Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 4 June 2014

MASKINI TEMBO WETU, WAMEKOSA NINI JAMANI?

Ndugu zangu,
Ujangili umeendelea kushika kasi nchini Tanzania, hasa wa tembo, licha ya jitihada kadhaa zinazofanywa na mamlaka husika.
Tembo kama huyu pichani anauawa kinyama na wendawazimu wachache ambao wanaangalia maslahi yao ya kuuza meno yake bila kujali hatma ya baadaye ya rasilimali zetu.
Zimekuwepo operesheni nyingi nchini, miongoni mwazo ni ile ya Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa mwaka 2013, ambayo ilisitishwa baada ya kudaiwa kwamba wasimamizi wake waliendesha vitendo vya utesaji kwa wale walioshukiwa kujihusisha na ujangili.
Lakini pamoja na kusitishwa huko, bado kikwazo kikubwa kinaonekana kipo serikalini, kwani tunaelezwa kwamba wapo maofisa wakubwa wanaojihusisha na biashara hiyo haramu, na wanatengeneza mamilioni ya fedha.
Ndugu zangu, lazima tuwe wazalendo, tuungane kwa pamoja kupinga unyama na ujambazi huu ambao kama hatukisimama imara unaweza kuwapukutisha hayawani wote nchini na tukabaki na picha za wanyama kwenye vitabu vyetu vya historia. Tembo ndiye mnyama mkubwa kabisa aliyesalia duniani katika jamii zile za dinosaur, hivyo ni urithi mwingine kwa vizazi vyetu.

Ndugu yenu,
Daniel Mbega,
Iringa - Tanzania

credit: www.kwanzajamii.com/?p=6216

No comments:

Post a Comment