Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 2 April 2014

WATANZANIA WALIOLIPULIWA NA OSAMA KUZOA SHS. 672 BILIONI

Osama bin Laden

Nairobi/Dar. Watanzania wanne waliojeruhiwa katika mlipuko wa bomu katika ubalozi wa Marekani mwaka 1998 na wengine watano waliofariki dunia katika mlipuko huo watalipwa fidia ya Sh672 bilioni, kiwango ambacho ni sawa na bajeti ya wizara nne za Tanzania.
Watanzania hao waliuawa na wengine kujeruhiwa katika moja ya mashambulizi pacha yaliyotokea kwa wakati mmoja jijini Dar es salaam na Nairobi, Kenya na ambayo yaliratibiwa na Osama Bin Laden akitumia mtandao wa kundi la Al Qaeda mwaka 1998 kwenye ofisi za balozi za Marekani.
Katika mashambulizi hayo yaliyotokea saa 4:00 asubuhi Agosti 7, 1998, Wakenya 200, Watanzania 10 na Wamarekani 12 walipoteza maisha na pia magaidi wawili nao walikufa.
Kati ya Watanzania 10, ni kesi za watu wanne tu waliouawa tu zilizofunguliwa kudai fidia ya watu hao kupoteza maisha.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Marekani, Thomas Bates alitoa hukumu hiyo wiki iliyopita, akiagiza pia kwamba serikali za Iran na Sudan lazima zilipe jumla ya Dola za Marekani 957 milioni (Sh1.53 trilioni) kwa Watanzania hao na Wamarekani 23 waliouawa au kujeruhiwa katika mashambulizi pacha ya kigaidi.
Jaji Bates alisema kiasi cha Dola 488 milioni za Marekani (Sh780.8 bilioni) kitalipwa kwa Wamarekani 12 waliouawa na familia zao. Dola 420 milioni za Marekani (Sh672 bilioni) zitalipwa kwa Watanzania wanne waliojeruhiwa katika mlipuko na Watanzania watano waliuawa katika shambulio hilo. Dola milioni 49 (Sh78.4 milioni) zitalipwa kwa raia wawili wa Marekani waliojeruhiwa katika milipuko hiyo.
“Milipuko ya mabomu katika balozi hizo mwaka 1998 iliwaathiri wanaoshtaki katika kesi hii, “Jaji Bates aliandika. Kupitia simulizi zao binafsi, inaonyesha kwamba hata zaidi ya miaka 15 baadaye kila mmoja bado ana kumbukumbu za kutisha za siku hiyo.
“Fidia hii haiwezi ikarudisha maisha ya wale waliokufa wala waliopata madhara. Badala yake, ni ya kutoa tu kifuta machozi. Lakini hiyo ni kidogo sana kwa wale wanaoshtaki.”
Hata hivyo, uamuzi wa Jaji Thomas Bates haujaeleza fedha hizo zitalipwa lini kwa waathirika hao.
Kiwango cha Sh672 bilioni ni sawa na bajeti za Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambayo katika mwaka wa fedha wa 2013/14 ilitengewa Sh20.4 bilioni, Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (Sh21.3 bilioni), Uchukuzi (Sh491.1 bilioni ) na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyotengewa Sh138.3 bilioni.
Thomas Fay, wakili aliyewawakilisha Watanzania na Wamarekani, alisema kuwa juhudi zinazotakiwa sasa ni kuanza kutambua mali za Iran na Sudan ambazo zinaweza kutaifishwa ili kulipa fidia hiyo.
Mwanasheria Mkuu wa Washington alisema kuwa hukumu ya Jaji Bates ni hatua muhimu katika kuhakikisha kuwa Wamarekani na Watanzania walioathirika kwa ugaidi huo wanapata haki kwa mateso waliyoyapata.

No comments:

Post a Comment