Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 3 June 2014

TAREHE KAMA YA LEO: MLIPUKO WA GESI ASILIA WAUA 500 RUSSIA

Jun 3, 1989:

Katika ajali mbaya ya kutisha, bomba la gesi asilia linalipuka tarehe kama ya leo mwaka 1989 katika eneo la Milima ya Ural huko Russia wakati treni mbili zikiwa zinapita hapo.
Mlipuko huko mkubwa ulitokea karibu na mji wa Ufa katika iliyokuwa Muungano wa Jamhuri za Kisovieti (USSR) ambao ulitokana na maamuzi mabovu ya wafanyakazi wa bomba hilo.
Wafanyakazi hao walikuwa wanatambua kwamba presha kwenye bomba ilikuwa imeshuka siku hiyo ya Juni 3 – dalili kwamba kulikuwa na tundu mahali. Hata hivyo, badala ya kufuata taratibu za msingi na kutazama matundu, wao wakaongeza presha na kufungulia gesi kwa wingi ili kuiongeza presha iwe juu. Gesi hiyo ikaendelea kutoka (kuvuja) na kusambaa kwenye eneo la jirani, nyingi ikituama kwenye eneo la chini jirani na njia treni takriban maili moja kutoka kwenye bomba.
Wakati haya yakitokea, treni mbili zilikuwa zinakaribia kwenye Reli ya Trans-Siberia, zikipishana karibu na ilipo gesi hiyo asilia.
Ghafla gesi ikapata moto na kusababisha mlipuko mkubwa uliosambaa kwenye eneo la urefu wa maili moja. Nguvu ya mlipuko huo ikayadondosha mabehewa kadhaa ya treni yaliyoanguka nje ya reli. Mamia ya miti katika msitu wa jirani yakateketea kutokana na joto kali.
Mlipuko huo na kuanguka kwa mabehewa ya treni vikasababisha maafa makubwa kwenye treni. Zaidi ya watu 500 wakapoteza maisha yao (idadi halisi haikuweza kupatikana) na wengine wengi wakaungua na kupata majeraha makubwa. Helikopta zikapelekwa kuwabeba majeruhi na kuwakimbiza haraka hospitali.


Jun 3, 1800:

RAIS ADAMS AINGIA KATIKA MAKAO MAKUU MAPYA


John Adams, rais wa pili wa Marekani, anakuwa rais wa kwanza kuishi Washington, D.C., wakati alipoanza kuishi Union Tavern huko Georgetown tarehe kama ya leo mwaka 1800.
Jiji la Washington liliandaliwa kuchukuwa nafasi ya Philadelphia kama makao makuu ya nchi katikati ya jamhuri hiyo mpya. Majimbo ya Maryland na Virginia yalirundika udongo pembezoni mwa Mto Potomac kuanzisha Wilaya ya Columbia, na kazi ilianza huko Washington mwaka 1791. Mtaalamu wa majengo wa Kifaransa Charles L'Enfant alichora ramani ya jiji hilo, likiwa na makumi ya miduara, mitaa inayokatiza, pamoja na bustani nyingi. Mwaka 1792, kazi ilianza katika majengo ya White House katika mtaa wa 1600 Pennsylvania Avenue chini ya usimamizi wa mtaalamu wa majengo Mmarekani mwenye asili ya Ireland James Hoban, ambaye ubinifu wake wa Ikulu ya White House ulitokana na muundo wa Leinster House ya jijini Dublin na mchoro wa jengo kama ulivyoelezwa katika kitabu cha ramani cha James Gibbs (Book of Architecture). Katika mwaka uliofuata, Benjamin Latrobe akaanza ujenzi katika majengo mengine muhimu ya serrikali, likiwemo la U.S. Capitol.
Juni 3, 1800, Rais Adams akahamia kwenye makazi ya muda kwenye makao makuu mapya wakati ujenzi ulipomalizika kwenye hekalu la rais. Mnamo Novemba 1, rais alikaribishwa ndani ya White House. Siku iliyofuata, Adams akamwandikia mkewe kuhusu nyumba yao mpya: "Naomba mbingu zilete Baraka nzuri kwenye nyumba hii, na kwa wale wote watakaokuja kuishi baadaye. Watu wenye busara tu ndio wanaopaswa kutawala chini ya dari ya nyumba hii!" Baadaye, Abigail Adams aliwasiki kwenye White House, na Novemba 17 Bunge la Congress la Marekani lilikutana kwa mara ya kwanza kwenye Makao Makuu ya Marekani.
Wakati wa Vita vya mwaka 1812, majengo yote yaliteketezwa na wanajeshi wa Uingereza mwaka 1814 katika kulipiza kisasi cha kuunguzwa kwa majengo ya serikali nchini Canada na majeshi ya Marekani. Ingawa mvua kubwa ililiokoa Jengo la Capitol ambalo lilikuwa halijakamilika, lakini White House iliteketea yote.
Hekalu hiyo lilijengwa upya na kutanuliwa kwa maelekezo ya James Hoban.


