Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 12 February 2014

SILIMA AWATAKA WADAU KUCHANGIA UJENZI WA KITUO CHA ZIMAMOTO KIGAMBONI

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Pereira Ame Silima akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ujenzi wa Kituo cha Zimamoto Kigamboni.  Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mhe. Dk. Faustine Ndugulile.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Pereira Ame Silima amewataka wadau kuchangia ujenzi wa Kituo cha Zimamoto kinachotarajiwa kujengwa katika eneo na Navy Kigamboni ili kupeleka karibu huduma za zimamoto na uokoaji kwa wakazi wa eneo hilo.
Mheshimiwa Pereira ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ujenzi wa Kituo hicho inayoongozwa na  Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile ambapo wajumbe wengine walitoka makampuni ya Mafuta ya TIPER, Hass Petrolium na Lake Oil. Mkutano huo pia  ulihudhuriwa na viongozi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakiongozwa na Mkuu wa Jeshi hilo, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha.
Alisema pamoja na kuwa jukumu la zimamoto na uokoaji ni la Serikali lakini wananchi na wadau wengine pia wanapaswa kutoa michango yao ya hali na mali ili kuchangia katika kuhakikisha kuwa  raia na mali zao wanakuwa salama.
Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Mhe. Faustin Ndugulile amesema tayari eneo la ujenzi wa Kituo hicho limeshapatikana katika eneo la Navy Kigamboni na kuwa kamati hiyo imeshafungua akaunti ya kwa ajili ya ujenzi wa Kituo hicho.
Katika kikao hicho Kampuni za TIPER, Hass Petrolium na Lake Oil zimeahidi kuanza kuchangia kiasi cha shilingi milioni kumi kila mmoja ambapo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeahidi kutoa shilingi milioni kumi na tano. Kampuni nyingine za MOIL, KOBIL na World Oil pia nazo zilishaahidi kuchangia shilingi milioni kumi kila moja wakati wa vikao vilivyopita.
Kituo hicho cha Zimamoto kinachotarajiwa kujengwa Kigamboni ni muhimu kwa eneo hilo ambalo pia linatarajiwa kujengwa mji wa kisasa.

Imetolewa  na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment