Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 30 December 2013

MSIMU WA KILIMO HUU, NALIMA MWENYEWE

 Mwenzenu nilisamehe Krismasi nikaenda shambani kulima. Naamini hii nayo ilikuwa ibada, maana ni vyema watoto wakagombea mlango wa chooni ili waisherehekee vyema sikukuu. Hata kama kashamba kadogo, kananitosha.

 Mvua zenyewe hizi za mang'amung'amu, bila taimingi unaweza kuvuna mabua. Mungu atusamehe nyakati nyingine.
 Haya ni mambo ya kawaida, lazima kuweka grisi kwenye chombo ili kulainisha mitambo. 
 Naam. Ndilo shamba langu hili, ninapowaambia nimekuwa mkulima mdogo watu hawaamini.
 
Kazi inaendelea. Yakiiva nitawaalika. Nimepanda mahindi na maharagwe. Karibu Iringa wadau.

No comments:

Post a Comment