Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 28 April 2014

UEFA-NUSU FAINALI: TIMU GANI KUTINGA FAINALI?





BAYERN AU REAL??? CHELSEA AU ATLETICO??
TAKWIMU ZA NUSU FAINALI KWA MUJIBU WA UEFA:
NUSU FAINALI:
Marudiano

[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza] Jumanne Aprili 29

Bayern Munich v Real Madrid [0-1]
Jumatano Aprili 30
Chelsea v Atletico Madrid [0-0]

FC Bayern Munich v Real Madrid CF
-Allianz Arena, Munich, Germany
-Rekodi ya Bayern Munich wakiwa Nyumbani kwao dhidi ya Real Madrid ni Ushindi: 8, Sare: 1 Kufungwa: 0.
-Real Madrid wameshinda mara 2 tu katika safari zao 27 Nchini Germany, mojawapo ikiwa ni ushindi wa Bao 6-1 dhidi ya FC Schalke katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Msimu huu.
-Bayern wamefanikiwa kupindua vipigo vya Mechi za Kwanza za Ulaya za Ugenini mara 9 kwa kushinda kwao, lakini wamefungwa mara 10 zikiwemo mara 7 katika Mechi zao 9 walizocheza mwisho na kuanza kufungwa Ugenini
-Katika Mechi 6 ambazo walifungwa Bao 1-0 Ugenini, Bayern wameweza kushinda Mechi 5 na ya mwisho ilikuwa Msimu wa 2011/12 walipofungwa na FC Basel kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na kuweza kuwatwanga 7-0 katika Marudiano Mjini Munich.
-Real Madrid wameweza kufuzu mara 43 kati ya 56 ambazo walitangulia kushinda Nyumbani kwao.
-Waliposhinda 1-0 Uwanjani Santiago Bernabéu, Real wameweza kushinda mara 4 kati ya 6 na mara hizo mbili walizotolewa kwenye Marudiano ilikuwa dhidi ya Juventus, Misimu ya 2004/05 na 1995/96, na mara zote walichapwa 2-0 kwenye Marudiano.

Chelsea FC v Club Atlético de Madrid
-Stamford Bridge, London, England

-Katika Mashindano ya UEFA, Chelsea wamefungwa mara 2 tu kati ya 7 ambazo walitoka Sare Ugenini.

-Wakitoka Sare 0-0 Ugenini, Chelsea wameshinda mara 1 tu na kufungwa mara 2 na hivi karibuni ni pale walipotolewa na Barcelona kwenye Nusu Fainali ya 2008/09 walipotoka 0-0 huko Nou Camp na kufungana 1-1 Stamford Bridge.

-Chelsea wameshinda mara 1 tu kati ya 4 walizokutana Nusu Fainali na Klabu toka Spain na hiyo moja ilikuwa dhidi ya Barcelona Msimu wa 2011/12. Mwaka 2009 walitolewa na Barcelona, 1998/99 walitolewa na RCD Mallorca kwenye Kombe la Washindi la UEFA na 1994/95, walibwagwa na Real Zaragoza.

-Atletico, ambao wamefuzu mara zote mbili baada kutoka Sare 0-0 Nyumbani, wameshinda mara 1 tu Ugenini dhidi ya Klabu za England kati ya Mechi 9. Mara hiyo 1 ni pale walipoifunga Leicester City FC Msimu wa 1997/98 kwenye Raundi ya Kwanza ya UEFA Cup.

-FAINALI: Estádio da Luz, Lisbon, Portugal 24 Mei 2014
Bayern Munich/Real Madrid v Chelsea/Atletico Madrid

CHANZO, MPENJABLOG

No comments:

Post a Comment