Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 4 June 2014

SEKONDARI YA LUMALA YAKABILIWA NA UPUNGUFU MKUBWA WA WALIMU WA SAYANSI

DSC0100Shule ya Sekondari ya Lumala ina upungufu mkubwa wa Walimu wa masomo ya Sayansi.
Shule hiyo ina walimu wawili tu wa masomo hayo kati ya walimu 52 waliyopo katika shule hiyo.
Hayo yamefahamika baada ya Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Angelina Madete baada ya kufanya ziara ya siku moja katika shule hiyo na kupata taarifa kutoka kwa Mkuu wa shule Bwana Christopher Mafuru.
Mwalimu Mkuu huyo alisema kwamba,pamoja na ukosefu wa walimu wa masomo ya Sayansi, shule hiyo ina  mradi wa upandaji miti kwa kuzingatia suala zima la utunzaji mazingira katika maeneo ya shule na makazi.
Shule hiyo ya Lumala imeshaotesha miche elfu kumi,kati ya hiyo miche 1,000 ni miche ya miti ya kivuli na maua.Mradi huo ni endelevu na utaendelea kupanda na kuotesha miti kadiri ya mahitaji ya shule.
Alisema kwamba mradi unakabiliwa na tatizo la ukame kutokananaukosefu wa mvuahali ambayo imefanya mradi huo kusimamisha kuotesha miti au miche katika mradi huo. Pamoja na changamoto hizo,shule ina mpango wa kuotesha miti zaidi ya 40,000  kwa mwaka 2014/2015.
Na Ofisi ya Makamu wa Rais. 
CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment