Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 27 April 2014

WATAKIWA KUTOA KWA MOYO

Na Zainab Maeda, Iringa

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Pindi Chana amewaagiza  viongozi na watendaji wa Serikali za Mitaa kukusanya takwimu kamili za watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi.
 Pindi alitoa agizo hilo juzi katika siku ya sikukuu ya pasaka wakati aliposhiriki katika hafla fupi ya chakula cha mchana na watoto yatima na wanaishi katika mazingira magumu katika Kanda ya Mlandege Manispaa ya Iringa, iliyoandaliwa na Diwani wa Viti Maalum wa Kanda hiyo Dora Nziku.
“Tupewe takwimu za watoto wanaoishi katika mazingira magumu na yatima pamoja na watoto wa mitaani, takwimu hizi zitatusaidia kufahamu watu hao kwa haraka zaidi na namna ya kuwashughulikia,” alisema Pindi na kuongeza:
“Watendaji wa Serikali za Mitaa  ni wajibu wenu wa kuwatambua watoto wetu walio yatima au wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa maisha yao pamoja na watoto wa mitaali ili wasaidiwe.”
Alisema kuwa watoto wamekuwa wakinyanyasika sana na mila na desturi zilizopo katika baadhi ya familia za Watanzania.
Mbali na kusema hayo aliwataka wazazi na walezi kuwajali watotot kwa kuwapa lishe bora ili wawe na afya bora.
 Naye mwandaaji wa hafla hiyo Diwani Dora aliwataka Watanzania kuwa na mioyo ya huruma kwa watotot kama hawa kwa kutoa chochote walichonacho kwa kuwa kutoa ni moyo na sio utajiri.

“Ndugu zangu watoto hawa ni wakwetu tunapaswa kujua nakufahamu wanavyoishi kwa Yule mwenye moyo wa kutoa tuwe tunawakumbuka watoto hawa ili wajiskia kuwa wapo sawa na wengine, nataka kuwaambia kuwa kutoa ni moyo na sio utajiri,” alisema Dora.

No comments:

Post a Comment