Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 26 June 2014

NIGERIA YAPIGWA 3-2 NA ARGENTINA, LAKINI YAFUZU HATUA YA 16 KOMBE LA DUNIA

Star: Lionel Messi (above) hit a brilliant double to help Argentina defeat Nigeria
 Nyota: Lionel Messi (juu) aliifungia mabao mawili Argentina dhidi ya Nigeria.
 
TIMU ya Taifa ya Nigeria maarufu kama Super Eagles imefanikiwa kufuzu hatua ya 16 ya kombe la dunia licha ya kufungwa mabao 3-2 dhidi ya Argentina.
Mshambuliaji hatari wa kikosi cha Alejandro Sabella, Lionel Messi amefunga mabao mawili katika dakika ya 3 na 45  katika ushindi uliowapa Argentina ushindi wa asilimia 100 katika kundi lao la F.
Bao la tatu la Argentina limefungwa na Marcos Rojo katika dakika ya 50.
Mabao mawili ya Nigeria yamefungwa na Ahmed Musa katika dakika ya 4 na 47.
Katika michuano ya mwaka huu, dhahiri, Argentina inamtegemea zaidi Messi katika mechi zake.
Baada ya kufunga mabao hayo, kocha Sabella alimpumzisha nyota huyu wa FC Barcelona kwa ajili ya mikikimikiki ya hatua ya 16.
Pia Sabella alishuhudia mshambuliaji wake, Sergio Kun Aguero akitolewa nje ya uwanja kwa kile kilichoonekana kupata maumivu ya misuli tena.
Main man: Messi (right) put his side into a 1-0 with this strike after just three minutes
 Mtu muhimu: Messi (kulia) akifunga bao la kuongoza baada ya dakika tatu tu kupita
Thank you: Messi points to the sky in celebration after his first goal of the game
 Asante mungu: Messi akinyosha vidole kama ishara ya kumshukuru mungu baada ya kufunga .
Kusoma zaidi takwimu za mchezo bofya www.bkmtata.blogspot.com

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment