Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 29 April 2014

AFISAA MKUU WA UN AZURU SUDAN KUSINI

Vurugu zinashuhudiwa nchini Sudan pande za kisiasa zikizozana kuhusu mamlaka

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu , Navi Pillay yuko nchini Sudan kusini kutathmin hali huko baada ya miezi minne ya mzozo .
Ziara yake inakuja siku kadhaa tu baada ya watu wenye silaha kushambulia kambi ya Umoja wa Mataifa iliyoko Bor, na kuwauwa takriban watu 58 wakiwemo wahudumu na watoto .

Bi Pillay atakutana pia na watu walioyahama makazi yao kutokana na vita. Juma lililopita mamia ya raia waliuawa Bentiu-- mji mkuu wa jimbo lenye utajiri wa Mafuta.

Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Kusini , Barnaba Mariel Benjamin ameiambia BBC kuwa serikali yake inataraji Umoja wa Mataifa utalaani mauaji ya raia wanayolaumiwa kuyafanya waasi.

Wakati huo huo wawakilishi wa pande husika na mzozo huo wamerejea mjini Addis Ababa Ethiopia kufufua mazungumzo ya amani.

CHANZO BBCSWAHILI


No comments:

Post a Comment