Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 28 July 2014

JUMUIYA YA WAZAZI KUPELEKA WAKAGUZI KWENYE SHULE YA LEGURUKI

index
Na Mahmoud Ahmad, Arusha

JUMUIA ya wazazi ya Chama cha Mapinduzi, taifa, imeahidi kupeleka timu ya wakaguzi ili kubaini watumishi ambao wamejinufaisha  na fedha za uendeshaji wa shule ya sekondari ,Leguruki iliyopo halmashauri ya wilaya ya Meru, inayokabiliwa na madeni mengi.
Hayo yamesemwa jana na Katibu wa jumuia ya wazazi mkoa wa Arusha, Daniel Mgaya, kwenye hafla ya uzinduzi wa mtambo wa umeme unaotumia nishati  ya jua,Solar kwenye shule hiyo, amesema kuwa makao makuu ya jumuia ya wazazi itatuma wakaguzi hao haraka mara baada ya sherehe ya sikuku ya Idd el Ftri.
Alisema kabla ya ufisadi uliofanywa na baadhi ya watumishi hao shule hiyo ilikua na uwezo wa kujiendsha pasipo kutegemea mchango wowote toka nje na kwamba hawatakuwa tayari kuona shule hiyo ikiadhirika huku ikijulikana wazi watu walioifikisha shule hiyo mahali hapo.
 Pia aliwatoa wasiwasi watumishi wa shule hiyo pamoja na wazazi juu ya uvumi kuwa shule imeshindwa kujiendesha na kwamba ipo katika hatua za mwisho za kufungwa na kwamba jumuiya yake haiko tayari kuifunga shule hiyo hivyo wazazi na watumishi waendelee kuiamini shule hiyo.
 “Wazazi pamoja na walimu wangu msiwe na wasiwasi shule hii haifungwi endeleeni kuchapa kazi na leteni watoto wenu shuleni ila ninachowaahidi baada ta ya sikukuu hii tutatuma timu ya wakaguzi kukagua mahesabu haiwezekani watu waibe fedha halafu wapite mitaani kutangaza shule imekufa na inafungwa”alisema Mgaya.
Aidha mkuu wa skull hiyo Emanuel Loyi alisema kuwa skulli hiyo imekuwa ikishindwa kujiendesha kutokana na deni kubwa la zaidi ya tsh million 24 hivyo ufungaji wa nishati hiyo uliofanywa na wafadhili kutoka nchini ubelgiji kutoka shirka la Energy Assintance na kugharimu kiasi cha tsh million 55 hivyo itaongeza kiwango cha ufaulu .
 Alisema madeni hayo ameyarithi kutoka kwa uongozi uliopita tangu mwaka 1991ambayo ni yale ya makato ya NSSF yaliyosababisha kufungiwa kabisa.Mzabuni wa chakula cha shule pamoja na mishahara ya walimu hali ambayo inashusha ari ya walimu kufanya kazi kwa bidii.
 Kufuatia hali hiyo Loyi aliuomba uongozi wa jumuiya hiyo kupitia kwa mgeni rasmi ambaye ni mwenyekiti wa jumuiya hiyo mkoa wa Arusha Bernard Murunya kwa niaba ya mwenyekiti wa jumuiya hiyo taifa Abdalah Bulembo kuandaa harambee ya kukusanya fedha kwaajili ya kulipa madeni hayo na mambo mengine ikiwemo kukamilisha ujenzi wa mabweni.
 Naye katibu wa wakuu wa skulli za sekondari mkoa wa Arusha Upendo Kakana aliiomba serikali ya Chama Cha Mapinduzi kusimamia sera yake ya uwekaji wa maabara katika kila shule za sekondari nchini ili kuweza kuinua zaidi kiwango cha elimu.
 Kwa upande wake mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi mkoani hapa Bernad Murunya aliahidi kufanyika kwa haraka kwa harambee hiyo iliyoahirishwa mwaka jana ili kuiondoa shule katika tatizo hilo la madeni sugu pamoja na kuboresha miundo mbinu yake ikiwemo umaliziaji wa mabweni.
 Aidha aliahidi kuboreshwa kwa miundo mbinu ya shule hiyo ili kuongeza kiwango cha wanafunzi ambapo tayari katika suala la taa limeshapatiwa ufumbuzi kupitia msaada huo na kilichobaki na ujenzi wa darasa la kompyuta kwaajili ya walimu kufundishwa ili nao wawafundishe wanafunzi wao.
 Watumishi wanaodaiwa kuondoka shuleni hapo ni pamoja na aliyekuwa mhasibu,mwalimu mkuu aliyegombea udiwani  na walimu wengine.

CREDIT: FULLSHANGWE

No comments:

Post a Comment