Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 3 June 2014

BURIANI ZAMANI: LEW WASSERMAN WA HOLLYWOOD


Rais wa muda mrefu wa kampuni ya Motion Picture Association of America (MPAA), Jack Valenti alipata kusema: “Kama Hollywood ni Mlima Olympus, basi Lew Wasserman ni Zeus (mungu).”
Wasserman, wakala na mtendaji mkuu wa studio anayetajwa kuwa mtu mwenye mafanikio makubwa katika Hollywood kwa miaka 40 baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, alifariki Juni 3, 2002 akiwa na miaka 89.
Alizaliwa Cleveland, Ohio, akiwa mtoto wa Wayahudi wa Orthodox waliohamia Marekani wakitokea Russia. Alianza kuigiza mitaani akishiriki michezo mbalimbali kabla ya kupata kazi kwenye kampuni ya Music Corporation of America (MCA) jijini Chicago. Mwaka 1938, mwanzilishi wa MCA Jules Stein alituma wasaidizi wake wakatanue biashara za kampuni yake huko Hollywood, Los Angeles, na kufikia mwaka 1948 akamteua Wasserman kuwa rais wa MCA.
Wasserman akaanza kupanua biashara ya filamu ya MCA, akiingia mikataba na nyota mbalimbali wa Hollywood na kuwaibua wengine. Baada ya WWII, orodha ya wateja wa MCA ilikuwa ndefu ikihusisha wachezaji filamu wakubwa, wakiwemo Bette Davis, Errol Flynn, James Stewart, Judy Garland, Henry Fonda, Myrna Loy, Fred Astaire, Ginger Rogers, Jack Benny, George Burns, Gracie Allen, Gregory Peck and Gene Kelly.
Pia Wasserman alikuwa amewaajiri waongoza filamu mahiri kama Billy Wilder na Alfred Hitchcock.


No comments:

Post a Comment