Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 29 October 2013

WANAHABARI IRINGA WALITAKA RAI LIWATAJE WAANDISHI WALIOHONGWA NA CCM

 Mwenyekiti  wa chama  cha  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa Frank Leonard kulia akitoa msimamo  wa  wanahabari dhidi ya  gazeti la Rai na mbunge Msigwa  leo ,kushoto ni katibu mtendaji wa IPC Francis Godwin.


 Wanahabari Clement Sanga kushoto akiwa na mwakilishi  wa New habari {2006} Ltd  wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania , Rai  na Bingwa mkoa  wa Iringa Mercy Mwalusamba wakati  wa kikao  cha  cha wanahabari  mkoa  wa Iringa  leo  kujadili habari  zilizoandikwa na gazeti la rai jumapili .


 Wanahabari  wakifuatilia kwa makini kikao  hicho


Na  Francis Godwin Blog

WANAHABARI  mkoani Iringa wamekanusha habari zilizoandikwa na gazeti la Rai  toleo Namba 1067 la Jumapili, Oktoba 27, 2013 kuwa wanahabari hao wamehongwa viongozi wa CCM mkoani humo ili wasiandike habari ya msaidizi wa Mbunge wa Isimani, Wiliam Lukuvi, Bw. Thom Malenga kukamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na ujangili.
Katika kikao chao kilichofanyika leo katika ofisi za Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa (IPC) mbali ya kukanusha habari hizo kuwa zimeandikwa kwa lengo la kuchafua tasnia ya habari mkoani humo, wamelitaka gazeti la Rai na Mbunge wa  Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwataja waandishi waliohongwa kabla ya wanahabari hao hawajachukua hatua zaidi.
"Gazeti la Rai Jumapili halijatutendea haki, limetuvunjia heshima kwa wadau wa habari mkoani Iringa na nje ya mkoa... tunachotaka Rai kuwataja waandishi waliohongwa ili tuchukuliane hatua... wasipofanya hivyo ndani ya siku 14 kuanzia leo Jumanne tutawafikisha Baraza la Habari Tanzania (MCT)," walisema katika tamko lao lililotolea na Mwenyekiti wa IPC, Frank Leonard.
Walisema gazeti la Rai limewachafua vibaya kutokana na jinsi lilivyoandika habari hiyo huku likishindwa kuwapa hata fursa ya kuwahoji ili kuweka uzani sawa.
Leonard alisema siyo kweli kwamba wanahabari Iringa walishindwa kuandika habari ya kukamatwa kwa Malenga bali kwa kuwa wao ni makini na hawakutaka kukurupuka hivyo walitaka kabla ya kuandika kuweza kumpata msemaji wa kikosi  hicho cha kupambana na ujangili ili kulizungumzia hilo kabla ya kuandika jambo ambalo wao kama wanahabari walikuwa wakilisikia mitaani bila kuwa na uhakika.
Uandishi wa habari mzuri ni pamoja na kuzingatia maadili ya uandishi na sio kuandika bila ya kuwa na uhakika wa kile unachokiandika.
Hata hivyo alisema kwa kuwa mbunge Msigwa amenukuliwa katika gazeti hilo kama  ndio msemaji wa jambo hilo wao kama wanahabari watamwandikia barua mbunge  huyo ili kusaidia kuwataja wanahabari waliohongwa pesa vinginevyo wao kama  wanahabari wa mkoa wa Iringa hawatamvumilia Mbunge Msigwa katika hilo.
Pia alisema kuwa suala hilo kwa sasa ameachiwa mwanasheria wa IPC ili kulifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuwaandikia barua Rai na Mbunge Msigwa kuwataka  kuthibitisha ukweli wa kilichoandikwa dhidi ya wanahabari Mkoa wa Iringa.
CHANZO: francis godwin blog
(Imehaririwa na Admin wa blog hii)

No comments:

Post a Comment