Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 31 July 2014

NIMEPOTEZA JAMAA WAWILI KWENYE AJALI YA MOROBEST

Maiti zikiwa zimelala huku wananchi wakihangaika kutoa majeruhi kwenye basi la Morobest jana asubuhi.
Majeruhi wa ajali ya basi la Morobest lililogongana na lori Pandambili wakiwa kwenye Kituo cha Afya Kibaigwa.
 Basi la Morobest likiwa limechakaa baada ya ajali mbaya iliyotokea jana Jumatano, Julai 30, 2014 katika Kijiji cha Pandambili wilayani Kongwa.
 Lori lililogongana na basi la Morobest ambapo mabomba yanaonekana yakiwa yameanguka na kuliponda basi hilo katika ajali iliyotokea jana Jumatano, Pandambili wilayani Kongwa. Watu 17 walifariki dunia papo hapo na wengine 52 kujeruhiwa vibaya. (PICHA ZOTE NA JAPHET MALONGO)

Ndugu zangu,
Katika ajali ya jana iliyolihusisha basi la abiria la Morobest na lori kwenye Kijiji cha Pandambili wilayani Kongwa nimepoteza jamaa zangu wawili na wengine watano wamejeruhiwa vibaya sana.
Jamaa zangu walikuwa wakielekea Dar es Salaam wakitokea Mpwapwa, ambako walikwenda kusalimia ndugu na jamaa.
Tuwaombee kwa Mungu awapumzishe kwa amani na wale majeruhi Mwenyezi Mungu awajalie afya na uponyaji wa haraka.
Amina.

Daniel Mbega,
Iringa





No comments:

Post a Comment