Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 1 April 2014

MALIASILI YALIPWA TSHS. 25 MILIONI, YAKAMATA MAJANGILI 544 NA MENO YA TEMBO

 

Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

WIZARA ya Mali asili na utalii imefanikiwa kukamata majangili 544 wanaojihusuisha na ujangili kwenye hifadhi mbalimbali hapa nchini pamoja na mizoga ya tembo 39,meno ya tembo mazima,katika oparesheni maalumu ambayo imeftanyika kati ya Januari na Machi mwaka huu.
Hataivyo kukamatwa kwa vitu hivyo kunatokan na doria ambazo zinafanywa na baadhi ya askari wa wanyama pori ambazo zilikuwa zinaendelea kufanyika katika mapori na hifadhi mbalimbali.
Akiongea na vyombo vya habari mapema leo Mkurugenzi wa wanyama pori Taifa Paul Sarakikya alisema kuwa hiyo imetokana na oparesheni ambayo inaendelea kufanywa na wizara hiyo huku lengo lake likiwa ni kupunguza kasi ya ujangili.
Aidha alisema kuwa katika kipindi cha mwezi January hadi kufikia Machi Mwaka huu jumla ya doria zilizosababsisha kukamtwa kwa vitu hivyo ni doria Mandays 30,372 ambapo zilikuwa ni kwa ajili ya kukabiliana na ujangili  ndani na hata nje ya hifadhi za taifa,mapori ya akiba nchini
Aliendelea kwa kusema kuwa katika kipindi husika jumla ya mizoga ya tembo 39 ilionekana ndani na nje ya hifadhi za taifa na mapori ya akibanchini huku meno mazima yakiwa ni 171 na vipande 22 vya meno ya tembo ghafi , vipande 302 vya meno ya tembo yaliyochakatwa yenye jumla ya kilo 662.62
Mbali na hilo pia alisema kuwa katika doria hizo waliweza kukamata vitu vingine ambavyo ni kama vile nyama pori za wanyama mbalimbali ambazo zilikuwa zinatolewa na majangili hayo kwa ajili ya viteo jambo ambalo ni kinyume kabisa na sheria ya nchi inavyosema na kufafanua zaidi
"tumefanikiwa kukamata hivi vitu kutokana na jitiada ambazo tumeziweka hapa kwetu na hata nje lakini bado tuna mikakati mingine mingi zaidi ya kuweza kuwateka majangili ambao wanasababisha madhara makubwa kwa taifa letu la tanzania"aliongeza Sarakikya
Katika hatua nyingine alifafanua kwa kudai kuwa waliweza kukamata hata vifaa mbalimbali ambavyo vilikuwa vinatumika na majangili hayo kwa ajili ya shuguli zao ndani ya mapori lakini hata hifadhi mbalimbali hapa nchini.
aliweza kutaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na Bunduki ya rashasha  moja, Rifle 3, shotgun 2, gobori 5 na jumla ya risasi 7 za aina mbalimbali  pamoja na malighafi kama vile  magari 5  ngombe 2663 misumeno 1 na mbao 745
kutokana na hilo pia watuhumiwa waliweza kulipa faini ya zaidi ya milioni 25 na pia hali hiyo iliweza kusababisha hata ujangili kushuka kwa kiwango cha asilimia 58 tofauti na mwaka jana ambapo ujangili ulikuwa ni mkubwa sana.

No comments:

Post a Comment