Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 1 June 2014

HISTORIA TAREHE KAMA YA LEO: MGODI WA MAKAA YA MAWE WALIPUKA NA KUUA 236 JAPAN


Tarehe kama ya leo mwaka 1965 mgodi wa makaa ya mawe wa Yamano jirani na Fukuoka, Japan ulilipuka na kuua watu 236. Janga hilo lingeweza kuepukwa kama waendeshaji wa mgodi huo wangeweka hata tahadhari za msingi. Miaka sita nyuma, wachimbaji saba walipoteza maisha yao na wengine 24 kujeruhiwa vibaya kwenye mgodi huo kutokana na kutokuwepo na njia za kiusalama. Lakini bado Juni Mosi, 1965, jumla ya wachimbaji 559 waliingia kwenye mgodi ambao haukuwa na vipimo vya methanometer – ambavyo vinatumika kudhibiti kiwango cha mentane – wala kuwa na ving’amuzi vya colorimetric, ambavyo vinabaini kiwango cha kemikali kwenye hewa. Yoshio Sakarauchi, waziri wa biashara na viwanda wa Japan, alijiuzuru kwa kashfa hiyo.

JUNI 1, 1980 – CNN YAANZA RASMI


KATIKA tarehe kama ya leo mwaka 1980, Kituo cha Luninga cha CNN (Cable News Network) cha Marekani, ambacho ni cha kwanza kabisa duniani kurusha matangazo yake kwa saa 4, kilianzishwa rasmi. Kituo hicho kilianza kurusha matangazo hayo majira ya saa 12 za jioni kwa saa za Mashariki – EST (saa 8 usiku kwa saa za Afrika Mashariki) yakitokea kwenye makao yake makuu jijini Atlanta, Georgia. Habari iliyoongoza siku hiyo ni jaribio la kutaka kuuawa kwa kiongozi na mtetezi wa haki za binadamu Vernon Jordan. CNN ilibadili mtazamo kwamba taarifa zinaweza kutangazwa kwa wakati maalum tu kwa siku. Wakati CNN inaanzishwa, habari za luninga zilikuwa zimetawaliwa na vituo vikubwa vitatu - ABC, CBS and NBC- ambazo zilikuwa zinatangaza kwa dakika 30 tu usiku. Awali ikitazamwa na Wamarekani milioni mbili tu majumbani, kwa sasa CNN inatazamwa na Wamarekani milioni 89 na zaidi ya watazamaji milioni 160 ulimwenguni kote.
CNN ilikuwa wazo la Robert "Ted" Turner, mfanyabiashara aliyeitwa “Mdomo wa Kusini”. Turner alizaliwa Novemba 19, 1938 mjini Cincinnati,Ohio, na familia yake ilihamia Georgia akiwa motto mdogo ambapo baba yake alikuwa anamiliki kampuni kubwa ya matangazo ya mabango. Baada ya baba yake kujiua mwaka 1963, Turner alichukua jukumu la kuiongoza kampuni hiyo. Mwaka 1970 alinunua kituo cha televisheni cha Atlanta ambacho kilikuwa kinaelekea kufa, kikiwa kinatangaza filamu za zamani, lakini yeye akakiimarisha na kuwa kikubwa. Turner pia alinunua timu ya baseball ya Atlanta Braves na ile ya mpira wa kikapu ya Atlanta Hawks na kuonyesha michezo yake kwenye kituo cha TBS (Turner Broadcasting System).


HABARI ZA MAUAJI KWENYE KAMBI YA JESHI WAKATI WA VITA KUU YA PILI ZAJULIKANA HADHARANI KWA MARA YA KWANZA
Mojawapo ya magari yaliyotumiwa na utwala wa Kinazi wa Hitler kuwaua Wayahudi huko Chelmno, Poland.

Tarehe kama ya leo mwaka 1942, gazeti change la mjini Warsaw, Poland, Liberty Brigade, linaripoti hadharani taarifa za kuuawa kwa gesi ya sumu kwa makumi ya maelfu ya Wayahudi huko Chelmno, kambi ya mauaji nchini Poland—karibu miezi saba baada ya zoezi la kuwaua wafungwa kuanza wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Mwaka mmoja nyuma, ulikuwa umeanzishwa mpango wa "Final Solution," wa kuwaua Wayahudi wa Ulaya ambapo Wayahudi 700 waliuawa kwa gesi ya sumu kwenye gari ambamo walikuwa wakisafirishiwa kupelekwa katika kijiji cha Chelmno, Poland. Gari hili la gesi ndilo likaja kuwa chemba ya mauaji ya Wayahudi 360,000 kutoka katika jumuiya 200 nchini Poland. ‘Faida’ ya mauaji hayo ilikuwa ni ya kimya kimya na haikuonekana.
Mwezi mmoja kabla ya mkutano wa Wannsee wa mwezi Januari 1942, ambapo maofisa wa Kinazi waliamua kuzungumzia rasmi mauaji ya Wayahudi, magari ya gesi ya sumu huko Chelmno yalitumika kuua hadi Wayahudi 1,000 kwa kutwa.
Mnamo Juni 1, 1942, habari ya kijana wa Kiyahudi, Emanuel Ringelblum, (ambaye alitoroka kwenye kambi ya mauaji huko Chelmno alikokuwa amelazimishwa kuzika miili ya watu waliokuwa wanamwagwa na magari yenye sumu), ikachapishwa na gazeti change la Kisoshalisti nchini Poland la Liberty Brigade. Ndipo Mataifa ya Magharibi yalipobaini unyama uliokuwa ukifanywa na Wanazi.

BENEDICT ARNOLD AFIKISHWA MAHAKAMANI WAKATI WA MAPINDUZI YA MAREKANI


Usikilizaji wa kesi ya Benedict Arnold ulianza huko Philadelphia, Pennsylvania. Baada ya kuonekana na rekodi safi huko nyuma mwanzoni mwa Mapinduzi ya Marekani, Arnold akashtakiwa kwa makosa 13 ya ukosefu wa uadilifu, ikiwemo kutumia vibaya magari ya serikali na kununua na kuuza vitu kwa magendo.
Japokuwa Arnold alifutiwa mashtaka yote, Jenerali George Washington akatoa amri ya kumweka ndani.
Wakati akiwa safarini katika kituo muhimu cha West Point kuona namna wanavyoweza kukabiliana na majeshi ya Uingereza, Arnold aliamua kumpuuza Washington na Wamarekani. Aliona kwamba hakuwa amezawadiwa au kushukuriwa kutokana na mafanikio yake ya kijeshi kwenye vita hivyo. Akaanza kuwasiliana na majasusi wa Uingereza kwa lengo la kuasi ili West Point iingie mikononi mwa Waingereza ambao tayari walikuwa wanaushikilia mji wa New York, hivyo kwa kuutwaa West Point wangeweza kuwa na nafasi ya kuzuia majeshi ya Marekani yaliyokuwa New England.
Mnamo Agosti 1780, Sir Henry Clinton alimpatia Arnold Pauni 20,000 kwa kuwapatia Waingereza askari 3,000 wa Marekani pamoja na kuusalimisha West Point. Arnold akamweleza Jenerali Washington kwamba West Point ilikuwa tayari kukabiliana na Waingereza wakati ukweli haukuwa hivyo. Pia alijaribu kuweka mtego wa kukamatwa kwa Jenerali Washington, mpango huo ungeweza kufanikiwa lakini taarifa yake ilichelewa kuwafikia Waingereza na Washington akatoroka. Mpango wa West Point kuangukia mikononi mwa Waingereza nao ulifeli wakati kanali mmoja wa Marekani alipopuuza amri ya Arnold ya kutoishambulia meli ya Waingereza.
Siri ya Arnold kusailiti ilifahamika kwa Wamarekani wakati ofisa mmoja wa Uingereza John AndrĂ©, aliyejifanya kama mesenja, alipokamatwa na kikosi cha AWOL cha Wamarekani waliokuwa msituni kaskazini mwa New York City.


WAJERUMANI WASHAMBULIA VIKOSI VYA UINGEREZA YPRES SALIENT

SIKU kama ya leo mwaka 1916, wakati vikosi vya wanamaji vya Ujerumani na Uingereza vilipopambana katika Bahari ya Kaskazini wakati wa Vita ya Jutland na Wafaransa wakipambana kuhakikisha Wajerumani hawautwai mji wa Verdun, vikosi vya Ujerumani vikaanzisha mashambulizi makubwa dhidi ya Uingereza huko Ypres Salient katika eneo la Western Front. Hii ilikuwa na wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.

KAMPUNI YA MAGARI YA NISSAN YAANZISHWA

Juni Mosi kama leo, mwaka 1934, kampuni ya Jidosha-Seizo Kabushiki-Kaisha (kwa Kiingereza Automobile Manufacturing Co., Ltd.) ya jijini Tokyo, yapata jina jipya na kuitwa: Nissan Motor Company.
Jidosha-Seizo Kabushiki-Kaisha ilianzishwa Desemba 1933. Nissan ilitengeneza gari lake la kwanza aina ya Datsun kwenye mtambo wake wa Yokohama mnamo Aprili 1935 na mwaka huo ikaanza kusambaza magari yake kwenda Australia. Kuanzia mwaka 1938 hadi wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, Nissan ikaanza kutengeneza malori na magari ya vita. Majeshi ya Washirika yalikiteka kiwanda cha Nissan mwaka 1945 na hayakukirejesha hadi miaka kumi baadaye.
Mwaka 1960, Nissan ikawa kampuni ya kwanza ya magari ya Kijapani kutwaa tuzo ya Uhandisi ya Deming. Aina mpya ya magari ya Datsun kama Bluebird (1959),  Cedric (1960) na Sunny (1966) yaliweza kuongeza mauzo ya Nissan ulimwenguni.
  
WAMUUNGA MKONO NIXON VIETNAM

Jun 1, 1971: Tarehe kama ya leo mwaka 1971 kundi la Vietnam Veterans for a Just Peace linajitokeza hadharani kuunga mkono uamuzi wa Rais Richard Nixon wa kuendesha vita vya Vietnam.

VIGOGO WAKUTANA KUJADILI VIETNAM

Tarehe kama ya leo mwaka 1964 maofisa wa juu wa Marekani wakutana mjini Honolulu kwa siku mbili kujadiliana kuhusu Vita ya Vietnam. Waliohudhuria ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje Dean Rusk, Waziri wa Ulinzi Robert McNamara, Balozi Henry Cabot Lodge, Jenerali William Westmoreland, Jenerali Maxwell Taylor, na Mkurugenzi wa Idara ya Kijasusi ya Marekani (CIA) John McCone. Mjadala huo ulihusisha hali ya vita Kaskazini mwa Vietnam, ikiwemo maeneo 94 muhimu ya kushambulia.

VITA YA COLD HARBOR YAANZA

Tarehe kama ya leo mwaka 1864, majeshi ya Uingereza (Confederates) anavishambulia vikosi vya Union katika eneo la Cold Harbor, Virginia, karibu maili 12 kutoka Richmond. Hii ilikuwa wakati wa Vita vya Mapinduzi.
Tangu kuanza kwa mwezi Mei 1864, Jenerali wa Jeshi la Union Ulysses S. Grant alikuwa amejipanga kulishambulia Jeshi la Robert E. Lee Kaskazini mwa Virginia karibu na Richmond. Hali hiyo ilikuwa na madhara kwa Jeshi la Grant huko Potomac, ambapo watu 60,000 waliuawa.


URUSI YAMSHTAKI SHCHARANSKY KWA UHAINI

Tarehe kama ya leo mwaka 1977 wakati wa Vita Baridi, serikali ya Urusi ilimfungulia mashtaka ya uhaini Anatoly Shcharansky, kiongozi wa kutetea hali za Wayahudi na mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Russia. Kitendo hicho kilitazamwa na mataifa ya Magharibi kama changamoto ya moja kwa moja kwa Rais wa Marekani Jimmy Carter kuhusiana na sera yake mpya ya mambo ya nje kuhusu haki za binadamu na kupinga ukandamizaji wa Urusi.
Shcharansky, aliyekuwa na miaka 29 na mtaalam wa kompyuta, alikuwa mashuhuri katika kundi lililojiita ‘Helsinki Group’ katika Muungano wa Kisovieti. Kundi hilo lilianzishwa mwaka 1975, baada ya kusainiwa kwa Sheria ya Usalama ya Ulaya (European Security Act) ambayo pia inajulikana kama Helsinki Accords. Mkutano huo uliofanyika jijini Helsinki, Finland uliwahusisha viongozi wa Marekani na Urusi ambao waliamua kuwaalika viongozi wa nchi nyingine 35.
Shcharansky alishtakiwa kwa uhaini, hususan kwa kupokea msaada wa fedha kutoka CIA ili kuanzisha machafuko nchini Urusi. Baada ya mwenendo wa mashtaka, akahukumiwa kifungo cha miaka 14 jela. Baadaye akaachiliwa huru Februari 1986, baada ya yeye na wafungwa wengine wane walipobadilishana na majasusi wanne wa Urusi waliokuwa wamefungwa huko Magharibi. Hiki kilikuwa ni kipindi cha utawala wa Mikhail Gorbachev ambaye wakati anaingia madarakani mwaka 1985, aliahidi kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa ili kupoza hali ya hewa nchini Urusi. Pamoja na hali hiyo, wanachama wa kundi la Helsinki na vikundi vingine waliendelea kudai uhuru na demokrasia na haki za binadamu hadi Muungano wa Urusi ulipovunjika mwaka 1991.

