Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 27 July 2014

TAMASHA LA MUZIKI WA CIGOGO LARINDIMA CHAMWINO IKULU, DODOMA

???????????????????????????????

Tamasha la saba la Muziki wa Cigogo 2014, lililoanza jana  Julai 25, kwenye kijiji cha Chamwino Ikulu, Mkoani hapa linarindima kwa kishindo na kufanya nji wote kuwa na shamrashara za aina yake.
 
Tamasha hilo ambapo jana lilizinduliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi,  linashirikisha vikundi zaidi ya 30 vikiwasha moto wa ngoma na muziki wa kitamaduni.
 
Kwa mwaka huu tamasha hilo ni la msimu wa  Saba (7) likifahamika kama (Wagogo music festival 2014)  lenye kauli mbiu  ‘Utamaduni na Amani’  linarindima kwa siku tatu na hiyo kesho Julai 27 linatarajia kufikia tamati.
 
Mkurugenzi mkuu wa tamasha hilo, Dk. Kedmon Mapana,  wa Kituo cha Sanaa Chamwino (Chamwino Arts Center-CAC) wandaaji wa tamasha hilo alisema wanatarajia Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, ndiye atakayelifunga rasmi tamasha hilo hiyo kesho.
 
“Kesho Julai 27, ndiyo tunafikia tamati na Mkuu wa Wilaya ya Chamwino anatarajia kuwa mgeni rasmi.” alisema Dk. Kedmon.
 
Tamasha hilo tokea kuanza kwake limekuwa katika mwangaza mpana wa kukuza na kuinua utamaduni wa Cigogo, ambapo kwa mwaka huu limeweza kukusanya wasanii zaidi ya 700 na wageni mbalimbali katika mji huo wa Chamwino Ikulu.
Aidha, alivitaja vikundi vinavyoshiriki tamasha hilo ni pamoja na kutoka Dodoma kuwa ni New Pendo, Yelusalem, Inueni mioyo, Yeriko, Nyota njema, Ushirikiano, Nyerere na Ebenezer.
 
Vikundi  vilivyo vijiji vya Wilaya ya Chamwino ni  Upendo (Kijiji cha Dabalo),  Imani, Sinai  (Kijiji cha Membe).  Mchungaji mwema, (Kijiji cha Nzali), Juhudi, Muhubiri (Kijiji cha Kawawa), Nyota njema, Safina, Ndagwa (Kijiji cha Msanga).
Msifuni (Kijiji cha Mlimwa), Nyota, Ufunuo (Kijiji cha Majeleko), Simba (Kijiji cha Mbele zungu) na Inueni mioyo (Kijiji cha Mgunga).
 
Vikundi kutoka Wilaya ya Kongwa imani ( Kijiji cha Mkutani), Faru (Kijiji cha Songambele) na  Safina (Kijiji cha Chigwingili), Pia  kikundi cha Uvuke na Upendo  (kutoka  Manispaa ya  Dodoma mjini).
 
Vikundi vingine ni Mandoo/Tasuba kutoka Bagamoyo  Mkoa wa Pwani, Nazareti (Dar es s Salaam), Muungano (Manyoni, Singida) na  Zanzibar.

SOURCE: FULLSHANGWE

No comments:

Post a Comment