Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 28 February 2014

MWEKEZAJI MERU AVAMIWA


Na Mwandishi wa Brotherdanny5.blogspot, Arusha

ZAIDI ya wananchi 200 kutoka katika Kijiji cha Karangai Kata ya Mbuguni Wilyani Meru Mkoani Arusha wamevamia shamba la Mwekezaji wa kampuni ya Tanzania Plantation na kuharibu mazao, sanjari na kuchoma nyumba moto kwa madai kuwa wanataka kumiliki ardhi yao.

Akiongelea suala hilo Meneja wa kampuni hiyo ya Tanzania Plantatio Andrew Slaa alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa nne za usiku ambapo wananchi walivamia makazi ya mwekezaji wao na kisha kuharibu mali ambazo thamani yake bado haijajulikana mpaka sasa.

Slaa alisema kuwa hataivyo wananchi hao walikuwa na silaha za jadi waliweza kutekeleza ahadi walizopewa na viongozi mbalimbali wa Kata hiyo akiwepo Diwani wa kata hiyo kuwa wanatakiwa kupewa ardhi yao.

"hivi karibuni wanasiasa walidai kuwa muwekezaji huyu ambaye anafanya kilimo katika mashamba haya hayupo kwa mujibu wa sheria kwaiyo hii ardhi ni mali yao na kutokana na kauli hiyo wananchi sasa juzi waliamua kuingilia kati na kisha kuharibu mali za huyu mwekezaji huku wakidai kuwa ardhi yote ambayo ni zaidi ya hekari 2000 ni mali yao"aliongeza Slaa 

Alisema kuwa wao kama watendaji wakuu wa kampuni hiyo tayari wanamipango lakini hata mikakati ya kuhakikisha kuwa wanakuwa na ujirani mwema na wananchi lakini wananchi nao wanakiuka sheria za uwekezaji na kisha kusababisha hasara kubwa 

Aidha kwa upande wa Mwekezaji mkuu wa kampuni hiyo Tanzania Plantation,Bw Pkadeep Lodhia alisema kuwa wananchi hao wamesababisha uharibifu mkubwa sana wa kuchoma nyumba , lakini pia kuharibu mbogamboga ambazo zilikuwa zimerpandwa kwa makusudi ndani ya eneo hilo 

Alisema kuwa mara nyingi sana amekuwa akitishiwa maisha na wananchi hao ambao wakati mwingine humwambia kuwa amepora ardhi yao na hivyo hata kufikia uamuzi wa kutaka kumchoma yeye na gari lake jambo ambalo ni shinikizo kubwa la wanasiasa.

"mimi naogopa hata wakati mwingine kufanya kazi zangu ndani ya shamba hili kwani kuna saa ambazo nanusurika kufa kwa ajili ya wananchi wananitishia maisha lakini sio mimi tu hadi wafanyakazi wangu lakini mpaka sasa nimeshapata hasara kubwa sana ya Mamilionhi ya fedha kutokana na uharibifu huu wa mali"aliongeza Lodhia 

Pia alisema kuwa anaiomba mamlaka husika kuhakikisha kuwa wanafanya uchunguzi wa kikamilifu zaidi yake na shamba lake lakini pia hata kuweza kuwachukulia sheria kali wanaosababisha uharibifu huo wa mara kwa mara kwani yeye ni mmiliki wa shamba hilo kuanzia mwaka 1995.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Munasa Nyirembe alisema kuwa Mwekezaji huyo yupo kwa mujibu wa sheria ya wawekezaji hapa nchini lakini wananchi nao wanapaswa kujua na kutambua kuwa wanachokifanya ni makosa tena makubwa na hivyo sheria itaanza kuchukua mkondo wake.

Naye Diwani wa kata hiyo ya Mbuguni,Thomas Mollel alisema kuwa kamwe hawezi kusiistiza uvamizi kwa mwekezaji huyo na kwa kusema hivyo anamuonea kwani sheria haiwezi kumruhusu kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment