Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 28 July 2014

MADAKTARI RUKWA WAONYESHA MFANO KWA KUCHANGIA DAMU KATIKA HOSPITALI KUU YA MKOA HUO

Sehemu ya damu iliyokuwa imechangiwa katika zoezi hilo.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dk. John Gurisha akipimwa kabla ya kuchangia damu katika zoezi lilioendeshwa na Shirika la Msalaba Mwekundu (Red Cross) katika kuchangia damu mkoani humo. Kumekuwepo na uhaba mkubwa wa damu katika Hospitali Kuu ya Mkoa wa Rukwa na vituo vingine, uhaba unaofikia nusu kwa nusu ikilinganishwaan kiasi kinachopatikana na mahitaji yaliyopo. Uhaba huo umesababishwa na mwamko hafifu wa wananchi kuchangia damu kutokana na hofu inayosababishwa na dhana potofu kuwa uchangiaji huo una madhara. Madaktari wa Hosptali Kuu ya Mkoa pamoja na watumishi wengine wa Serikali waliamua kujitolea ili kuonyesha mfano kwa wananchi waweze kuondokana na hofu hiyo na kujitokeza kuchangia damu kuokoa maisha ya Watanzania wanaohitaji huduma hiyo muhimu.
Baadhi ya madaktari wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Rukwa wakichangia damu.
Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Esther Kasegezya akichangia damu katika zoezi hilo.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Rukwa Dk. Samwel Marwa akipatiwa vipimo muda mfupi kabla ya kuchangia damu.
Dk. Marwa akichangia damu.
Mchangiaji baada kutoa damu hupata viburudisho ikiwemo vinywaji baridi na biskuti maalum.

(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa)

No comments:

Post a Comment