Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 28 April 2014

HUKUMU YA MUSLIM BROTHERHOOD KUTOLEWA


Hukumu dhidi ya Muslim Brotherhood kutolewa.

Mahakama moja katika mji wa Minya leo inatarajiwa kutoa uamuzi wake wa mwisho kuhusu hukumu ya kifo iliyotolewa mwezi uliopita kwa wafuasi 529 wa vuguvugu la Muslim Brotherhood ambalo sasa limepigwa marufuku nchini humo.

 Kesi hiyo ilizua shutuma kali kutoka jamii ya kimataifa.
Watu hao walipatikana na hatia ya kumuua afisa mmoja wa polisi katika rabsha zilizozuka mwezi Agosti mwaka uliopita.
Watu hao walihukumiwa kifo kwa mara ya kwanza mwezi Machi baada ya kesi kufanyika kwa takriban saa moja.
Mawakili wa utetezi walinyimwa fursa ya kujieleza na hata mashtaka hayakutangazwa.
Baadaye kesi hiyo iliwasilishwa mbele ya mmoja ya viongozi wakuu wa kidini ili kuamuliwa tena lakini maoni yake hayakuzingatiwa.
Miongoni mwa waliohukumiwa kunyongwa ni vijana wawili wenye umri wa miaka 17, mtu mmoja mlemavu na wakili aliyewakilisha baadhi ya
washukiwa hadi alipokamatwa.
Mawakili wa washtakiwa wamesema watakata rufaa iwapo mahakama itapitisha hukumu zilizotolewa.
Baadhi ya wataalam wa maswala ya sheria wametabiri kuwa huenda kesi dhidi ya waku hao ikasikizwa tena.
Mahakama pia inatarajiwa kutoa uamuzi katika kesi ya pili dhidi ya watu 700 wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood
baadhi wakikabiliwa na mashtaka ya kuhusika katika machafuko.


CHANZO, BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment