Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 12 February 2014

YANGA WAIFUATA KOMOROZINE KESHO


YANGA SC inatarajiwa kuondoka kesho kwa ndege ya shirika la Precession Air kwenda Comoro kwa ajili ya mchezo wa marudiano Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Komorozine mwishoni mwa wiki hii.
Ofisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba taratibu zote za safari zimekamilika, ila idadi ya wachezaji wanaondoka bado hawajaipokea kutoka benchi la ufundi.
Yanga inaondoka kesho ikiwa na matumaini makubwa ya kusonga mbele, baada ya kuichapa Komorozine mabao 7-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Dar es Salaam Jumamosi.

Iwapo Yanga itahitimisha vyema kampeni yake hiyo, itakutana na mabingwa watetezi, Al Ahly mwezi ujao.    

<BIN ZUBEIRY>

No comments:

Post a Comment