Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 28 May 2014

TAARIFA YA WIZARA KUHUSU ZAWADI ZA WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI 2013



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

TAARIFA KWA UMMA

UFAFANUZI KUHUSU ZAWADI KWA WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI KATIKA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI MWAKA 2013

Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kilifanyika tarehe 10 Mei, 2014 katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma ambapo tuzo mbalimbali zilitolewa zikiwemo za fedha na zile zisizo za fedha kwa makundi tofauti tofauti.

Tuzo ya fedha taslimu ilitolewa kwa wanafunzi 30 waliofanya vizuri katika mtihani wa mwaka 2013 ambapo wanafunzi watano bora wasichana na watano bora wavulana waliofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kumaliza Elimu ya Msingi walipata shilingi 125,000/=, Wanafunzi watano bora wasichana na watano bora wavulana waliofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kumaliza Elimu ya Sekondari Kidato cha Nne walipata shilingi 250,000/= na Wanafunzi watano bora wasichana na watano bora wavulana waliofanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya kumaliza Elimu ya Sekondari Kidato cha Sita walipata shilingi 500,000/=. 

Fedha hizi zilitolewa na serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja na Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China na zilitolewa kama fedha taslimu. 

Aidha, fedha nyingine taslimu iliyotolewa ilikuwa ni Hundi ya Shilingi 3,000,000/= kwa walimu wa shule 60 zilizoongeza ufaulu katika mtihani wa mwaka 2013.

Pamoja na fedha taslimu za shilingi 250,000/= wanafunzi 10 wa Kidato cha Nne walipewa vocha za thamani ya shilingi 500,000/= kwa ajili ya kununulia vitabu vya kiada na ziada.

Aidha, Wizara imeamua kuwakabidhi wanafunzi 10 wa Kidato cha Nne fedha taslimu Sh. 500,000/= badala ya vocha ili wanunue vitabu wao wenyewe. Hii ni kwasababu wanafunzi hawa wanaweza kujiunga na Kidato cha Tano katika tahasusi (combination) mbalimbali na ni vyema wakanunua vitabu kulingana na tahasusi zao.

Katika kutoa zawadi hizo yamejitokeza mapungufu kadhaa ambayo yalisababisha usumbufu kwa baadhi ya wanafunzi na wazazi wao waliofika Dodoma kupokea zawadi hizo. 

Wizara inaomba radhi kwa wanafunzi na wazazi hao kutokana na usumbufu uliojitokeza. Aidha, matatizo yaliyojitokeza yameshatatuliwa.

Prof. Sifuni E. Mchome
KATIBU MKUU
26/5/2014

No comments:

Post a Comment