Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 12 February 2014

KALI ONGALA AACHWA AZAM SAFARI YA MSUMBIJI, KIKOSI CHAONDOKA KESHO

Menaja wa Azam FC, Jemadari Said ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, Kali raia wa Uingereza mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) aliyekulia Sinza mjini Dar es Salaam, atakosa safari hiyo kwa sababu pasipoti yake imeisha.
Hata hivyo, Jemedari hakusema kama mtoto huyo wa mwanamuziki maarufu wa zamani nchini marehemu Dk Remmy Ongala kama ataungana na timu hiyo Msumbiji atakapomaliza matatizo ya pasipoti yake au la.
Azam FC iliyoanza kwa ushindi mwembamba wa 1-0 Jumapili Uwanja wa Azam Complex Jumapili, itaondoka kesho Saa 4:00 asubuhi kwa ndege ya Fast Jet hadi Johannesburg, Afrika Kusini ambako wataunganisha ndege ya shirika la Msumbiji kwenda Beira itakapochezwa mechi hiyo.
Azam itaondoka na wachezaji 21 ambao ni makipa; Mwadini Ali, Aishi Manula na Jackson Wandwi, mabeki Luckson Kakolaki, Erasto Nyoni, Malika Ndeule, Aggrey Morris, Said Mourad, David Mwantika, viungo Ibrahim Mwaipopo, Kipre Balou, Jabir Aziz, Salum Abubakar, Himid Mao, Khamis Mcha na washambuliaji John Bocco, Kipre Tchetche, Brian Umony, Seif Abdallah, Gaudence Mwaikimba na Ismael Kone.
Benchi la Ufundi litaongozwa na Kocha Mkuu Mcameroon, Joseph Marius Omog, kocha wa makipa Iddi Abubakar, Meneja Jemadari Said, Daktari Mkuu Mwanandi Mwankemwa, Mchua misuli Paul Gomez na mtunza vifaa Yussuf Nzawila.
Azam inahitaji sare yoyote baada ya ushindi wa 1-0 nyumbani ili kusonga mbele.
<BIN ZUBEIRY>

No comments:

Post a Comment