Jun 1, 1941:

WAJERUMANI WATWAA MJI WA CRETE 1941

Tarehe kama ya leo mwaka 1941 wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia, mji wa Crete, ambao ulikuwa ngome ya Majeshi ya Washirika nchini Ugiriki, unatwaliwa na Wajerumani katika mapambano makali.
Mwisho mwa mwaka 1940, jeshi la Ugiriki, likisaidiwa na jeshi la anga la Uingereza, lilifanikiwa kuizuia Italia isivamie nchi hiyo. Lakini Aprili 1941, ushindi huo ukawa kipigo wakati kiongozi wa Nazi, Adolf Hitler alipoliongoza jeshi lake ambalo halikuwa limepigwa ili kuishambulia Ugiriki. Jeshi la Ujerumani lilikwenda haraka na kuishambulia Ugiriki  kiasi kwamba Waingereza waliahirisha mpango wao wa kutuma vikosi vyao kuisaidia Ugiriki.
Aprili 23, mfalme wa Ugiriki na serikali yake walihamia Crete, kisiwa kilichoko kusini mwa Ugiriki, na Aprili 24 vikosi vya Majeshi ya Washirika vilihamia kisiwani humo. Wajerumani walishambulia meli hizo na kuua askari na mabaharia 15,000 wa vikosi vya Washirika. Hadi kufikia Aprili 29, askari 50,000 wa Uingereza, Ugiriki, Australia na New Zealand walikuwa wametua kisiwani humo.
Wiki tatu baadaye Wajerumani walianzia harakati za kuivamia Crete, na zaidi askari 20,000 wa miavuli wa Ujerumani walikuwa wametua kisiwani humo. Pamoja na mapambano makali, Wajerumani walifanikiwa kuutwaa mji huo na kufikia Juni 1, askari 20,000 waliosalia wa Vikosi vya Washirika walikuwa wametoroka.

Jun 1, 1900:

HOOVER ATEKWA KATIKA MACHAFUKO CHINA

Tarehe kama ya leo mwaka 1900, Herbert Hoover ambaye baadaye alikuja kuwa Rais wa Marekani, pamoja na mkewe Lou walikamatwa katikati ya machafuko nchini China maarufu kama Boxer Rebellion.
Baada ya kufunga ndoa mjini Monterey, California, mnamo Februari 10, 1899, Herbert na Lou Hoover waliondoka kwenda fungate nchini China, ambako Hoover alitarajiwa kuanza kazi mpya kama mshauri wa uchimbaji madini kwa mtawala wa China akiwa na kampuni ya Bewick, Moreing and Co. Wanandoa hao walikuwa wameoana katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja wakati kundi la wanaharakati la China lilipoasi dhidi ya wakoloni, wakwawakamata Wazungu 800 kwenye mji wa Tientsin. Hoover aliwaongoza wazungu wenzake kujenga kingo katika makazi yao ya mji huo wakati mkewe Lou alikuwa akisaidia katika hospitali. Inaelezwa kwamba, wakati wa machafuko hayo yaliyodumu kwa mwezi mmoja, Hoover aliwaokoa watoto wa Kichina katikati ya mapigano.
Baada ya vikosi vya majeshi ya ushiriki kuwaokoa akina Hoover na kuwasafirisha wazungu wengine nje ya China, Herbert Hoover akawa mmoja wa wamiliki wa Bewick, Moreing and Co. alikuwa waziri wa biashara chini ya marais Warren Harding na Calvin Coolidge kuanzia mwaka 1921 hadi 1924. Akawania urais mwaka 1928 na kushinda.


