Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 30 May 2014

SHUKRANI: PRIVATE BRIAN SALVA RWEYEMAMU

PRIVATE BRIAN SALVA RWEYEMAMU
27.12.1987-15.05.2014
Familia ya Bwana Salva Rweyemamu na Bibi Isabella Kafumba Rweyemamu wa Kinondoni, Dar Es Salaam inayo heshima kubwa kutoa shukrani za dhati kabisa kwa ndugu, Jamaa na marafiki ambao walishiriki kwa namna moja ama nyingine kufanikisha msiba, mazishi na hatimaye matanga ya mtoto wao mpendwa, Brian Salva Rweyemamu aliyefariki dunia alfajiri ya Alhamisi ya Mei 15 kwenye Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo na kuzikwa katika Makaburi ya Kinondoni, Jumamosi Mei 17, 2014.
Kwa vile waliotuunga mkono na kutufariji wakati wa kipindi hiki kigumu cha msiba huu mkubwa ni wengi na ni vigumu kuwataja wote kwa majina, Familia, inapenda kwa heshima na taadhima nyingi kutoa shukurani za jumla ikiwaomba wote mkubali kuzipokea shukurani hizo kwa moyo ule ule kama mlivyotuunga mkono. Mmetufariji sana. Mmekesha nasi, mmeshinda nasi, nyote mmekuwa kimbilio salama kwetu wakati wa kipindi hiki kigumu. 
Mmeonesha upendo wa kweli kweli kwetu kama Familia na kwa mwanetu Brian ambao angerejea kwenye uzima tena, naye bila shaka yoyote angetoa shukurani za dhati ya moyo wake.
                        Hata hivyo, tunapenda kutoa shukurani kwa makundi machache ya marafiki ambao mchango wao utabakia kwenye nyoyo za wazazi wa Brian Rweyemamu tukianza na majirani na marafiki wa karibu wa Familia ambao mchango wao kamwe hautasahauliwa.
Familia pia inapenda kuwashukuru viongozi na wanajumuia wa Jumuia ya Mtakatifu Clara, Kanda ya Mtakatifu Bernadetta, Kinondoni A na Parokia na Kwaya ya Mtakatifu Martin de Pores ya Mwananyamala ikiongozwa na Baba Paroko Phocus A. Massawe kwa huduma kubwa za kiroho wakati wa msiba huo mkubwa uliotufika.
Familia vile vile inapenda kutoa shukurani za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mama Salma Kikwete kwa ushiriki wao katika msiba wetu ambao wameuelezea kama msiba wao pia. 
Tunaishukuru mno Ofisi Binafsi ya Rais (OBR), Ikulu, kwa mchango wake katika kufanikisha mazishi ya Brian na kwa jitihada za watumishi wake katika kuifariji na kuipa nguvu Familia yetu. 
Aidha, tunatoa shukurani kwa wafanyakazi na uongozi wa Ikulu ukiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Katibu Mkuu, Ikulu, Bwana Peter Ilomo. Mchango wenu, wa jumla na wa mfanyakazi mmoja mmoja, ulitufariji kupita kiasi na daima tutaendelea kukumbuka ukarimu wenu. 
Tunaishukuru pia Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) na watumishi wake kwa ushiriki wao wa kutupoza na machungu yetu.
Tunaushukuru sana Uongozi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, waajiri wa Brian kwa jitihada kubwa za kujaribu kuokoa maisha ya mwajiriwa wao na hatimaye kuunga mkono jitihada zote za mazishi yake. Tunamshukuru Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange, tunaushukuru uongozi wa Hospitali Kuu ya Jeshi, Lugalo ukiongozwa na Brigedia Jenerali Makere, madaktari na wauguzi pamoja na wasio na taaluma ya udaktari ambao kwa pamoja walihangaika mno kunusuru maisha ya Brian. Jitihada zao zilikuwa kubwa mno, lakini Mwenyezi Mungu alikuwa na mipango yake mwenyewe. 
Aidha, tunaushukuru uongozi wa Kikosi cha  Nyumbu Project cha Kibaha alikokuwa akifanya kazi Brian pamoja na wafanyakazi wake wote kwa kushiriki kikamilifu kwa hali na mali kuhakikisha kwamba wanamuaga na kumlaza mwenzao katika nyumba yake ya milele kwa heshima zote alizostahili.
Tunaushukuru uongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam na wakuu wote wa Wilaya chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Saidi Mecky Sadiq kwa uongozi wao na uelekezi sahihi wakati wa msiba huo.Aidha, tunawashukuru viongozi mbali mbali wa kitaifa – viongozi wastaafu, mawaziri, makatibu wakuu na waandamizi wengine wa Serikali kwa kutujali sana wakati wa msiba huo kwa kuwa nasi, ama kuwasiliana nasi kwa njia nyingine nyingi.
Pia tunashukuru uongozi na wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Shule ya Julius Nyerere – Mbezi beach, Kampuni ya Platinum Credit kwa ushiriki na  mchango wao katika shughuli hii kubwa. Aidha, Familia inapenda kuvishukuru vyombo vya habari, wanahabari na wanajumuia nzima ya habari kwa mchango wao katika kuwahabarisha wananchi kuhusu msiba huu. Tunawashukuru sana.
            Vile vile, Familia inawashukuru sana wanakijiji cha Kimbugu, Kata ya Katoke, Wilaya ya Muleba, Mkoa wa Kagera, kwa kuupokea vizuri na kuushughulikia kwa heshima zote za mila msiba wa mtoto wao Brian Rweyemamu. Kama walivyo wana-Kimbugu, tunawashukuru wana-Chato kwa kuupokea na kuumaliza msiba wa Brian kwa heshima na taadhima na Ibada kubwa iliyoendeshwa na Baba Paroko wa Parokia ya Kanisa Katoliki Chato, Fr Henry Mulinganisa, msimamizi wa uhakika na mhimili wa kiroho wa familia ya Mzee Bernard Kabululu.

Familia pia inayo heshima kubwa kuwajulisha na kuwakaribisha ndugu, jamaa na marafiki kwenye Hitma ya Msiba wa Brian Rweyemamu itakayofanyika kwa mkesha siku ya Ijumaa Mei 30, 2014 na kumalizia kwa Ibada itakayofanyika Kanisa Katoliki, Mwananyamala kesho (Jumamosi) Mei 31, 2014 kuanzia saa 12.30 asubuhi na kufuatiwa na kifungua kinywa na chakula cha mchana nyumbani kwa wazazi wake Brian – Kinondoni, mkabala na Vijana Hostel na Mango Garden, Dar es Salaam. 
Mnakaribishwa Nyote.

CREDIT: MICHUZI BLOG

No comments:

Post a Comment