Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 31 October 2013

WAZIRI NAHODHA AONGOZA MAZISHI YA LUTENI MILIMA

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha akitia saini kitabu cha mahudhurio, alipohudhuria kuuaga mwili wa marehemu Luteni Rajabu Mlima kwenye kambi ya Jeshi la Ulinzia la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ya Lugalo jijini Dar es Salaam.
Waziri Nahodha akisalimiana na maafisa na viongozi wa JWTZ
Waombolezaji waliohudhuria kuuaga mwili wa marehemu.

Askari wakiuteremsha mwili wa marehemu baada ya kuwasili.
Askari wameubeba mwili wa marehemu.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akitoa heshima za mwisho.
Mchumba wa marehemu akimliwaza mwanae ambaye pia ni motto wa marehemu wakati wa kuuaga mwili kwenye viwanja vya Lugalo. Picha zote na Hussein Makame, Ofisa Habari Idara ya Habari (MAELEZO).

 
Na Hussein Makame, MAELEZO

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha ameongoza mamia ya waombelezaji kuuaga mwili wa Afisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) marehemu Luteni Rajabu Mlima aliyefariki Oktoba 27 mwaka huu wakati akitekeleza jukumu la kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Akizungumza na wanahabari katika viwanja vya Kambi ya Lugalo ya JWTZ jijini Dar es Salaam baada ya kuuuaga mwili wa shujaa huyo, Waziri Nahodha aliseka kuwa Tanzania haitaacha kutekeleza majukumu yake ya kulinda amani nchini DRC hadi hapo iatakapohakikisha kwamba nchi hiyo imekuwa na amani.
Hata hivyo, alisema kuwa kufuatia kumpoteza shujaa huyo Serikali kupitia Wizara yake itaendelea kuwa bega kwa bega na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi kutokana na kumpoteza mpendwa wao.
Akitoa salamu za rambirambi kutokana na msiba huo, Mnadhimu wa Jeshi hilo Luteni Genarali Samuel Ndomba alisema kuwa marehemu Luteni Mlima alifariki baada ya kupigwa risasi wakati akilinda raia wa DRC wasidhuriwe na mapigano kati ya Jeshi la nchi hiyo na waasi wa M23.
Luteni Generali Ndomba alisema shujaa huyo alifariki saa 5:08 asubuhi jumapili iliyopita wakati kikundi chao kilipokuwa kikiwalinda raia wa DRC kwenye mji wa Kiwanja karibu na miliya ya Gavana iliyoko nchini humo.
Aliongeza kuwa marehemu Luteni Mlima alikuwa mmoja wa Maafisa katika kikundi cha JWTZ nchini DRC ambacho kinashiriki katika operersheni ya kulinda amani kikiwa ni sehemu ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa (MONUSCO).
“Marehemu wakati wa uhai wake na hasa katika operesheni hii inayoendelea nchini humo alifanya kazi zake kwa ujasiri na uhodari wa hali ya juu ambao kwa kiasi kikukbwa umechangia kuleta heshima na sifa ambazo jeshi na nchi yetu imepata katika nyanja za ulinzi wa amani Afrika.Tutaendelea kumkumbuka kwa mchango wake kwa Jeshi na Taifa letu” alisema Mnadhimu Mkuu huyo wa JWTZ.
Aliongeza kuwa “Kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi, Maafisa na watumishi wa umma natoa salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiriki wa karibu kwa masiba huu, tunaungana na familia katika kipindi hiki cha maombolezo na wakati huo tukiendelea kumuomba Mwenyezi Mungu awape faraja na ustahamilivu katika ki[phiki kigumu na majonzi.Mwenyezi mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu Luteni Rajabu Ahmed Mlima, Amen”
Naye kaka wa marehemu Dk. Azizi Mlima alisema kuwa kwa niaba ya familia wanashukuru sana JWTZ na Serikali kwa ujumla kwa kumpokea ndugu yao na kwa shughuli nzima za mazishi yake hasa ikizingatiwa kwamba amefariki wakati akitekeleza majukumu ya Kitaifa na Kimataifa ya kuleta amani katika ukanda wa Maziwa Makuu.
Akizungumza kwa majonzi mchumba wa marehemu Luteni Asia Hussein alisema amepokea kwa masikitiko msiba huo kwani walikuwa wanatarajia kufunga ndoa mwishoni wma mwaka huu.
Pamoja na viongozi hao wa Serikali, pia Makatibu Wakuu wa Wuzara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na wizara nyingine, Mabalozi na Maafisa wastaafu wa Jeshi hilo walihudhuria kuuaga mwili wa marehemu kwenyekambi ya Lugalo.
Marehemu baada ya kuagwa katika viwanja hivyo alipelekwa nyumbani kwa familia yake Mbezi Beach jijini Dar es Salaam ambapo familia ilimuaga kabla ya kuzikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam huku akiwa ameacha mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 10 Zuhrat.

No comments:

Post a Comment