Jun 1, 1871:

JOHN WESLEY HARDIN AWASILI ABILENE 




Tarehe kama ya leo mwaka 1871, John Wesley Hardin, mmoja wa wahalifu wakubwa katika historia ya Marekani, aliwasili huko Abilene, Kansas, ambako alijenga urafiki wa muda na Marshal Wild Bill Hickok.
Hardin alianza tabia ya fujo na ugomvi tangu akiwa mdogo. Wakati akiwa na miaka 14, nusura amuue kijana mmoja wakati wakigombea msichana, akimchoma mara mbili kwa kisu. Mwaka mmoja baadaye akamuua mwanamume mwenye asili ya Kiafrika wakati walipopambana katika mieleka. Wakati anakwenda kufungwa jela mwaka 1878, Hardin alidai kwamba alikuwa amewaua watu 44.
Mwaka 1871, wakati Hardin akiwa na miaka 18, mmiliki mmoja wa ranchi wa Texas akamwajiri kijana huyo kuongoza kundi la ng’ombe kutoka Chisholm Trail kwenda Abilene, Texas. Hardin alikuwa anatamani kuondoka Texas, kwani siku chache kabla, alikuwa amemuua polisi wa Texas aliyekuwa akimsafirisha yeye kumpeleka Waco kusikiliza kesi yake. Hardin alitaka aishi maisha ya kujificha, lakini akashindwa kuzidhibiti hasira zake kwa muda mrefu. Wakati akiswaga ng’ombe, kundi la ng’ombe wa jamaa mmoja wa Mexico likachanganyika na ng’ombe aliokuwa nao Hardin. Alipolalamika kwa Mexico aliyekuwa akiswaga ng’ombe hao, wakashindwa kuelewana, hivyo akaamua kumpiga risasi ya kwenye moyo.
Wakati Hardin alipowasili Abilene, Kansas, siku kama ya leo mwaka 1871, kiongozi wa mji huo, Wild Bill Hickok, hakuwa na haja ya kumshtaki mtu aliyeua nje ya himaya yake. Badala yake akawa amempenda kijana huyo ambaye alikuwa amemzidi miaka 16 na wakawa marafiki, japo urafiki wenyewe ulikuwa wa mashaka. Kama ilivyokuwa kwa wanasheria wa magharibi, Wildd Bill Hickok alikuwa amefanya mauaji kadhaa. Lazima alikuwa ameona kitu ndani ya Hardin ambacho kilimvutia, akiamini kwamba kwa tabia yake ya hasira angeweza kumtumia. Kwa upande wake, Hardin alifurahi kuwa rafiki wa mtu huyo maarufu kwa upigaji bunduki.
Kwa wiki kadhaa, Hickok na Hardin walikunywa pamoja na walichangia wasichana, lakini imani ya Hickok kwa kijana huyo ilikuwa ndogo. Wakati akiwa Abilene, Hardin alikodi chumba katika hoteli ya Amerina House. Usiku mmoja, mgeni mmoja wa chumba cha jirani alikuwa anakoroma sana. Hardin alikerwa mno na kitendo hicho hivyo akaanza kufyatua risasi ili kumnyamazisha. Risasi ya kwanza ilimshtua mgeni huyo, lakini ile ya pili ilimnyamazisha moja kwa moja.
Hardin akabaini kwamba urafiki wake na Hickok wala usingemsaidia. "Niliamini," Hardin alisema baadaye, "kwamba kama Wild Bill angenikuta katika hali nisiyo na msaada, wala asingesikiliza maelezo, bali angeniua ili aongeze kwenye orodha yake." Akiwa amevaa singland, Hardin alitoroka kupitia dirisha la hoteli na kuingia mitaani. Usiku huo akajificha kwenye jumba la kufugia farasa, alfajiri na mapema akaiba farasi mmoja na kwenda kwenye kambi ya ng’ombe. Siku iliyofuata akaelekea Texas, hakurudi tena Abilene.

Alikufa mwaka 1895 baada ya kupigwa risasi mgongoni na polisi wa El Paso. Alikuwa na miaka 42.

No comments:

Post a Comment