Jun 3, 1989:

MASHAMBILIAI YA TIANANMEN YAANZA CHINA





Huku machafuko ya kudai mabadiliko ya kidemokrasia yakiingia wiki ya 17, tarehe kama ya leo mwaka 1989 serikali ya China inaruhusu askari wake na mizinga kushambulia eneo la Tiananmen Square jijini Beijing kwa gharama zozote. Hadi kufikia usiku wa manane Juni 4, majeshi ya China yalikuwa yamesafisha eneo hilo, yakiua mamia ya waandamanaji na maelfu kukamatwa.
Mnamo Aprili 15, kifo cha Hu Yaobang, kiongozi wa zamani wa chama cha Communist (CP) ambaye alikuwa anaunga mkono mabadiliko ya kidemokrasia, kiliwaamsha wanafunzi 100,000 walioamua kukusanyika hapo Tiananmen Square kumkumbuka kiongozi huyo na kueleza malalamiko yao kwa serikali.
Aprili 22, kumbukumbu rasmi ya Hu Yaobang ilifanyika kwenye Ukumbi wa Great Hall of the People, na wawakilishi wa wanafunzi walibeba ujumbe hadi kwenye ngazi za ukumbi huo, wakitaka kukutana na Waziri Mkuu Li Peng. Serikali ya China iligoma kukutana nao, na kusababisha mgomo wa masomo katika vyuo vyote vya China na kuitisha maandamano ya nchi nzima.
Wakipuuza onyo la serikali la kutawanyika na kutoandamana, wanafunzi kutoka zaidi ya vyuo vikuu 40 wakaanza kuandamana hapo Tiananmen Aprili 27. Wanafunzi hao waliungwa mkono na wafanyakazi, wanataaluma, na watumishi wa umma, na hadi kufikia mwezi Mei zaidi ya watu milioni moja walikuwa wamejaa kwenye eneo hilo, eneo ambalo Mao Zedong alilitumia kuitangaza Jamhuri ya Watu wa China mwaka 1949.
Mnamo Mei 20, serikali ikatangaza hali ya hatari jijini Beijing, na wanajeshi pamoja na magari ya mizinga wakaitwa kuwatawanya watu hao. Hata hivyo, umati mkubwa wa wanafunzi na wananchi wengi wakawazuia wanajeshi hao kusonga mbele, na hadi kufikia Mei 23 majeshi ya serikali yalikuwa yamerudi nyuma nje ya Beijing. Juni 3, huku usuluhishi wa kumaliza mgomo huo ukiwa umeshindwa kufikiwa na madai ya mabadiliko ya kidemokrasia yakiendelea kushika kasi, majeshi yakapokea amri kutoka serikali ya China kuivamia Tiananmen Square na mitaa yote ya Beijing.
  
Jun 3, 1916:

RAIS WOODROW WILSON ASAINI SHERIA YA ULINZI WA TAIFA


Mnamo Juni 3, 1916, Rais wa Marekani Woodrow Wilson anasaini sheria ya Ulinzi (National Defense Act), ambayo ilitanua ukubwa na muundo wa ‘National Guard’—mtandao wa vikosi vya ulinzi vya taifa ambao ulikuwa unakua kwa kasi tangu nyakati za ukoloni.
Ingawa Theodore Roosevelt na wanachama wengine wa Republican walikuwa wakiisukuma Marekani iingie kwenye Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, lakini Wilson, aliyeingia madarakani mwaka 1912, alishikiria msimamo wake wa kutofungamana na upande wowote katika miaka kadhaa ya vita hivyo. Katika nusu ya kwanza ya mwaka 1916, huku vikosi vya Jeshi la Marekani pamoja na National Guard vikiitwa kupambana na kiongozi wa waasi wa Mexico Pancho Villa wakati aliposhambulia majimbo ya Kusini Magharibi ma Marekani, Wilson na Baraza la Congress wakaona kuna umuhimu wa kuimarisha majeshi na kuongeza matayarisho ya kijeshi ya Marekani. Ndipo akasaini sheria hiyo Juni 3.
Pia mwezi Juni 1916, Wilson alifanikiwa kupitisha sheria ya jeshi la majini, Naval Appropriations Act, ambayo ililenga kulifanya Jeshi la Maji la Marekani kuwa sawa na lile la Uingereza hadi kufikia mwaka 1925. Mwezi Novemba mwaka huo, Wilson akachaguliwa tena huku kauli mbiu ya kampeni zake ikiwa ‘Hakutuhusisha kwenye vita’.

Jun 3, 1940:

WAJERUMANI WAISHAMBULIA PARIS KWA MABOMU



Tarehe kama ya leo mwaka 1940, vikosi vya jeshi la anga la Ujerumani vinaishambulia Paris kwa mabomu, na kuua watu 254, wengi wao wakiwa raia wa kawaida. Hii ilikuwa ni wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Wakiwa wamedhamiria kuvuruga uchumi na jeshi la Ufaransa, kupunguza idadi ya watu, na kuvunja morali na uwezo wa kuunga mkono mataifa mengi, Wajerumani waliushambulia mji wa Paris bila kujali watakaokufa ni raia wa kawaida, wakiwemo watoto wadogo.
Mashambulizi hayo yalifanikiwa kuleta hofu, kwani waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa aliweza kuwazuia maofisa wa serikali wasitoroke Paris akiwatishia kwamba wangepata adhabu kali.

Jun 3, 1970:

NIXON ASEMA OPERESHENI YA CAMBODIA ILIKUWA NA MAFANIKIO


Katika hotuba yake iliyoonyeshwa kwenye luninga tarehe kama ya leo mwaka 1970, Rais Richard Nixon anakiri kwamba operesheni ya majeshi ya pamoja kati ya Marekani Vietnam Kusini iliyofanyika nchini Cambodia “ilikuwa na mafanikio makubwa zaidi katika vita hiyo ya muda mrefu," na kwamba alikuwa na uwezo wa kuanza kuondoa vikosi vya Marekani Kusini mwa Vietnam.
Marekani na vikosi vya jeshi la Vietnam Kusini walikuwa wameanzisha mapambano huko Cambodia kuanzia Aprili 29, 1967, operesheni ambayo ilihusisha maeneo 13 ya kuwafagia wanajeshi wa Vietnam Kaskazini umbali wa maili katikati ya Cambodia. Wanajeshi 50,000 wa Vietnam Kusini na wanajeshi 30,000 wa Marekani walihusika kwenye operesheni hiyo ikiwa ni operesheni kubwa zaidi kufanyika mwaka huo wa 1967.

Jun 3, 1990:

BUSH NA GORBACHEV WAMALIZA MKUTANO WA PILI


Rais George Bush wa Marekani na Rais Mikhail Gorbachev wa Urusi wamaliza mkutano wao wa siku tatu tarehe kama ya leo mwaka 1990 kwa maneno mazuri ya urafiki lakini bila kuwa na maafikiano sahihi ya muungano wa Ujerumani.
Bush na Gorbachev walifanya mkutano wao wa pili jijini Washington, D.C. Mada kubwa ilikuwa hali ya baadaye ya Ujerumani iliyoungana. Utawala wa Kikomunisti Ujerumani Mashariki ulikuwa umeanguka na Ukuta wa Berlin ulikuwa umeporomoshwa mwaka 1989. Tofauti zikajitokeza baina ya Marekani na Urusi kuhusu suala la Ujerumani iliyoungana katika Vita Baridi Ulaya.
Marekani ilitaka Ujerumani mpya iwe mwanachama wa NATO (North Atlantic Treaty Organization), umoja uliokuwa umeundwa tangu mwaka 1949 kwa ajili ya kujihami dhidi ya Urusi iliyokuwa inataka kujitanua Ulaya Magharibi.
Urusi nayo ikiwa tayari inahofia Ujerumani iliyoungana na yenye nguvu za kijeshi, ikahofia Ujerumani isijiunge na NATO. Gorbachev alipendekeza kwamba Ujerumani mpya iwe mwanachama wa NATO na Warsaw Pact, umoja wa kikomunisti uliofanana na NATO.
Mbali ya mazungumzo ya suala hilo mkutano huo wa pili ulizungumzia hatma ya Lithuania, jamhuri ya Kisovieti ambayo ilikuwa imetangaza uhuru wake mwisho mwa mwaka 1989. Serikali ya Urusi iliitikia kwa ukali kuhusu harakati za uhuru wa Lithuania, ikiweka vikwazo vya kiuchumi na kutishi kuivamia kijeshi. Utawala wa Bush uliunga mkono uhuru wa Lithuania na kuitaka Urusi iachane na vitisho hivyo dhidi ya taifa hilo. Hakuna maafikiano yaliyofikiwa kwa mada zote mbili.

Jun 3, 1937:

DUKE WA WINDSOR AFUNGA NDOA


Nchini Ufaransa, tarehe kama ya leo mwaka 1937, Duke wa Windsor—ambaye alikuwa Mfalme Edward VIII wa Uingereza na Ireland Kaskazini – anamuoa Wallis Warfield, mtalaka wa Kimarekani ambaye alisababisha aliachie taji lake la Ufalme wa Uingereza Desemba 1936.
Edward, aliyezaliwa mwaka 1896, alikuwa mtoto wa kwanza wa Mfalme George V, ambaye alitawala Uingereza kuanzia mwaka mwaka 1910. Alikuwa ofisa wa jeshi wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia na katika miaka ya 1920 alifanya ziara nyingi za kiutu ng’ambo akiwa Prince wa Wales, taji linalotolewa kwa watoto wa kiume ambao ndio wanaotarajiwa kuwa warithi wa Ufalme wa Uingereza.
Wakati wa kushuka wa kuchumi, alisaidia kuandaa program za kazi kwa ajili ya watu wasio na ajira na alikuwa anaheshimiwa na watu wengi katika miaka ya mwisho ya uhai wa baba yake.
Edward, akiwa bado hajaoa wakati akikaribia kutimiza miaka 40, akajiunga na jumuiya ya watanashati wa London na kila wakati akawa anahudhuria pale Fort Belvedere, nyumbani kwao. Hadi kufikia mwaka 1934, alikuwa amezama kwenye penzi zito na mwanamke Mmarekani Wallis Warfield Simpson, ambaye alikuwa ameolewa na Ernest Simpson, mfanyabiashara Mwingireza-Mmarekani ambaye aliishi naWallis jirani na London. Wallis, ambaye alizaliwa Pennsylvania mwaka 1896 na kukulia Maryland, awali alikuwa ameolewa na kutalikiana na rubani wa kikosi cha jeshi la Majini la Marekani.
Familia ya kifalme ilipinga uamuzi wa Edward kumuoa kimada huyo aliyeolewa akaachika, lakini kufikia mwaka 1936 Edward akaamua kumuoa Wallis. Kabla hajajadiliana uamuzi huo na baba yake, Mfalme George V akafariki dunia Januari 20, 1936, na Edward akatawazwa mfalme.
Mfamle mpya alikuwa maarufu kwa watu wake, na sherehe za kutawazwa kwake zilipangwa kufanyika Mei 1937. Uhusiano wake na Wallis ukaripotiwa na magazeti ya Marekani na bara zima la Ulaya, lakini kutokana na makubaliano ya kiungwana baina ya serikali na vyombo ya habari vya Uingereza, uhusiano huo haukuweza kuripotiwa kwenye magazeti ya Uingereza. Oktoba 27, 1936, Wallis akapewa hati ya awali ya talaka, akiwa na nia hasa ya kuolewa na mfalme, hali iliyoleteleza kuwepo kwa kashfa nzito.
Kwa Kanisa la England na wanasiasa wengi wa Uingereza, mwanamke wa Kimarekani aliyeachika mara mbili alikuwa hakubaliki kuwa Mamlkia wa Uingereza. Winston Churchill, ambaye wakati huo alikuwa mwanachama wa Conservative asiye na sauti kuu, alikuwa manachama pekee kumuunga mkono Edward katika uamuzi huo.
Pamoja na vikwazo vyote dhidi yake, Edward hakuweza kuzuiwa. Akasema kwamba Wallis hatakuwa na haki ya hadhi ama mali, lakini Desemba 2 Waziri Mkuu Stanley Baldwin akapinga uamuzi huo kwamba haukuwa na maana yoyote.
Siku iliyofuata, kashfa hiyo nzito ikafumuka kwenye kurasa za mbele za magazeti ya Uingereza na ikajadiliwa hadharani kwenye Bunge. Baada ya kutofikia muafaka wowote, mfalme akaachia taji lake Desemba 10. Siku iliyofuata Bunge likaidhinisha uamuzi huo, na siku 325 za utawala wa Edward VIII zikafikia kikomo.
Jioni hiyo, mfamle huyo mstaafu akazungumza kwenye radio na kueleza: "Imekuwa vigumu kwangu kubeba mzigo wa uwajibikaji na kuachia majukumu ya Mfalme, kama ninavyotaka kufanya, bila msaada wa mwanamke nimpendaye."
Desemba 12, mdogo ake, Duke of York, akatangazwa kuwa Mfalme George VI. Siku hiyo mfalme mpya akamfanya kaka yake kuwa Duke wa Windsor.
Wakati huo, Edward alikua tayari ameondoka kwenda Austria, ambako alikuwa akiishi na rafiki zake pamoja na Wallis aliyekuwa akiendelea kusubiria talaka yake kamili. Mwanamke huyo alipata talaka yake Mei 1937. Juni 3, 1937 yeye na Duke wa Windsor wakafunga ndoa kwenye Kanisa la Chateau de Cande nchini Ufaransa. Kasisi wa Kanisa la England ndiye aliyefungisha ndoa hiyo, ambayo ilihudhuriwa na watu 16 tu.
Kwa miaka miwili iliyofuata, wawili hao walishi Ufaransa lakini walitembelea nchi nyingine za Ulaya, ikiwemo Ujerumani ambako Duke alienziwa na maofisa wa Kinazi Oktoba 1937 na akakutana na Adolf Hitler.
Baada ya kuanza kwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, Duke akakubali nafasi ya kuwa ofisa mshawishi kwa Ufaransa. Juni 1940, Ufaransa ikaangukia mikononi mwa majeshi ya Kinazi,na Edward na Wallis wakaenda Hispania.
Katika kipindi hicho, serikali ya Kinazi ilisuka mpango wa kumteka Edward kwa malengo ya kumrejesha kwenye taji la Ufalme wa Uingereza ili awe kibaraka wao. George VI, kama ilivyokuwa kwa waziri mkuu, Winston Churchill, alikuwa anapinga hatua yoyote ya amani dhidi ya Ujerumani ya Hitler. Akiwa hajui mpango wa utekaji nyara uliosukwa na Nazi lakini akitambua huruma ya Edward kwa Nazi kabla ya vita hivyo, Churchill akamteua haraka Edward kuwa gavana wa Bahamas huko West Indies. Edward akaenda huko Agosti 1, 1940, akikwepa meli ya Nazi SS ambayo ilitumwa kwenda kuwateka na mkewe.
Mwaka 1945, Duke akajiuzulu nafasi hiyo, na wawili hao wakarejea kuishi Ufaransa. Edward alikwenda mara chache sana England, hasa kuhudhuria mazishi ya Mfalme George VI mwaka 1952 pamoja na mama yake, Malkia Mary, mwaka 1953.
Ni mwaka 1967 ambapo Duke na mkewe walialikwa na familia ya kifalme kuhudhuria sherehe rasmi ya kifalme, kuweka shahada liyotolewa kwa Malkia Mary. Edward alifariki jijini Paris mwaka 1972 lakini akazikwa Frogmore, katika eneo la Windsor Castle. Mwaka 1986, Wallis na akazikwa pembeni yake.

Jun 3, 1965:

MNAREKANI ATEMBEA ANGANI


Juni 3, 1965 maili 120 juu ya ardhi, Meja Edward H. White II anafungua mlango wa chombo cha Gemini 4 na kutoka nje, akiwa mwanaanga wa kwanza Mmarekani kutembea angani.
Akiwa amefungwa na mkanda wenye urefu wa futi 25 na kudhibiti mwendo wake akitumia bunduki ya hewa ya oksijeni, White alibakia nje ya chombo hicho kwa dakika 20.

Akiwa mtembea angani, White alikuwa ametanguliwa na mwanaanga wa Urusi Aleksei A. Leonov, ambaye mnamo Machi 18, 1965, alikuwa binadamu wa kwanza kabisa kutembea angani.

No comments:

Post a Comment