Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 27 April 2014

WAKULIMA 500 KUFUNDISHWA RASILIMALI FEDHA


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot.com, Arusha

ZAIDI  ya wakulima 500 kutoka katika Kanda ya Kaskazini wanatarajiwa kupewa elimu ya rasilimali fedha na kuongeza ufahamu na uelewa juu ya huduma mbalimbali za kifedha zitolewazo na benki.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wakulima wa Mbogamboga, Matunda na Viungo (TAHA) Jacqueline Mkindi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maonesho ya kuunganisha kilimo biashara na taasisi za kifedha yatakayofanyika April 25 na 26 mwaka huu katika viwanja vya AVDRC Tengeru.
Alisema kuwa, kwa sasa asilimia kubwa ya taasisi za kifedha zimekuwa zikiwakandamiza wakulima kwa kuwatoza riba kubwa kwenye mikopo hali ambayo imekuwa ikiwasababishia wakulima hao kupoteza imani na mikopo kutoka katika taasisi hizo.
Alidai kuwa hali hiyo imekuwa ni changamoto kubwa sana kwa wakulima hao,kwani wakati mwingine imewawia vigumu kushindwa kufikia malengo yao waliyojiwekea kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha katika kuendesha miradi yao midogomidogo.
"Kutokana na changamoto hiyo sasa tumeamua kuandaa maonesho yatakayoweza kuwakutanisha taasisi za kifedha pamoja na wakulima ambapo hapo taasisi hizo zitaweza kutambua mahitaji ya wakulima, na jinsi ya kuweza kuwasaidia tofauti na hapo awali," alisema Jacqueline.
Pia alisema kuwa maonesho hayo yataenda sambasamba na uwasilishwaji wa mada mbalimbali ikiwemo uaandaji bora wa mipango biashara, umuhimu wa soko la hisa katika kuhakikisha upatikanaji wa mitaji wa muda mrefu na matumizi bora ya mikopo katika biashara hususani za kilimo  ili walengwa waweze kujifunza zaidi juu ya mbinu bora za kufikia na kupata mitaji kwa kufanya biashara.
Kwa upande wake mratibu wa mtandao wa Agri-Hub Tanzania Tom Ole Sikar alisema kuwa maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wakulima pamoja na wamiliki wa biashara za kilimo kama vile wachuuzi,wauzaji wa pembejeo na wasindikaji kutambua fursa mbalimbali za mitaji pamoja na usalama wa kifedha zilizopo kwa biashara za kilimo.
Hata hivyo alisema kuwa wadau ambao wengi wao ni wakulima wataweza kupata fursa ya kutambua njia bora za kuboresha biashara na utoaji wa huduma kwa walengwa pamoja na kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara wengine wa kilimo waliofanikiwa kutembelea maonesho yaliyopita.

No comments:

Post a Comment