Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 2 June 2014

TAREHE KAMA YA LEO: KLABU ZA SOKA ZA ENGLAND ZAPIGWA ‘BAN’ ULAYA KWA MIAKA MITANO


 Maiti katika uwanja wa Heysel, Ubelgiji
 Wanausalama wakiangalia jinsi uwanja ulivyobomoka na kusababisha vifo vya watu 39.
 Uokoaji wa watu walioangukiwa na ukuta.
Na Juventus wakatwaa ubingwa kwa ushindi wa bao 1-0.


Tarehe kama ya leo, yaani Juni 2, 1985, Umoja wa Vyama vya Soka Ulaya (UEFA) lilizifungia klabu za soka za England kushiriki mashindano yote ya Ulaya. Adhabu hiyo ilifuatia vifo vya mashabiki 39 wa Italia na Ubelgiji kwenye Uwanja wa Heysel jijini Brussels katika vurugu zilizosababishwa na mashabiki wanazi wa England wakati wa mechi ya fainali ya Ulaya.
Mchezo wa fainali ya Klabu Bingwa Ulaya mwaka 1985 ulizikutanisha timu za Juventus ya Italia na Liverpool ya England, ambayo ilikuwa inatetea ubingwa wake. Majira ya saa 1 usiku, muda mfupi kabla ya mchezo kuanza, kundi la mashabiki wa Liverpool waliokuwa wamelewa chakari, ambao kutwa nzima walikuwa wanagida pombe kwenye baa za Brussels, wakawavamia mashabiki wa Juventus.
Katika harakati hizo, ukuta wa uwanja ukabomoka na kuwangukia baadhi ya watazamaji. Wengine walikanyagwa wakati wakikimbia kutoka nje ya uwanja. Kwa ujumla, mashabiki 32 wa Juventus walikufa, pamoja na watu wengine saba waliokuwa wakitazama. Mamia ya watu wengine waliumia.
Ili kuepuka vurugu nyingine zisije zikatokea, mchezo huo ukaendelea kama kawaida na Juventus wakaibuka mabingwa kwa ushindi wa bao 1–0.
Baada ya tukio hilo, klabu zote za England zikafungiwa kushiriki Klabu Bingwa laya na Kombe la UEFA kwa miaka mitano. Adhabu ya Liverpool, ambayo awali ilikuwa ya muda usiojulikana, baadaye ikawa kutoshiriki kwa miaka 10, na baadaye kupunguzwa hadi miaka sita.
Kuanzia mwaka 1977 hadi 1984, klabu za England zilikuwa zimetwaa mataji saba kati ya nane ya Ulaya, na kuzuiliwa kwao lilikuwa pigo kwa nchi na mchezo huo kwa ujumla.
Hata hivyo, wakati adhabu hiyo ilipotolewa, Waziri Mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher aliunga mkono kwa asilimia zote akisema: "Lazima mchezo usafishwe kutokana na vujo za manazi hawa kuanzia nyumbani na ndipo pengine tunaweza tukaenda ng’ambo tena."
Madhara hayo hayakuishia kwenye adhabu ya kufungiwa, Liverpool ilijikuta mashabiki wake 14 wakipatikana na haia ya kuua bila kukusudia nchini Berlin katika hukumu ya mwaka 1989 baada ya kesi hiyo kuendeshwa kwa miezi mitano. Mashabiki hao wakafungwa miaka mitatu jela, huku wakipunguziwa nusu ya kifungo hicho.
Klabu za England zilirejeshwa kwenye mashindano ya Ulaya baada ya fainali za Kombe la Dunia 1990. Miaka 15 baadaye, mnamo Aprili 5, 2005, Liverpool ikaichapa Juventus 2-1 kwenye mchezo wa kwanza war obo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Ilikuwa ni mechi ya kwanza tangu timu hizo zilipopambana kwenye Uwanja wa Heysel. Mashabiki walisimama kimya kwa muda mwanzoni mwa mchezo, kukumbuka watu 39 waliokufa mwaka 1985. Mechi ya marudiano ilifanyika siku tisa baadaye Aprili 14 mjini Turin, ambapo Liverool iliilazisha Juventus kwenda suluhu. Liverpool iliendelea hadi kutwaa ubingwa wa Ulaya msimu huo.


Jun 2, 1953:

MALKIA ELIZABETH II ATAWAZWA







Mnamo Juni 2, 1953,Malkia Elizabeth II alitawazwa rasmi kwenye taji la ufalme la Uingereza katika sherehe kubwa. Askofu Mkuu wa Canterbury Geoffrey Fisher ndiye aliyemtawaza. Watu mashuhuri, viongozi na wageni elfu moja walihudhuria sherehe hizo huko Westminster Abbey, jijini London na mamia kwa mamilioni walisikiliza kupitia kwenye vituo vya radio na kwa mara ya kwanza wakatazama kupitia kwenye luninga.
Baada ya sherehe hizo, mamilioni ya watu walimshangilia malkia huyo aliyekuwa na miaka 27 na mumewe, Duke wa Edinburgh aliyekuwa na miaka 30, wakati walipopita barabarani kwa umbali wa maili tano.
Elizabeth, aliyezaliwa mwaka 1926, alikuwa binti wa kwanza wa Prince George, mtoto wa pili wa kiume wa Mfalme George V. babu yake alifariki mwaka 1936, na baba yake mkubwa akatawazwa Mfalme Edward VIII. Baadaye mwaka huo, Edward akaondolewa kwenye ufalme kufuatia uamuzi wake wa kumuoa Wallis Warfield Simpson, Mmarekani aliyekuwa ametalikiwa, na baba yake Elizabeth akatawazwa Mfalme George VI badala yake.
Wakati wa Vita vya Uingereza (Battle of Britain), Princess Elizabeth na mdogo wake, Princess Margaret, walishi mafichoni nje ya London, lakini wazazi wao waliingia matatizoni baada ya Hekalu la Kifalme (Buchingham Palace) kupigwa mabomu na vikosi vya anga vya Ujerumani. Baadaye wakati wa vita, Elizabeth akiwa amefundishwa na kuwa luteni usu katika vikosi vya wanajeshi wanawake ambapo alikuwa akiendesha na kutengeneza malori.
Mwaka 1947, aliolewa na binamu yake wa mbali, Philip Mountbatten, prince wa zamani wa Ugiriki na Denmark ambaye aliachia taji lake ili amuoe Elizabeth. Akatawazwa kuwa Duke wa Edinburgh wakati wa sherehe ya ndoa yao. Sherehe za ndoa yao ziliamsha mizuka ya Waingereza, ambao walikuwa wakikabiliwa na uchumi mbovu baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Mtoto wao wa kwanza, Prince Charles, alizaliwa mwaka 1948 hapo Buckingham Palace. Mtoto wa pili, Princess Anne, alizaliwa mwaka 1950. Mnamo Februari 6, 1952, walikuwa nchini Kenya katika ziara wakati waliposikia kwamba mfalme amekufa.
Mnamo Aprili 21, 2006, Malkia Elizabeth alitimiza miaka 80 (sasa ana miaka 88), na kuwa Mwingireza wa tatu kushikilia taji la Uingereza.


Jun 2, 1865:

VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE MAREKANI VYAMALIZIKA

Katika tukio lilionyesha kufikia mwisho wa Vita vya Wenyewe kwa Wenyewe nchini Marekani, Jenerali wa Confederate Edmund Kirby Smith, aliyekuwa akiongoza vikosi vilivyokuwa magharibi mwa Mississippi, tarehe kama ya leo mwaka 1865 alisaini makubaliano ya kusalimu amri yaliyotolewa na wasuluhishi wa Muungano. Baada ya Smith kusalimu amri, majeshi ya Confederates yakasambaratika na kuleta utulivu katika vita vya umwagaji damu mkubwa nchini Marekani vilivyodumu kwa miaka minne. Vita hivyo vilianza Aprili 12, 1861.


Jun 2, 1944:

MAREKANI YAANZA ‘KUSHUSHA MAKOMBORA’ KATIKA OPERESHENI FRANTIC


Tarehe kama ya leo mwaka 1944, warusha makombora wa Marekani kutoka Kikosi cha 15 cha Jeshi la Anga walianzisha Operesheni Frantic na kuanza kushusha makombora Ulaya ya Kati, wakitokea kwenye kituo chao cha anga cha Italia, lakini yakarushwa kutokea vituo vya anga vya Poltava, Urusi, katika kile ambacho kiliitwa "shuttle bombing."
Kikosi cha 15 cha Anga kiliundwa maalum kwa ajili ya kuuvuruga uchumi wa Ujerumani kikiongozwa na Jenerali Carl Spaatz, rubani mpiganaji wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Kikosi hiki kilianzishwa na Joseph Stalin kusaidia Red Army katika kampeni zake nchini Romania. Katika kubadilishana na msaada wa Kikosi cha 15, Stalin aliwaruhusu warusha makombora wa Marekani watue ndani ya ardhi ya urusi wakati wakiendesha Operesheni Frantic, ukiwa ni mpango wa kuuvuruga uchumi wa viwanda wa Ujerumani katika maeneo iliyokuwa imeyakalia ya Silesia, Hungary, na Romania.

Jun 2, 1915:

VIKOSI VYA AUSTRO-GERMAN VYWASHAMBULIA WARUSI HUKO PRZEMYSL


Mnamo Juni 2, 1915, vikosi vya Austro-Hungaria na Ujerumani viliendelea na mashambulizi yao dhidi ya wanajeshi wa Russia waliokuwa wakiushikilia mji wa Przemysl (sasa uko nchini Poland).
Vikosi vya Austro-German vilikuwa vinakaribia kupata ushindi dhidi ya jeshi la Russia lililokuwa limechoka huko Przemysl; hata hivyo mji huo uliangukia mikononi mwa Majeshi ya Kati chini ya Ujerumani siku iliyofuata, ushindi ambao hatimaye uliifanya Russia ishindwe kuumiliki Galicia.

Jun 2, 1935:

BABE RUTH ASTAAFU



Tarehe kama ya leo mwaka 1935, Babe Ruth, mmoja wa wacheza baseball hodari zaidi katika historia, alistaafu kucheza akiwa na timu ya Boston Braves baada ya kushiriki Major League kwa misimu 22. Mwaka uliofuata, Ruth, ambaye umbile lake lilikuwa kumbwa mno, akawa mmoja wa wachezaji watano walioingizwa kwenye orodha ya wachezaji mashuhuri (hall of fame).
George Herman Ruth alizaliwa Februari 6, 1895, katika familia maskini huko Baltimore. Akasoma shule ya wavulana ya  St. Mary's Industrial School iliyokuwa chini ya mapadre wa Kanisa Katoliki, huko ndiko alikojifunza kucheza baseball. Akiwa na miaka 19 akasajiliwa na timu ya Baltimore Orioles, ambayo ilikuwa ikishiriki ligi ndogo ya Boston Red Sox. Alichezea Red Sox hadi mwaka 1920 alipojiunga na New York Yankees na umaarufu wake ndio ulioifanya timu hiyo ikafungua uwanja wake wa Yankees.

Jun 2, 1924:

COOLIDGE ASAINI SHERIA YA RAIA WA INDIA


Tarehe kama ya leo mwaka 1924, Rais Calvin Coolidge alisaini Sheria ya Raia wa India (Indian Citizen Act), iliyotoa uraia wa moja kwa moja wa Marekani kwa wakazi wa Marekani waliozaliwa nchini humo.

Jun 2, 1886:

GROVER CLEVELAND AOA AKIWA IKULU


Rais Grover Cleveland anakuwa rais wa kwanza aliyeko madarakani kuoa akiwa Ikulu (White House) katika tarehe kama ya leo mwaka 1886.
Cleveland aliingia White House akiwa mseja (bachelor) na akaondoka madarakani akiwa na mke na baba wa watoto wawili. Mkewe alikuwa mwanamke mrembo aliyekuwa amemzidi kwa miaka 27, ambaye aliitwa Frances Folsom. Frances alikuwa binti wa mwanasheria mwenza na msaidizi wake Cleveland. Wakati binti huyo akiwa na miaka 11, baba yake akafariki na Cleveland akawa mlezi wake, akiendelea kuwa rafiki wa karibu wa mama yake.
Watu wengi walidhani Cleveland angeweza kumuoa mjane wa rafiki yake lakini badala yake wakashangazwa wakati alipomuoa binti wa rafikiye mara tu alipofikisha umri wa miaka 21.
Katika tukio lingine la kwanza ndani ya White House, binti wa pili wa Frances na Cleveland, Esther alikuwa mtoto wa kwanza kuzaliwa katika chumba cha kulala cha White House.


Majanga


Jun 2, 1921:

MAFURIKO YALETA UHARIBIFU COLORADO 


Mvua kubwa yanyesha tarehe kama ya leo, mwaka 1921 huko Pueblo County jimboni Colorado, na kuleta mafuriko makubwa yaliyosababisha vifo vya watu 120 na rasilimali na majengo yenye thamani ya dola 25 milioni (sawa na Dola 230 milioni kwa fedha za sasa) vikiharibiwa. Hadi kufikia wakati huo, haya yalikuwa mafuriko mabaya zaidi katika historia ya jimbo hilo.
Mto Arkansas unapita katika uwanda wa kusini-magharibi wa Colorado. Wananchi wa eneo hilo walikuwa wamejenga kingo kando ya mto kuzuia mafuriko. Hata hivyo, kingo hizo hazikufaa kitu kwa mafuriko hayo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha kwenye eneo hilo Juni 1921. Mafuriko haya yalidumu kwa wiki nzima.
  
Jun 2, 2012:

HOSNI MUBARAK AFUNGWA MAISHA


Tarehe kama ya leo mwaka 2012, rais wa zamani wa Misri, Hosni Mubarak, anakutwa na hatia ya kushindwa kuzuia mauaji ya mamia ya waandamanaji waliokuwa wakipinga serikali yake wakati wa machafuko makubwa maarufu ya mwaka 2011 ambayo yalishuhudia mwisho wa utawala wake wa karibu miaka 30.
Mubarak akiwa na miaka 84 alihukumiwa kifungo cha maisha jela.
Mzaliwa wa Misri mwaka 1928, Mubarak alikuwa kamanda wa jeshi la anga la Misri kabla ya kuteuliwa kuwa makamu wa rais mwaka 1975 chini ya Rais Anwar Sadat. Baada ya Sadat kuuawa na Waislamu wakati wa gwaride la jeshi jijini Cairo Oktoba 1981, Mubarak akawa rais wa nne wa Misri. Miongo mitatu kama mtawala wa taifa la Kiarabu lenye watu wengi zaidi ilitawaliwa na rushwa kubwa serikalini, vurugu za kisiasa na kudumaa kwa uchumi. Katika utawala wake wote, Misri ilikuwa chini ya “utawala wa hali ya hatari”, ukiipa nguvu serikali kukamata na kuwaeka watu vizuizini vila kuwafungulia mashtaka. Ukatili wa polisi uliripotiwa.
Maandamano yaliyosababisha Mubarak kung’oka yalianza Januari 25, 2011, wakati wananchi walipotaka aachie ngazi huku wakiandamana katika mitaa mbalimbali ya Cairo na miji mingine.

No comments:

Post a Comment