Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 3 June 2014

'HAPPY BIRTHDAY': CHARLES KAJEGE NA LARRY MCMURTRY


CHARLES MUGUTA KAJEGE 

Alizaliwa Juni 3, 1962. Aliingia Bungeni mwaka 2005 kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM). Baada ya matokeo kutenguliwa na Mahakama Kuu mwaka 2009 kufuatia kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na Mtamwega Mgaywa wa TLP, alikata rufaa katika Mahakama ya Rufaa iliyomrejesha tena. Lakini akashindwa kwenye kura za maoni na Alphaxard Kangi Lugola. Elimu ya msingi aliipata katika shule ya Namibu (1968 hadi 1974), elimu ya sekondari aliipata katika shule ya sekondari Kazima (1977 hadi 1980) baadaye akajiunga na kidato cha tano na sita katika shule ya Azania (1981 hadi 1983). Kati ya mwaka 1986 na 1992 alihitimu shahada ya kwanza ya Uchumi katika Chuo Kikuu cha Bogazigi, mwaka 1994 akahitimu stashahada ya Uhusiano wa Kimataifa katika Chuo cha Centre For Foreign Relations, mwaka 1997 na 1999 alihitimu shahada ya uzamili katika Fedha na Uchumi katika Chuo Kikuu cha London, Uingereza, na mwaka 2000 na 2002 alihitimu shahada ya uzamili katika Fedha na Masoko kutoka Chuo Kikuu cha Miami, Marekani.
Tangu mwaka 1984 hadi 2005 alikuwa Ofisa wa Mambo ya Nje katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Jun 3, 1936:

MWANDISHI LARRY MCMURTRY AZALIWA


Larry McMurtry, mmoja wa waandishi wa kisasa wenye vipaji wa magharibi, anazaliwa siku kama ya leo, lakini mwaka 1936 huko Wichita Falls, Texas.
Familia ya McMurtry ilikuwa imejihusisha na masuala ya ranchi Texas kwa mizazi vitatu, na yeye alianza kujihusisha na masuala ya ranchi tangu akiwa mdogo.
Hata hivyo, McMurtry, alikuwa anapendelea zaidi vitabu kuliko mifugo. Baada ya kusoma Chuo Kikuu cha Rice, McMurtry alielekea California, ambako alijiunga na program ya uandishi wa ubunifu ya Wallace Stegner katika Chuo Kikuu cha Stanford.
Stegner, ambaye alikuwa ameandika vitabu kadhaa vya riwaya vilivyofanya vizuri, kikiwemo The Big Rock Candy Mountain (1943), alibaini kipaji cha McMurtry na akamshawishi aandike kuhusiana na Magharibi ya sasa.
Akiwa hana uhakika kama angeweza kuishi kwa kutegemea uandishi, McMurtry akaanzisha maduka ya vitabu katika miji ya ya Texas na Washington, D.C., na kuugawanya muda wake kati ya maeneo hayo mawili. Katika kitabu chake cha kwanza cha riwaya, McMurtry pia alihusisha masuala ya mijini na vijijini, ikiwa ni staili mpya.
Vitabu vya mwanzo kabisa vya McMurtry, ni pamoja na Horseman, Pass By (1961), ambacho kilikuwa msingi wa filamu maarufu ya Hud. Vitabu vingine vya McMurtry ni pamoja na Leaving Cheyenne (1963), The Last Picture Show (1966), Moving On (1970), Lonesome Dove (1986), Anything for Billy (1988), na Buffalo Girls (1990).


No comments:

Post a Comment