tunapotumia, halafu yanapokuwa chakavu anatuuzia FUSSO MBILI chakavu  kwa million 600.

Msingi wa hoja zetu ni kitendo cha MBOWE kukiuzia chama VX V8 MBILI ambazo amenunua kwa pesa za chama halafu anazisajiri kwa jina la MBOWE HOTELS.
Hiyo ndio misingi ya hoja zetu, Slaa alitakiwa kujibu hoja hoja hizi, aeleze ni kwanini anatumia vibaya pesa za umma hata kabla hajaingia madarakani, SLAA aeleze kama leo tupo wapinzani tunachezea katiba hivi, je tukiingia madarakani tutakuwaje?

SLAA aeleze kama sisi viongozi wake wa wilaya ni WAJINGA, nay eye ndio katibu mkuu wetu, sasa je yeye ni KUBWA JINGA?, AU MJINGA MKUU?, AU ZEZETA? Unawezaje kukaa na viongozi WAJINGA, ukawaomba ushauri, ukawatumia halafu wakikusoa ndio ukawajua kuwa WAJINGA, je SLAA sio MJINGA ZAIDI YETU?

E. KUHUSU KUWAKANA WAJUMBE NA WANACHADEMA.

Ni vema mkatambua kuwa viongozi wakuu wa CHADEMA wanakimbilia Kuwakana wanachama na viongozi wake pindi linapotokea swala bila kujibu vilivyopo ndani ya swala hilo, jana wamemkana JOSEPH YONAH ambaye ni mwenyekiti halali wa CHADEMA wilaya ya temeke kiasi cha mwanzoni mwa mwaka huu KUMTEKA NA KUMTESA.
Lakini pia huu hapa ni mwendelezo wa tabia ya CHADEMA KUWAKANA VIONGOZI WAO NA MATENDO YAO.

·         Alipouwawa CHACHA WANGWE, na ilipotangazwa kwamba wakati anauwawa alikuwa na ndugu DEUS MALLYA ambaye ni mwanaChama wa CHADEMA kwenye Gari, asubuhi yake, Ndugu John Mnyika, alimkana na kusema hamtambui na kwamba serikali iseme DEUS MALLYA NI NANI na anatokea wapi?, na mambo mengineyo, na DEUS MALLYA naye akajidai hamjui, alipotoka GEREZANI akamuomba msamaha kwa kumkana.
   
·         Alipojihudhuru uenyekiti wa Mkoa wa SINGIDA muasisi wa CHADEMA mkoani Humo, ndugu Wilfred Kitundu, Chadema badala ya kujibu hoja zake Walimkana

·         Alipojiondoa chamani katibu wa sekretariety na muajiriwa wa chama ambaye pia ni mwenyekiti wa mkoa wa Lindi, ndugu Ally Chitanda, chadema hakujibu hoja zake wakamkana

·         Mzee EDWIN MTEI alipotoa kauli kwamba TUME YA MABADILIKO YA KATIBA ni ya KIDINI na kwamba KIKWETE ameteua WAISLAM WENGI kuliko wakristo, MBOWE AKAMKANA

·         JOSHUA NASSARY alopotoa kauli kwamba mikoa ya KASKAZINI itajitenga na kuanzisha nchi yao ya JAMUHURI YA KASKAZINI, Mbowe akamkana.

·         Hata MBOWE mwenyewe alipotangaza Hadharani kwamba amerudisha gari la kiongozi wa UPINZANI BUNGENI na kwamba halitaki tena, AKAJIKANA na AKAENDELEA KULITUMIA MPAKA LEO

·         Hata MNYIKA na LISSU na wabunge wengine walipotangaza kutokuchukua POSHO BUNGENI, WALIJIKANA NA WANAENDELEA KUCHUKUA MPAKA SASA

·         Hata MBOWE na SLAA  walipotangaza kwamba CUF ni CCM B na MBATIA ni kibaraka wa CCM WAKAJIKANA na leo Wamejiingiza humo humo na kuungana nao
Hivyo tunawataka wawe na hulka za kujibu hoja na sio kukimbilia kuwakana watu ambao ni wanachama halali.

Sasa kama kilan atakayekosoa anakanwa, nani atabaki?, nani mwanachama halali, MBOWE na SLAA TU ama?

Tamko hili limesomwa leo 25.6.2014 na;-
JORUM ABDALLAH MBOGO

………………………………………..

MWANACHAMA WA CHADEMA
MWENYEKITI WA CHA CHADEMA WILAYA YA KALIUA
MJUMBE WA BARAZA KUU LA CHADEMA TAIFA
MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CHADEMA TAIFA.

Tunaambatanisha na nakala za Barua za kwa Msajiri na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu.


                                                                                                    JORUM  ABDALLAH MBOGO
                                                                                                                              S.L.P  1110
                                                                                                                              TABORA
                                                                                                                              25.06.2014
MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
MTAA WA SAMORA NA OHIO
S.L.P 9080
DAR ES SALAAM
DAR ES SALAAM.    
   
                      Ndugu.
YAH: MAOMBI YA TAARIFA YA UKAGUZI WA CHADEMA.
Husika na somo hapo juu.

Mimi ni mwanachama na kiongozi wa ngazi ya wilaya wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la chama

Kwa kipindi kirefu ndani ya chama chetu tumekuwa tukilalamikia matumizi mabaya ya pesa hasa za ruzuku, pesa ambazo msingi wake ni kodi za wananchi na hivyo kuwa ni pesa za umma. Hii inatokana na ukweli kwamba mpaka sasa chama kimepokea jumla ya BILION 10.038 kama ruzuku kutoka serikali kuu, kwa kipindi cha miezi 42 kutokea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010

Tumejitahidi sana kudai taarifa sahihi za matumizi ya pesa hizo bila mafanikio.
Kwa kuwa tunatambua kwamba ni hivi karibuni tu, ofisi yako imemaliza kufanya UKAGUZI MAALUM WA MAHESABU KWA VYAMA VYA SIASA kikiwemo na CHADEMA, na kwamba taarifa yake mmeshaiwasilisha Bungeni.

Kutokana na ukweli kwamba wengi wetu sisi sio wabunge na hatuna uwezo wa kuipata hiyo Taarifa ambayo ni muhimu sana.

Na kwa kuzingatia kwamba sisi ndio wenye chama na sisi ndio walipa kodi zinazoipatia chama Ruzuku. Ni wajibu wetu kusimamia matumizi yake.

Hivyo basi, kwa niaba ya viongozi na wanachama wenzangu wasiopungua 82, tunaiomba ofisi yako itusaidie yafuatayo

1.    ITUPATIE NAKALA YA TAARIFA ILIYOKAGULIWA
2.    IITOE NAKALA HIYO KWA UMMA ILI UMMA UJUE NAMNA KODI ZAO ZINAVYOTUMIWA

Tunatumaini kwamba Ombi letu litashuhulikiwa kwa uzito na umuhimu wa kipekee

Tunatanguliza shukrani zetu za dhati.


Wako katika ujenzi wa Taifa

……………………………………………………

JORUM ABDALLAH MBOGO

MWANACHAMA WA CHADEMA
MWENYEKITI WA CHA CHADEMA WILAYA YA KALIUA
MJUMBE WA BARAZA KUU LA CHADEMA TAIFA
MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CHADEMA TAIFA.

Nakala :- Vyombo vya habari




                                                                                                                   JORUM  ABDALLAH MBOGO
                                                                                                                              S.L.P  1110
                                                                                                                              TABORA
                                                                                                                              25.06.2014
MSAJIRI WA VYAMA VYA SIASA
S.L.P  63010
DAR ES SALAAM
TANZANIA

   Ndugu,
YAH: MAOMBI YA UFAFANUZI WA KIKATIBA JUU YA UVUNJIFU WA KATIBA NA YA  CHAMA UNAOFANYWA NA VIONGOZI
 Mheshimwa Msajiri, Somo hapo juu la husika.
Mimi ni mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,

Kwa niaba ya wanachama wenzangu, tunaleta kwako malalamiko ya uvunjifu wa  katiba ya chama Yanayotokana na matamko yanayoendelea kutolewa na viongozi wa kitaifa juu ya kuungana na UKAWA yenye tafsiri kwamba wataachiana majimbo ya kugombea ili waweze kuingia madarakani na kuunda serikali ya pamoja.

 kama hivyo ndivyo  wanakiuka  SURA YA TISA. IBARA YA 9.3.1 ya KATIBA YA CHADEMA  inayosema ‘’chama kinaweza kuunda mseto na chama au vyama vingine vyenye madhumuni na malengo yanayofannaili kuimarisha iwezo wa kushinda uchaguzi mkuu au wa serikali moja ya mtaa kwa lengo la kuunda utawala wa pamoja’’

Kwa kuwa viongozi wa CHADEMA na CUF na NCCR wameungana na kuunda chama kingine cha UKAWA kwa mujibu wa SURA YA TISA ibara ya 9.3.3 ‘’chama kinaweza kuungana na chama ama vyama vingine kuunda chama kipya’’  hivyo wamevunja SURA TISAIbara ya 9.3.4 inayosema ‘’Uamuzi kuhusu vipengere 9.3.1, na 9.3.3 utafanywa na mkutano mkuu wa Taifa na kuhusu kipengere 9.3.2 na Baraza KUU’’.

Na hivyo sisi kama chama hatujakaa BARAZA KUU ili kupitisha AGENDA za huo mkutano mkuu na wala MKUTANO mkuu haujaitishwa kujadili maamuzi hayo yaliyofikiwa na viongozi wetu.

Mheshimiwa Msajiri, Tunafahamu kwamba KANUNI za chama SURA YA TISA kuanzia ibara ya 9.0 Mpaka ibara ya 9.7 zinatoa uhuru wa chama kuungana na kufanya ushirika na vyama vingine kwa kadri itakavyoona inafaa.

 Ila kanuni hizi zinaweka mkanganyiko wa kitafsiri, na hivyo zinazuiwa na kuuliwa nguvu na  Ibara ya 9.2.3 yaKATIBA YA CHAMA Inayosema ‘’kukitokea migongano kati ya kipengele cha katiba na kile cha kanuni, kipengele cha katiba kitatawala’’.  Hivyo kanuni zinazotoa uhuru huo haziwezi kutumika hapa.

Mheshimiwa msajiri, kwa kuwa wewe ndio mlezi na msimamizi wa vyama vyote vya siasa, na kwa kuwa hakuna chama cha siasa kilicho juu ya katiba yake, hivyo tunakuomba uingilie kati mgogoro huu wa uvunjifu wa katiba unaofanywa kwa makusudi na viongozi wa chama.

Tunakuomba pia uuagize uongozi wa kitaifa uitishe haraka kikao cha baraza kuu, kwani tumeshapitisha miezi mi nne sasa ya kisheria ambayo baraza kuu lilipaswa kukaliwa, mara ya mwisho tulikaa kikao cha baraza kuu mwezi febryary mwaka 2013, hivyo tulitakiwa tena tukae baraza kuu mwezi February mwaka huu. Hatujaitwa, wala hatujapewa sababu yoyote yenye mantiki.

Vile vile tunakuomba uwaagize viongozi wa chama waitishe chaguzi halali za zhama na waache kuchomeka watu wao wanaowataka kwa hila, kwa mujibu wa ratiba tulizozipitisha uchaguzi ulupiswa kuwa umeshafanyika kufikia December 2013, na baadae june 2014, lakini mpaka tunavyokuandikia leo, hakuna lililofanyika.

Tunakutakia kila la heri katika kutusaidia ufafanuzi huu.

Tunatanguliza shukrani za dhati na tukiamini swala letu litafanyiwa linavyostahili.

Wako katika ujenzi wa Taifa.  

                                             
JORUM ABDALLAH MBOGO

………………………………………..

MWANACHAMA WA CHADEMA
MWENYEKITI WA CHA CHADEMA WILAYA YA KALIUA
MJUMBE WA BARAZA KUU LA CHADEMA TAIFA
MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CHADEMA TAIFA.

Nakala :- Vyombo vya habari

No comments:

Post a Comment