Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 22 October 2013

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MGODI WA CHUMA WA LIGANGA


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Meneja mradi wa Maganga Matatitu Resource Development limited Bw. Lawrence Manyama  kuhusu mlima huo uliosheheni mashapu ya chuma alipotembelea eneo lenye utajiri wa chuma la  Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wawekezaji wa kampuni ya Sichuan Hongda ya China ambao ni wawekezaji katika eneo lenye utajiri wa chuma la  Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013. Kampuni hiyo inatarajiwa kujenga kiwanda cha kufua chuma mapema mwakani kitachajiri watu 32,000 kitakapokamilika.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akionesha kilele cha Central Liganga hill ambacho ni mojawapo ya sehemu ambazo kampuni ya Sichuan Hongda ya China itachimba mashapu ya chuma na kuyafua katika  kiwanda kikubwa cha kufua chuma kitachoajiri watu 32, 000 katika eneo hilo lenye utajiri wa chuma la  Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi alipoowasili katika uwanja wa mikutano wa Ludewa ambako alihutubia mkutano wa hadhara. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment