Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 22 February 2014

JAMBO SQUAD YAWAPAGAWISHA WAKAZI ARUSHA

Na Mwandishi Wetu, Arusha

WASANII maarufu ambao wamefanikiwa kufanya vizuri katika soko la muziki wa kizazai kipya maarufu kama Jambo  Squard mwishoni mwa wiki walipagawisha vilivyo mashabiki wao katika uwanja wa sheikh Amri Abeid  jijini Arusha.

Wasanii hao ambao walisindikizwa na kundi zima la Balance Diet lililopo jijini hapa walipiga shoo ya kukata na shoka wakati kituo cha redio 5 kilichopo jijini Arusha kufungua mwaka na mashabiki wao kutoka mikoa ya Arusha,Kilimanjaro na Manyara.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa kituo hicho Robert Francis meneja mbunifu wa kampuni ya Tan Communication Media Vicky  Mwokoyo alisema kuwa wameamua kufanya tamasha hilo ili kuwawezesha mashabiki wa kituo hicho na mashabiki wa Jambo Squard kupata buradani katika viwanja hivyo ambayo kwa muda mrefu hawakuipata.

Hata hivyo alisema kuwa tamasha hilo ni kama kufungua mwaka na kurudisha burudani na mapenzi yao kwa mashabiki wao kama ambavyo mashabiki wamekuwa wasikilizaji bora   kituo hicho ambacho kwa sasa kimekuwa na kutanuka karibu mikoa yote ya Tanzania.

Mbali na hayo pia meneja huyo aliongeza kuwa  kwa mwaka huu 2014 watakuwa na matamasha mengi lengo likiwa ni kutoa burudani na kuwa na desturi ya kukutana na mashabiki wao ikiwa ni moja ya kufahamu vitu gani wanaihitaji zaidi lakini pia kuwawezesha mashabiki wote kupata burudani zaidi hata wale wa hali ya chini kwa kuweka viingilio ambavyo havitawanyima mashabiki wengine kukosa burudani

“tutakuwa tunafanya mara kwa mara matamasha kwa mwaka huu tumejipanga lengo ni kutoa burudani zaidi nakuwawezesha wote kushiriki hata wale wa mashabiki wetu wasiojiweza nao ni sehemu yetu na ni lazima wapate burudani”alisema Vicky

Mbali na wasanii hao wa Jambo Squard kupiga ambayo ama kwa  hakika mashabiki waliridhika wasanii wengine wengi walipata fursa ya kuonesha vipaji vyao kama Spark,na Kundi la balance Diet linaloundwa na vijana watatu.

No comments:

Post a Comment