Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 29 July 2014

HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA NA MAMLAKA YA BONDE LA PANGANI WATAKIWA KUONDOA MIGOGORO

IMG_0628
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Binilith Mahenge

Na Mahmoud Ahmad, Arusha
 
Serekali imeagiza bonde la mto Pangani na Halmashauri ya Jiji la Arusha inapopima maeneo  kuhakikisha inawashirikisha wananchi ili kuondoa migogoro inayojitokeza ya kugmbea maji na kusababisha madhara makubwa ikiwemo uvunjifu wa amani.
 Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira, Dk. Binilith Mahenge, alipokuwa akihitimisha ziara yake baada ya kutembelea chanzo cha maji kinachomilikiwa na Shamba la Kahawa la Burka Coffee Estate Limited jijini Arusha.
Alisema Bonde la Mto Pangani na Halmashauri ya Jiji ni lazima kushirikiana wakati wa kupima maeneo yote ambayo ni vyanzo vya maji kwa kushirikisha wananchi ili kuondoa migogoro ya kugombea maji inayojitokeza mara kwa mara na kusababisha uvunjifu wa amani na uharibifu wa mali.
 Waziri alisema mara baada ya kupima ni lazima vijengewe na kulindwa ili wachache wasije wakageuza matumizi  na kusababisha walio wengi kukosa maji ambayo ni haki ya kila mmoja na pia maji ni uhai wa viumbe.hivyo chanzo hicho ni muhimu kitunzwe na kuboreshwa  kwa kuwa kinatumiwa na wananchi wengi wakazi waliopo jirani katika maeneoya Burka na Olasti
Alisema katika baadhi ya maeneo nchini kumekuwepo na migogoro kati ya wananchi na wawekezaji kugombea vyanzo vya maji hivyo umefika wakati maeneo yote ya vyanzo vya maji yakapimwa na kuwekewa taratibu na hivyo kuondoa migogoro inayojitokeza.
Kwa upande wake mkuu wa Bonde la Mto Pangani, Joel Lao, alisema inakadriwa miaka kumi ijayo  maji katika chanzo hicho yatapungua kutokana na ongezeko la watu, hivyo kuna haja ya kutafutwa chanzo kingine .
Alisema chanzo hicho kimeweza kutunzwa na kuwa cha kuvutia kwa mazingira kutokana na kuwa ndani ya Shamba ambalo linaendelkezwa na kulindwa hivyo kuzuia wavamizi wasiweze kuingia na kuendesha shughuli zisizo rasmi ambazo haziendani na uhifadhi wa mazingira.
Awali meneja wa shamba hilo Hamza Kassim, alisema  kuwa shamba hilo lilimilikishwa  chanzo hicho mwaka 2006 na Bonde la Mto Pangani na kuwekewa, mifereji ya maji kwa ajili ya umwagiliaji, waliwekewa  mita ya maji ili kuelewa kiwango cha matumizi ambayo hulipia huku wananchi wakitumia maji hayo bila mita hivyo haifahamiki kiwango cha maji wanachotumia.
Alisema kuwa  Shamba hilo limeendelea kukitunza chanzo hicho, na mwaka jana wananchi zaidi ya 400 waishio maeneo ya jirani ya chanzo hicho, ya Olasti na Burka, walivamia chanzo hicho kusababisha uharibifu mkubwa  kwa kisingizio cha kukosa maji.
Meneja huyo alisema maji yalipungua kutokana na ukame uliojitokeza kwa kipindi kirefu na hivyo wananchi walidhania kuwa wamenyimwa maji na shamba hilo na hivyo kuamua kujikusanya na kuvamia na kufanya uhalibifu  mkubwa wa mali.
Alisema shamba hilo linatumia chanzo hicho cha maji kwa shughuli za umwagiliaji wa kilimo cha Kahawa na maji mengine huwa yanaelekezwa kwa wananchi  na kunapotokea ukame maji hupungua jambo ambalo wananchi hudhania wananyimwa maji.
Meneja alisema kuwa  wamekuwa wakifanya mikutano mingi na wananchgi ili kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo wa maji lakini hadi leo hakujapatikana muafaka.
Kutokana na hali hiyo wanaomba msaada ili kuweza kupatikana kwa muafaka kati ya shamba hilo la mwekezaji na uongozi wa serikali za maeneo hayo .

Source Credit: Fullshangwe

No comments:

Post a Comment