Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 30 April 2014

SUDAN K.KUJUA HATIMA YAKE KATIKA EAC LEO


Mkutano wa jumuiya ya Afrika Mashariki waanza leo Tanzania

Mkutano wa kumi na mbili wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaaanza rasmi hii leo mjini Arusha nchini Tanzania.

Miongoni mwa maswala muhimu yatakayojadiliwa ombi la Sudan Kusini kutaka kujiunga na jumuiya hiyo.

Mkutano wa mwisho kama huu uliofanyika mjini Kampala Uganda mwezi Novemba mwaka jana, uliweka bayana kwamba ni katika mkutano huuu wa Arusha, ambapo tarehe ya Sudan Kusini kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki itakapotangazwa.

Lakini wadadisi wanasema kuwa msukosuko wa kiuchumi pamoja na vita vya wenyewe kwa wenyewe huenda ikawa sababu ya taifa hilo kunyimwa uanachama wa jumuiya hiyo. Hii ni baada ya machafuko ya wenyewe kwa wenyewe kuzuka, na kusambaratisha nchi hiyo kisiasa na kiuchumi.

Maswala mengine yatakayojadiliwa ni ripoti ya mawaziri, mikakati ya kifedha katika kuiendesha jumuiya hiyo na mbinu za nchi wanachama kuendelea kupeana taarifa za kijasusi, katika juhudi za kupambana na tishio la ugaidi.

CHANZO, BBCSWAHILI. 

No comments:

Post a Comment