Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 22 February 2014

BARAZA LA MADIWANI LAWAFUKUZA WATENDAJI WAKE

Na Mwandishi Wetu, Arusha 

BARAZA la madiwani halmashauri ya wilaya ya Arusha limewafukuza kazi watumishi wanne huku mwingine akishushwa cheo baada ya kujiridhisha na uchunguzi uliokuwa unafanywa dhidi yao kwa madai ya kusababisha Halmashauri hiyo hasara kubwa sana
Aidha uchunguzi dhidi ya watumishi hao ambao wanne wanatokea kitengo cha fedha kilitokana na hasara mbalimbali ambazo zilitokea katika Halmashauri hiyo kwa muda mrefu
Akitangaza kuwafukuza kazi Mwenyekiti wa halmashauri hiyo ambaye Simon Saningo alisema kuwa wameeridhika kabisa kuwafukuza kazi watumishi hao baada ya kuunda tume ambayo ilidhibitisha hadharani kuwa wamesababisha haara kubwa kwa halmashauri hiyo
alidai kuwa hapo awali wakati wafanyakazi hao wakiwa kwenye kitengo cha fedha walikuwa wanakiuka maadili ya fedha za serikali na hata wakati mwingine kulazimika kula njama mbalimbali kwa ajili ya kutumia vibaya fedha za umma
"kila mara sisi tulikuwa tunapata hatin chafu kutoka kwa CAG lakini sababu tulikuwa hatuzioni baada ya uchunguzi tukabain kuwa kuna fedha nyingi zimetafunwa na watu wasio waaminifu hasa hawa ambao ni waaasibu,na tulipounda tume kwa kuwa sheria inaturusu ndipo tulipoweza kubaini kuwa wamehusika sana na hivyo sasa tunawafukuza kazi lakini pia hata kuwafikisha kwenye vyombo husika"aliongeza Saningo
Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo aliwatangaza waliofukuzwa kazi sanjari na kfikishwa kwenye vyombo vya dola kuwa ni pamoja na Method Bwela ambaye alikuwa mweka hazina,Andrew Bahati ambaye ni muhasibu,Careen Mwanga ambaye naye pia ni Muhasibu
Wengine ni pamoja na Dominika Mihale ambaye naye alikuwa ni muhasibu ambapo kwa sasa ameshushwa cheo, huku mtumishi mwingine ambaye ni Lucas Mwalusamba(Mfamasia wa Wilaya)kwa sasa naye badio anaendelea kuchunguzwa lakini uchunguzi utakapokamilika basi na yeye atachukuliwa hatua kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma
Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Fidelis Lumat aliwataka watumish wote wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa wanafuata maadili ya kazi na kuachana na tabia ya kuwa na tamaa za mara kwa mara
Lumato alidai kuwa wakati mwingine tamaa ndiyo inayosababisha watumishi kuingia majaribuni wakati wananchi nao wakiwa wanahitaji misaaada yao ya hali na mali.

No comments:

Post a Comment