Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 15 February 2014

NCHI ZENYE UWEZO ZATAKIWA KUSAIDIA NCHI MASKINI


Na Mwandishi Wetu, Arusha

IMEELEZWA kuwa endapo kama nchi zenye uwezo wa kifedha zitaweza kusaidia nchi maskini  ambazo hazina uwezo wa kifedha kwenye masuala ya majanga ya mabadiliko ya tabia nchi basi tatizo hilo litaweza kupungua kwa kiwango kikubwa sana duniani na hivyo kufanya hata sekta mbalimbali kuwa na uwezo wa kusaidia jamii.
Kwa sasa asilimia kubwa ya nchi ambazo zinakabiliwa na changamoto hiyo ya majanga ya mabadiliko tabia nchi zinashindwa kupiga hatua kwa kuwa hazina uwezo wa kifedha wa kutosha kuwasaidia wananchi wake

hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati ya dunia ya sayansi ya mabadiliko tabia ya nchi Bw Richard Muyumbi wakati akiongea na wadau wa masula ya mabadiliko ya tabia ya nchi mapema jana jijini Arusha 

Muyumbi alidai kuwa suala la mabadiliko tabia ya nchi linakuwa gumu sana kuweza kumalizika kwa haraka kwa kuwa baadhi ya nchi hazina uwezo wa kutenga fungu kubwa sana la kupambana na majanga hayo ya nchi hali ambayo inaongeza sana kasi ya madhara 

Alidai kuwa kama watafanya hivyo ni wazi kuwa dunia ya sasa itapunguza sana madhara ambayo yanatokana na suala hilo ambapo pia hata rasilimali za msingi nazo zitaweza kuwanufaisha walengwa 

wakati huo huo alizitaka hata Nchi nyingine nazo kuhakikisha kuwa mbali na kuweza kuweka mikakati mbadala ya kupambana na mabadiliko tabia nchi lakini pia ziweze kuweka mikakti ya kutafuta teknolojia mbadala kwa wananchi 

Amedai kuwa kwa kuweka teknolojia kutaweza kupunguza tatizo hilo kwa kiwango kwani kwa sasa asilimia kubwa ya wananchi wakumbana na majanga hayo ya mabadiliko tabia nchi kwa kuwa hawana teknolojia za kutosha .

No comments:

Post a Comment