Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 9 April 2014

JIHADHARINI NA MTANDAO WA TCRA FOUNDATION

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAHADHARI NA MTANDAO WA UTAPELI UNAOJIITA TCRA FOUNDATION


Mamlaka ya Mawasiliano imebaini kuwa kuna mtandao wa matapeli wanaotumia jina la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kutumia tovuti inayojiita “TCRA Foundation” na inayodanganya kutoa mikopo kwa maendeleo kwa watu.

Mtandao huu umetengenezwa wa kutumia picha zilizopo kwenye mitandao mbalimbali zikiwaonyesha Raisi Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Makawe Mbarawa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Prof. John Nkoma.

Aidha mtandao huu unadai kuwa Mamlaka kwa kushirikiana na Kampuni za Simu za Vodacom na Tigo pamoja na Benki ya CRDB na NMB zinashirikiana kuendesha Foundation hiyo.

Mamlaka ya Mawasiliano inawatahadharisha wananchi kuwa haina “Foundation” yoyote ya kutoa misaada ya fedha. Mtandao huu unatumika kuwalaghai wananchi na kuwaibia fedha zao kwa kuwataka watume fedha za kujiunga na mtandaqo huo kwa number za simu za Tigo na Vodacom zinazoonesha kusajiliwa kwa jina la Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania. Sio kweli na ni wizi na udanganyifu.

Mamlaka ya Mawasiliano inawataka wananchi kuwa na tahadhari na watu hawa ambao hutumia mitandao ya Mawasiliano ya simu na intaneti kufanya utapeli. Usitume fedha wala kujiunga na mitandao ya namna hii.

Aidha Mamlaka ya Mawasiliano inawaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa wanapobaini utapeli wa namna hii kwa kutoa taarifa kwa Mamlaka kwa vyombo vingine vya usalama ikiwa watahisi au kuwa na taarifa za watu wanaojihusisha na udanganyifu huu katika mitandao ya Mawasiliano ili kuzuia vitendo hivi vilivyoshamiri katika siku za hivi karibuni.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
8Aprili 2014


No comments:

Post a Comment