Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 9 April 2014

WILAYA NNE ARUSHA ZAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UZAZI, LISHE


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

IMEELEZWA kuwa mkoa wa Arusha bado unakabiliwa na changamoto ya huduma za uzazi pamoja na lishe bora hali ambayo inasababisha malengo ya Milenia kukwama huku idadi ya vifo vya mama na watoto ikiendelea kuongezeka.
Aidha kwa wilaya nne kati ya saba bado zinaendelea kuzalisha watoto majumbani huku Wilaya nne nazo tena zikiendelea kukabiliwa na changamoto ya lishe duni kwenye jamii.
Hayo yameelezwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Dk Frida Mokiti wakati akiongea na wadau pamoja na wataalamu wa sekta ya afya wa mkoa wa Arusha ambao walikutanishwa na shirika la EGPAF mapema wiki hiii huku lengo likiwa  ni kuweza kujadili agenda za afya kwa mkoa wa Arusha.Dkt Mokiti alisema kuwa kwa sasa wilaya ambazo zina jamii ya wafugaji zinakabiliwa na changamoto ya uzazi hafifu pamoja na lishe duni  hali ambayo inasababisha malengo yaliweza kuweka na mkoa kufifia.Aliendelea kwa kusema kuwa wilaya ambazo zinatoa huduma ya uzazi chini ya asilimia 50 kuwa ni pamoja na wilaya za Monduli, Longido, pamoja na Ngorongoro hali ambayo inaendelea kusababisha vifo vya  mama na mtoto kutokea kila mara.Mbali na hayo alidai kuwa wilaya za Meru, Jiji la Arusha,Karatu, ndizo ambazo zimeweza kurahisisha huduma za uzazi kwa mama wajawazito na watoto ambapo wao wanatoa huduma kwa kiwango cha asilimia 70  huku lengo likiwa ni asilimia 80."Hapa tunaweza kuona kuwa hizi asilimia za wilaya nne kwa kweli ni mbaya sana na zinahitaji msaada mkubwa sana kwani hii inasababisha vifo vya watoto na mama zao kuzidi kuongezeka lakini kwa sasa tunampango wa kuweka mikakati itakayoweza kusaidia afya za wananchi wetu kuimarika kwani pia kutokana na hili linasababisha  wengi kuzalia majumbani"aliongeza Dkt MokitiKutokana na hilo pia alisema kuwa utoaji wa huduma za uzazi kwa wanawake na watoto pia bado zinakabilia na changamoto ya lishe duni hali ambayo ni chanzo kikubwa sana cha vifo hasa vya watoto wadogo Dkt Mokiti alisema kuwa Mpaka sasa wilaya ambazo zinakabiliwa na changamoto hiyo ya lishe Duni kuwa ni pamoja na Wilaya za Monduli, Longido, Ngorongoro,pamoja na Wilaya ya Karatu.Katika hatua nyingine naye Meneja wa shirika la EGPAF kutoka katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro Ponsiano Riziki alisema kuwa ili kuatatua changamoto zote hizo kunahitajika umoja baina ya watendaji wa serikali na asasi binafsi.Ponsiano alisema kuwa kwa sasa Shirika hilo limeeka mikakati ya kuwakutanisha kwa pamoja wadau wote ili kuwa na kauli moja ambayo itaweza kutoa majawabu ya afya za jamii kwenye mkoa wa Arusha.

No comments:

Post a Comment