Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 13 February 2014

MZAMBIA AKAMATWA NA MTAMBO WA DOLA BANDIA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahamed Msangi.

Raia  mmoja wa Zambia amekamatwa mkoani hapa akimiliki mtambo wa kutengeneza fedha bandia pamoja na karatasi zinazotumika kama malighafi ya kutengenezea fedha hizo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahamed Msangi jana aliwaambia wandishi wa habari kuwa, mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi mjini Tunduma akiwa mpakani mwa Tanzania na Zambia.
Alisema uchunguzi unaonyesha kuwa mtambo uliokamatwa unatumika kutengenezea dola bandia za Marekani huku pia mtuhumiwa akikutwa akiwa na karatasi za kutengenezea dola bandia zijulikanazo kwa jina la ‘Black Dollar’.
Kamanda alisema mtu aliyekamatwa ni  mkazi wa Chingola nchini Zambia, ambaye mbali na kunaswa akiwa na mtambo huo pia alikutwa na vipande vya madini bandia ambayo bado hayajafahamika.
Alisema mtuhumiwa alikamatwa akiwa upande wa Tanzania baada ya askari wa Jeshi la Polisi kuendesha msako katika maeneo mbalimbali ya mpakani wilayani Momba.
Kwa mujibu wa Kamanda Msangi, taratibu zaidi za kisheria zinafanyika ili kumfikisha mahakamani sheria ichukue mkondo wake.
CHANZO: NIPASHE     

No comments:

Post a Comment