Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 22 February 2014

POLISI ARUSHA YAUA MAJAMBAZI WANNE, MMOJA ATOROKA, ASKARI NAYE AJERULIWA


Na MWANDISHI WETU, ARUSHA

Polisi mkoa wa Arusha limeua watu wanne wanadhaniwa kuwa ni majambazi huku mwingine akikimbia, na askari mwingine kujeruliwa kwa risasi na majambazi hayo

Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus sabas alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa moja usiku ndani ya baa moja iyulikanayo  kwa majina ya Pama iliopo Makao mapya jijini hapa

Sabas alisema kuwa siku ya tukio majambazi hayo yalifika katika baa hiyi ya pama kwa malengo ya kuoanga njama za kwenda kuvamia kituo kimoja cha mafuta cha jijini hapa lakini nda ndipo wasamaruua wema walipotoa taarifa kwa jeshi hilo.

Alisema baada ya kupewa taraifa walifika katika eneo la tukio ambapo jambazi mmoja alihisi kuwa polisi wameshafika ndani ya baa hiyo na ndipo alipofyatua risasi tatu hewani ambayo iliweza kumjerui askari polis  mwenye nam ba F.1416 D/SSGT RICHARD ambaye alijeruliwa kwenye mkono wake.

Sabas alisema kuwa katika tukio hilo watu wane wanaosadikiwa kuwa ni majambazi ,na wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 25-35 ambao mpaka sasa hawajafahamika majina yao  waliuwawa katika majibizano ya risasi baina yao na polisi.

“baada ya hapo mapambano yalikuwa ni makali sana na tunaweza kusema kuwa askari wetu waliweza kuwadhibiti majambazi hayo kwa kuwa tayari mpaka dakika hiyo walikuwa wameshajeruliwa na risasi”aliongeza Sabas.

Katika hatua nyingine alisema kuwa wakati wakiwa njiani kuwapeleka hospitalini majambazi hayo kwa ajili ya kupata matibabu walifariki dunia ingawaje mpaka sasa hawajaweza kufahamuika majina yao wala makazi yao. Huku Jambazi mmoja naye akitoroka huku akiwa na silaha.

Hataivyo Sabas alisema kuwa katika eneo la Tukio Askarti liweza kukuta  Silaha  aina ya Bastola STAR  yenye namba 426460FNHPISTOLE MODEL KAL 7.65 ikiwa na risasi tatu  huku pia begi moja  la mgongoni lenye rangi nyekundu likiwa na risasi nne .

No comments:

Post a Comment