Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 31 July 2014

NDANDA FC YAHITAJI ‘BUNDUKI MBILI’ KUJIKAMILISHA MAWINDO YA LIGI KUU

ndanda
Na Baraka Mpenja, Dar es Salaam

NDANDA FC ya Mtwara inaingia kambini leo kuendelea kujiwinda na mikikimikiki ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 inayotarajia kuanza kushika kasi septemba 20 mwaka huu.
Katibu mkuu wa klabu hiyo, Seleman Kuchele ameuambia mtandao huu kuwa kwa kiasi kikubwa wamekamilisha ripoti ya kocha wao aliyokabidhi baada ya kumalizika kwa ligi daraja la kwanza, na wamebakiza nafasi mbili tu za usajili.
“Sisi tunaendelea kuikamilisha ripoti ya mwalimu. Kocha alikuwa anahitaji wachezaji tisa na mpaka sasa hivi tumesajili wachezaji saba na wawili tupo katika mipango ya mwisho na kwasababu muda umeongezwa, tutakuwa katika wakati mzuri wa kukamilisha,” Alisema Kuchele.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

No comments:

Post a Comment